Viongozi wa juu CHADEMA watofautiana

Viongozi wa juu CHADEMA watofautiana

Taswira

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2012
Posts
1,198
Reaction score
452
Katika hali ya kushitua,Mh:mbowe akiongea na wanachi na wanachama wa chadema hii leo Ubungo plaza amesema
'Eti nashangaa kuna watu wanataka CHADEMA kimuache Lwakatare na kumsimamisha uongozi kwa uzushi uliopandikizwa na CCM, Hilo halitafanyika' - Mwenyekiti wa Chadema Kamanda Freeman Mbowe.

IKUMBUKWE siku chache zilizopita naibu katibu Mkuu wa CHADEMA Mh. Zitto Kabwe alitoa mapendekezo ya kuomba Mshitakiwa mkuu kwenye kesi ya Ugaidi ambaye ni Ndugu rwakatale mkuu wa usalama wa chadema awajibike kisiasa. Kuwajibika kisiasa ni pamoja na kuachia ngazi ya ukurugenzi wa usalama ili kupisha uchunguzi salama na kukiacha chama salama. Pia Lwakatare chama kijichunguze na shutuma zinazokikabili huku Lwakatare akiwa nje ya ulingo wa viongozi waandamizi wa chadema.

Hata hivyo katika hali ya kustaabisha barua ya zitto ilivuja wakati Zitto anadai ilikuwa ni barua ya siri kati yake na ofisi ya katibu mkuu wa chadema.

SASA
Kauli ya Mbowe hii leo kumkana zitto (kauli) mbeye ya wanachama wa chadema inaleta sura gani ndani ya chadema?

Je inadhihirisha hata ile barua ya mapendekezo ya Zitto ilivujishwa kwa maksudi kama njia ya kumpinga zitto?

Au kauli ya Mbowe ya leo inamkingia kifua katibu mkuu kutowajibika kwa kuvujisha barua kwa sababu barua haikubebe ujumbe wenye maana kwa chama na Lwaktare?
 
Nani na nani wametofautiana hapo?zitto alitoa maoni yake binafsi kabla ya kujua msimamo wa chama,mbowe kaweka wazi msimamo wa chama(zitto akiwa naibu katibu)shida iko wapi?
 
Mleta uzi unaonekana wewe ni kiazi sana. Kwani kuna tatizo gani hapo?

Yale yalikuwa ni mapendekezo ya Zitto na si uamuzi wa chama. Sasa kuna shidagani kama Zitto alitoa ushauri na chama kikasema hapa?

Kwani nilazima kila kitu anachosema Zitto chama kiaafiki? Kila mtu anamtazamo wake, hata Mbowe mwenyewe alikuwa na mtazamo tofauti na hiki alichokisema leo, lakini yote hayo yanaletwa kwenye kikao yanajadiliwa!

Uache utoto na ushabiki wa kijinga.
 
Mie nilikuwepo ubungo plaza,niliingia saa sita na nusu mchana nikatoka saa nane kamili mchana.Nakiri kuwa kama chadema kinataka kukua basi Mbowe aachie ngazi! Huyu jamaa hana lolote kabisa,awaachie akina mnyika na wengine waongoze chama,ni mtupu ajabu
 
We inaonyesha unaangalia upande mmoja tu. Mwalimu wangu mmoja aliniambia unapokwenda kwenye kikao chochote usiwe na majibu wala swali lolote, ila inatakiwa upate swali kulingana na hoja zinazojitokeza.

We unajua kikao kilichofanyika kiliadhimia kusimamia kesi ya Rwakatare zisimamiwe na chama. Pia, CDM imetoa mawakili wa kesi hiyo.

Sasa, maoni ya Zito yalikuwa maamuzi ya chama?

 
nitachangia baadaye,ngoja kwanza nipate Value maana naona hawa jama wanamtosa kamanda wangu ZZK kininja
 
Hivi ofisi ya Zitto na ya Slaa zipo kwenye umbali mkubwa kiasi gani? Dr. Slaa ni katibu mkuu na Zitto ni Naibu katibu mkuu. Hivi kulikuwa na sababu yoyote ya msingi ya Zitto kumwandikia barua Dr. Slaa? Kwanini hakwenda kuongea naye in person au asubiri vikao ambavyo yeye ni mmoja wa wapangaji wake ili atoe hilo pendekezo? CHADEMA hakuna utaratibu wa vikao vya dharura vya viongozi wakuu wa chama? Kwani hakuomba kikao cha dharura, na hasa kwa jambo kubwa kama hili?

Na kwanini barua ilivuja? Mbowe amegundua kwamba Zitto anataka kuwachezea akili. Na wanataka wamwonyeshe kwamba hawanunuliki kirahisi hivyo kwa pesa za mafisadi. Zitto anatakiwa atulize akili kidogo katika utendaji wake wa mambo. Asitafute sana kuonekana.
 
unajuaje wameshakaaa kikao ndani ya chama ........aisee nimesafiri tika mwanza kwenda arusha bara bara ina mashimo halafu waserikali wanajaza udongo kwenye hayo mashimo katikati ya lami lakini mvua nayo inayafukuwa kazi kweli.....hasa kutoka nzega kwenda igunga
 
Taswira.

Aliyesema Lwekatare awajibishwe sio huyo uliye mtaja wewe peke yake kwa mapenzi yako. Walio sema na kushauri kuwa Lwex atoswe ni pamoja na kipenzi cha EL na mtu anaye iabudu CCM isipokuwa spika wake, huyu ni Pasco.

Kwa maelezo yako, kwa kuwa mwenyekiti hajataja jina la ulie mtaja wewe, na kwa kuwa waliopendekeza na kushauri Lwex atoswe ni wengi ikiwemo ma-ccm, basi ki-mantiki hoja yako ya kusema kuwa "viongozi wa chadema watosana" haina mashiko na ni hoja inayo sadifu ombwe la kimantiki ndani yako.

Kwa kuwa umeamua kuliweka kwa mrengo ulioutaka wewe wa kuonyesha kuwa viongozi wa chadema wameanza kutosana, mimi mpenda chadema na mwanachama wa chadema ambaye naiona chadema kama tumaini jipya, nitafurahi kama njozi zako kwa viongozi wangu itatokea wakatosana kwa ajili ya maslahi ya chama(chadema).

Hata hivyo tambua kuwa Kutofautina kimawazo na kimtazamo ni moja wapo ya kiashiria cha afya ya ubongo na kushamiri kwa demokrasia kwenye chama.

Chama imara ni zaidi ya viongozi/kiongozi mmoja mmoja. Chama imara ni chenye wanachama wanao jitambua.
 
Last edited by a moderator:
wametofautiana nn, mbona zitto alishaukubali uamuzi wa chama na ndo huo aliosema m/kiti.....
 
Mie nilikuwepo ubungo plaza,niliingia saa sita na nusu mchana nikatoka saa nane kamili mchana.Nakiri kuwa kama chadema kinataka kukua basi Mbowe aachie ngazi! Huyu jamaa hana lolote kabisa,awaachie akina mnyika na wengine waongoze chama,ni mtupu ajabu
Bahati mbaya iliyo kubwa ni kwamba Mbowe hakuwahi hata siku moja kutoa kauli zake binafsi. Anayoyasema leo Mbowe ni makubaliano ya kikao cha kamati kuu ya CHADEMA iliyokaa tar 3&4 mwezi wa nne.
 
Zitto si jana tu kasema msimamo wake ndio huwo wa chama na msemaji ni Lisu sasa sijui nikubanwa haja kubwa au kuwashwa?????????
 
Hivi ofisi ya Zitto na ya Slaa zipo kwenye umbali mkubwa kiasi gani? Dr. Slaa ni katibu mkuu na Zitto ni Naibu katibu mkuu. Hivi kulikuwa na sababu yoyote ya msingi ya Zitto kumwandikia barua Dr. Slaa? Kwanini hakwenda kuongea naye in person au asubiri vikao ambavyo yeye ni mmoja wa wapangaji wake ili atoe hilo pendekezo? CHADEMA hakuna utaratibu wa vikao vya dharura vya viongozi wakuu wa chama? Kwani hakuomba kikao cha dharura, na hasa kwa jambo kubwa kama hili?

Na kwanini barua ilivuja? Mbowe amegundua kwamba Zitto anataka kuwachezea akili. Na wanataka wamwonyeshe kwamba hawanunuliki kirahisi hivyo kwa pesa za mafisadi. Zitto anatakiwa atulize akili kidogo katika utendaji wake wa mambo. Asitafute sana kuonekana.

pamoja na heshima kwa mbowe lakini kwa sasa afanye apumzike, siasa za sasa zinahitaji uongozi wa vijana wasomi , afanye apumzike sambamba na slaa wabaki kuwa washauri
 
acha ujinga juzi huko umagambani Mwigulu na Kagasheki wamepingana hadharani mbona hukuwafungulia uzi.?


hivi unaelewa maana ya mwenyekiti au unakurupuka tu.
1.chadema ipo makini kuliko serikali ya ccm
2.Chadema ipo makini kuliko usalama wa taifa.
3.Chadema ipo makini kuliko ccm yenyewe
Huyo ni Dr.Slaa leo ndani ya Ubungo Plaza kwenye uzinduzi wa kanda ya pwani.

wewe endelea kubweka kama wale wabunge wanaopiga kelele mwanzoni, mwishoni wanaunga hoja mia kwa mia.!!
 
Mie nilikuwepo ubungo plaza,niliingia saa sita na nusu mchana nikatoka saa nane kamili mchana.Nakiri kuwa kama chadema kinataka kukua basi Mbowe aachie ngazi! Huyu jamaa hana lolote kabisa,awaachie akina mnyika na wengine waongoze chama,ni mtupu ajabu

Ni yeye na utupu wake ndiyo aliye kifikisha chama hapa kilipo hadi mnakiogopa na kinawanyima usingizi.
 
Taswira acha uongo kwa hiyo amesema ana msema zitto?

Kwani hiyo barua una uhakika haukuvuja kabla ya kumfikia katibu mkuu?

Acha uchanganishi!
 
Last edited by a moderator:
Hivi ofisi ya Zitto na ya Slaa zipo kwenye umbali mkubwa kiasi gani? Dr. Slaa ni katibu mkuu na Zitto ni Naibu katibu mkuu. Hivi kulikuwa na sababu yoyote ya msingi ya Zitto kumwandikia barua Dr. Slaa? Kwanini hakwenda kuongea naye in person au asubiri vikao ambavyo yeye ni mmoja wa wapangaji wake ili atoe hilo pendekezo? CHADEMA hakuna utaratibu wa vikao vya dharura vya viongozi wakuu wa chama? Kwani hakuomba kikao cha dharura, na hasa kwa jambo kubwa kama hili?

Na kwanini barua ilivuja? Mbowe amegundua kwamba Zitto anataka kuwachezea akili. Na wanataka wamwonyeshe kwamba hawanunuliki kirahisi hivyo kwa pesa za mafisadi. Zitto anatakiwa atulize akili kidogo katika utendaji wake wa mambo. Asitafute sana kuonekana.

Dah! Mkuu pokea like yangu. And most likely ile barua (isiyo hata na saini) "ilivujishwa" humu JF na mwandishi mwenyewe siku moja baadaye akawatuhumu viongozi wenzake kwamba ndio waliofanya hivyo. Hizi siasa za majitaka za magamba kuna watu wanataka kuzilazimisha kwingine kwa sababu wanazozijua wenyewe. Kirusi halisi ni mwandishi mwenyewe.
 
Back
Top Bottom