Viongozi wa juu CHADEMA watofautiana

Viongozi wa juu CHADEMA watofautiana

Mie nilikuwepo ubungo plaza,niliingia saa sita na nusu mchana nikatoka saa nane kamili mchana.Nakiri kuwa kama chadema kinataka kukua basi Mbowe aachie ngazi! Huyu jamaa hana lolote kabisa,awaachie akina mnyika na wengine waongoze chama,ni mtupu ajabu

kwa hiyo kuingia kwako saa 6 na kutoka saa 8 kuna maana gani kuhusiana na kutofaa kwa Mbowe?
 
Juzi tu ulisema upo simiyu na wala hutaki kuckia cdm wala cuf or ccm leo tena unadai ulikuwa ubungo plaza? Ulidhani ule nimkutano wa UDP? Unaweza mlinganisha mbowe na john cheyo?
 
Porojo .....ukachaji lap top usijenyimwa posho,UPO KWENYE LIST WEWE NI MMOJA WA WALEEEEEEEEE MNAOLIPWA NA MAFISADI PAPA WA CHAMA TAWALA KILA SIKU ILI KUZIMA MAWAZO YA WEREVU HUMU,huna wa kumshawishi kwa hizi propaganda za enzi zileeeeeeeeeeee....
 
Watashauri nini? Wapotelee mbali kabisa, wamefanya kimekuwa kama waasi

Kamwe CHADEMA haitaendeshwa kwa mashinikizo ya MACCM na vibaraka wake, Bali CCM na vibraka wake ndio watakaoendeshwa kwa mashinikizo ya CHADEMA.
 
kwa hiyo kuingia kwako saa 6 na kutoka saa 8 kuna maana gani kuhusiana na kutofaa kwa Mbowe?

nadhani anataka kusema kuwa mbowe ni mweupe upstair kinachompa nguvu kwenye chama ni fweza yake na ile ishu ya baba mkwe ie mwenye chama
 
Mkuu, Mudi Mtoi, ni kweli mimi ni kipenzi cha EL, ndio maana nikampendekeza asimamishwe kama mgombea wa CCM ili atumike kama "pace maker" ili litimie lile neno "rais wa 2015" lazima atoke Kaskazini!".
Pia ni kweli naiabudu sana CCM ndio maana nikaisifu kwa kusema, CCM Imechokwa na mimi ndie mtu wa mwanzo huku kumsifu Mwenyekiti wa CCM kwa kumuita JK ni Kiongozi Dhaifu!, ndio maana ninawaabudia hata kina Chenge, Sitta na kina Mwigulu, huku nikiishutumu Chadema kila kukicha!.
Pasco.

Kaka Pasco.

Naomba tu nikiri kuwa kwa leo sija kuelewa kwa huu mchango wako! Ngoja niendelee kuwamini kuwa leo ni weekend huenda mtima wako umeelemewa na mvinyo wa kispaniola!

Ukikaa sawasawa na kuwaza kwa kutumia wallet ya EL utarudi kwenye sense zako. (Samahani), nayasema haya maana huwezi kumtenga EL na yote usiyo yaafiki.
 
Last edited by a moderator:
pamoja na heshima kwa mbowe lakini kwa sasa afanye apumzike, siasa za sasa zinahitaji uongozi wa vijana wasomi , afanye apumzike sambamba na slaa wabaki kuwa washauri
Unatoa maoni au unamwaga sumu?

Unatoa ushauri au unasambaza virusi?
 
Mie nilikuwepo ubungo plaza,niliingia saa sita na nusu mchana nikatoka saa nane kamili mchana.Nakiri kuwa kama chadema kinataka kukua basi Mbowe aachie ngazi! Huyu jamaa hana lolote kabisa,awaachie akina mnyika na wengine waongoze chama,ni mtupu ajabu
Tumbo lako litaendelea kukudhalilisha milele
 
Kauli ya Mwigulu imetimia Mbowe ana mtetea Gaidi Mwenzake kwa garama yoyote ile!

Ni lazima ujipime na kujichunguza akili yako mara mbili mbili kama bado zina akili, Sababu ukiona unaanza kuamini maneno ya Mwigulu basi ujue haupo salama kifikra.
 
Nimepoteza imani na huyu mh.zito.
Mwanzoni niliwapinga waliokuwa wakimtaja kuwa ni tatzo kwenye chama pia hana nia njema na chadema kamwe sasa nimekubari.
Huyu zto kwenye hili sakata la
Lwakatare hawezi kosa kwenye mkanda huo tena inaonekana atakua anahuska sana,kutekwa kwa Ulimboka skumskia hata akilaani tukio hilo leo anaandika barua kuwa lwakatare ajiuzuru nafasi alizonazo ili kupisha uchunguzi huru,hivi lwakatare ni nani katka serikali hii ambaye nafasi yake inaweza kuzuia ama kuathiri uchunguz wa vyombo huska kufanya kazi yao kwa uhuru?kwani Lwakatare ni waziri?katibu mkuu?usalama wa taifa?ktk serkali?kwa barua ya zto nimepata mashaka sana na mtu huyu kwani siamini kwamba anweza kuwa mvivu wa kufkri kiasi hicho na asitambue hayo.Ana mahusiano mazuri na baadhi ya viongoz waandamiz wa ccm tena ni kwa maslahi yake,na kwanini yeye anapenda kuwa kinyume na viongoz wenzke?Mnaomwamini zto nyie endeleeni mi acha nishukie njiani staki tena kumhusudu huyu dogo kwani akili yake sio.
 
pamoja na heshima kwa mbowe lakini kwa sasa afanye apumzike, siasa za sasa zinahitaji uongozi wa vijana wasomi , afanye apumzike sambamba na slaa wabaki kuwa washauri
Viongozi vijana wasomi kama Stephen Wassira na Samuel Sitta. Asante mkuu kwa ushauri
 
Mie nilikuwepo ubungo plaza,niliingia saa sita na nusu mchana nikatoka saa nane kamili mchana.Nakiri kuwa kama chadema kinataka kukua basi Mbowe aachie ngazi! Huyu jamaa hana lolote kabisa,awaachie akina mnyika na wengine waongoze chama,ni mtupu ajabu
.
Kweli wewe ni pilitoni na ubungo plaza nina uhakika hukuwepo kawadanganye watoto wenzio.
 
Mie nilikuwepo ubungo plaza,niliingia saa sita na nusu mchana nikatoka saa nane kamili mchana.Nakiri kuwa kama chadema kinataka kukua basi Mbowe aachie ngazi! Huyu jamaa hana lolote kabisa,awaachie akina mnyika na wengine waongoze chama,ni mtupu ajabu

Mhh!hii kali kabisa. Umeingia saa sita na nusu mchana. Halafu unakiri kama CDM kinataka kikue Mbowe awachie kina Mnyika kwa sababu ni mtupu.

Hapo umejenga hoja gani ili kutushawishi kwamba Mbowe anapaswa kuachia ngazi? Kama hujatuambia alichosema wala alichofanya, kuachia kwake ngazi na utupu wake uko wapi? Hivi akili yako ilikuwa inafikiria tu kwamba Mbowe aachie ngazi au una sababu za kweli?

Mbona sioni uhusiano wa kuingia kwako Ubungo Plaza saa sita na nusu na hoja ya kuachia ngazi? Ulitakiwa uandike kwamba ulipoingia saa sita na nusu uliona ..... au ulisikia ,... kutoka kwa Mbowe na hivyo unaona kwa hayo uliyoona anapaswa kuachia ngazi. Wewe hujawahi kuandika insha nini?
 
Viongozi vijana wasomi kama Stephen Wassira na Samuel Sitta. Asante mkuu kwa ushauri

wasira na sitta ni wenyeviti au makatibu wakuu wa chama gani? TUMIA FIKRA HURU , mwanadamu aliumbwa HURU jifungue minyororo ya kuataka watu wafikiri kwa niaba yako.
 
Back
Top Bottom