Viongozi wa dini mkanyeni Makonda!!

Hilo neno kutoka kwa makonda wala silioni kuwa lina tatizo.

Simply amemaanisha kuwa yupo na Mwenyeezi Mungu na anasimamia haki.

Nakubaliana na wewe Faiza 100%, hao maadui wa Makonda wanataka kupotosha maana halisi ya kile alichokuwa anaelezea. Makonda yuko pale kuwatetea wanyonge wanaooonewa na hawa wenyeviti wa mitaa na maafisa ardhi ili wapate haki kama MUNGU alivyoagiza . Wanaomkashifu Makonda ni hao ambao wanafaidika na uhalifu wanaofanya kwa mfano wenyeviti wa mitaa ambao kwa kushirikiana na wajumbe wao huficha uhalifu; mfano ni huku Mbezi Beach A ambako walikamatwa wauza madawa ya kulevya na watu wenye silaha za vita!! Inashangaza pale ofisi ya mwenyekiti wa mtaa inapotumika kuwanyanyasa wale wanaowataja wahalifu hawa kwenye mikutano ya hadhara!!! Makonda hakikisha unawalinda hawa raia wema hapo ndipo wananchi watawasaidia polisi kulinda usalama wa raia.
 
Kunukuliwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akisema kuwa anapokuwa amesimama yeye basi anakuwa amesimama Mungu, kumeleta mfadhaiko miongoni mwa watu wenye akili timamu wanaojua nini inamaanishwa inaposemwa neno "Mungu". Lakini kauli hiyo pia imezifedhehesha dini zote zilizoko duniani.

Kila watu wakienda wanakoabudu wanaambiwa wanamuabudu "Mungu", halafu anasimama mtu na kusema akisimama yeye anakuwa amesimama Mungu, hili ni dharau kwa waabudu Mungu. Makonda anataka kusema yeye ni Mungu ama ni Mwakilishi wa Mungu?

Kama waislamu wanasema "hakuna apaswaye kuabudiwa ila ni Mungu pekee..." nao ndugu zao Wakristo wanasema "Mungu ni mwenye wivu.." inakuwaje wanakaa kimya mtu mwingine anapojifananisha na Mungu? Au viongozi wa dini nao wanaamini anaposimama Makonda anakuwa amesimama Mungu?

Ukimya wa viongozi wa dini juu ya kauli ya Makonda kuhusu Mungu unapalilia ile dhana kwamba viongozi wa dini Tanzania wana Shirika na viongozi wa Serikali wanaotokana na CCM. Maana kuna wakati watu waliuliza inakuwaje viongozi wa vyama vya upinzani huwa hawaalikwi kwenye yale matamasha ya "amani"? Kumbe inawezekana waandaji labda huwa wanaogopa kumuudhi Mungu kwa kuwaalika Mashetani.

Hata kama aliahidi kusaidia kujenga Makao Makuu ya BAKWATA ama alimtembelea Kadinali Pengo Ofisini kwake, ni lazima Makonda aonywe na akemewe hadharani kwa tendo lake la kujilinganisha na Mungu. Viongozi wa dini huo ukereketwa wenu wa CCM unawaondolea sifa ya kuwa viongozi wa dini kwani sifa mojawapo ya kuwa kiongozi wa dini ni kuzuia Mungu KUDHIHAKIWA!!
Amri ya kwanza ya Mungu unasema: Ndimi Bwana Mungu wako tusiabudu miungu wengine.
 
Ni sawa na mwana wa shetani binadaamu utajiringanishaje na Mungu amerudia tena leo
 
Wanachukua sadaka zetu, wanatuhimiza tutoe zaka na tuwe watu wema kwa kuwa Mungu anataka tuwe hivyo. Anakuja mtu anasema akisimama yeye anakuwa anasimama Mungu na viongozi wetu wote wa dini wako kimya. Kuna nini?
Sasa si mungu kasimama? Viongozi wa dini si wasimamia ofisi za mungu makonda bana?
 
Kunukuliwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akisema kuwa anapokuwa amesimama yeye basi anakuwa amesimama Mungu, kumeleta mfadhaiko miongoni mwa watu wenye akili timamu wanaojua nini inamaanishwa inaposemwa neno "Mungu". Lakini kauli hiyo pia imezifedhehesha dini zote zilizoko duniani.

Kila watu wakienda wanakoabudu wanaambiwa wanamuabudu "Mungu", halafu anasimama mtu na kusema akisimama yeye anakuwa amesimama Mungu, hili ni dharau kwa waabudu Mungu. Makonda anataka kusema yeye ni Mungu ama ni Mwakilishi wa Mungu?

Kama waislamu wanasema "hakuna apaswaye kuabudiwa ila ni Mungu pekee..." nao ndugu zao Wakristo wanasema "Mungu ni mwenye wivu.." inakuwaje wanakaa kimya mtu mwingine anapojifananisha na Mungu? Au viongozi wa dini nao wanaamini anaposimama Makonda anakuwa amesimama Mungu?

Ukimya wa viongozi wa dini juu ya kauli ya Makonda kuhusu Mungu unapalilia ile dhana kwamba viongozi wa dini Tanzania wana Shirika na viongozi wa Serikali wanaotokana na CCM. Maana kuna wakati watu waliuliza inakuwaje viongozi wa vyama vya upinzani huwa hawaalikwi kwenye yale matamasha ya "amani"? Kumbe inawezekana waandaji labda huwa wanaogopa kumuudhi Mungu kwa kuwaalika Mashetani.

Hata kama aliahidi kusaidia kujenga Makao Makuu ya BAKWATA ama alimtembelea Kadinali Pengo Ofisini kwake, ni lazima Makonda aonywe na akemewe hadharani kwa tendo lake la kujilinganisha na Mungu. Viongozi wa dini huo ukereketwa wenu wa CCM unawaondolea sifa ya kuwa viongozi wa dini kwani sifa mojawapo ya kuwa kiongozi wa dini ni kuzuia Mungu KUDHIHAKIWA!!

Labda wamekula maharage ya wapi sijuwi hawa!!???
 
Kama kweli katamka kauli hiyo, amekufuru sana inabidi amwombe msamaha Mwenyezi Ezi Mungu. Mwenyezi Ezi Mungu ni mmoja tu tena hana mfano.
 
Mungu wa Dar ana access na Ikulu muda wowote anaotaka
1481552116616.jpg
 
CCM inapofusha watu akili na utashi wao. FaizaFoxy mara kadhaa amekanusha wakristo kusema Yesu ni mwana wa Mungu lakini leo anaunga mkono Makonda kusema kwamba akisimama yeye anakuwa amesimama Mungu!! Kweli CCM imewajaza ujinga watu wengi sana ambao hata wengine huwezi kuwadhania!
 
Makonda anaomba sana Mungu amsaidie na kumlinda. Na hayo anayarudia sana katika hotuba.
Kitendo cha watu wazima na akili zao kuchukua tungo moja tata ya Makonda ambayo inaweza kutafsirika kinyume na makusudio yake kinaonyesha ana maadui wengi waliokereka na vita anavyopigana Makonda.
Shame on you all. Get a life!
 
Wanachukua sadaka zetu, wanatuhimiza tutoe zaka na tuwe watu wema kwa kuwa Mungu anataka tuwe hivyo. Anakuja mtu anasema akisimama yeye anakuwa anasimama Mungu na viongozi wetu wote wa dini wako kimya. Kuna nini?
Viongozi wa dini, tena zote, toeni kauli juu ya hili IKIWA KWELI MNA HOFU YA MUNGU, NA ILI TUENDELEE KUWAAMINI.
 
Alimaanisha mungu yupi, yule wa kwenye wimbo wa taifa au?
Sitaki kuamini kama mungu wa msikitini,yule wa makanisani na wale miungu wahindi ni kitu kimoja.
 
Kunukuliwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akisema kuwa anapokuwa amesimama yeye basi anakuwa amesimama Mungu, kumeleta mfadhaiko miongoni mwa watu wenye akili timamu wanaojua nini inamaanishwa inaposemwa neno "Mungu". Lakini kauli hiyo pia imezifedhehesha dini zote zilizoko duniani.

Kila watu wakienda wanakoabudu wanaambiwa wanamuabudu "Mungu", halafu anasimama mtu na kusema akisimama yeye anakuwa amesimama Mungu, hili ni dharau kwa waabudu Mungu. Makonda anataka kusema yeye ni Mungu ama ni Mwakilishi wa Mungu?

Kama waislamu wanasema "hakuna apaswaye kuabudiwa ila ni Mungu pekee..." nao ndugu zao Wakristo wanasema "Mungu ni mwenye wivu.." inakuwaje wanakaa kimya mtu mwingine anapojifananisha na Mungu? Au viongozi wa dini nao wanaamini anaposimama Makonda anakuwa amesimama Mungu?

Ukimya wa viongozi wa dini juu ya kauli ya Makonda kuhusu Mungu unapalilia ile dhana kwamba viongozi wa dini Tanzania wana Shirika na viongozi wa Serikali wanaotokana na CCM. Maana kuna wakati watu waliuliza inakuwaje viongozi wa vyama vya upinzani huwa hawaalikwi kwenye yale matamasha ya "amani"? Kumbe inawezekana waandaji labda huwa wanaogopa kumuudhi Mungu kwa kuwaalika Mashetani.

Hata kama aliahidi kusaidia kujenga Makao Makuu ya BAKWATA ama alimtembelea Kadinali Pengo Ofisini kwake, ni lazima Makonda aonywe na akemewe hadharani kwa tendo lake la kujilinganisha na Mungu. Viongozi wa dini huo ukereketwa wenu wa CCM unawaondolea sifa ya kuwa viongozi wa dini kwani sifa mojawapo ya kuwa kiongozi wa dini ni kuzuia Mungu KUDHIHAKIWA!!

NA YAKIMWENDEA VIBAYA, ANAENDA KWA HAO VIONGOZI WA DINI WAMSAIDIE KUMWOMBEA, HA HA HA!
 
Ninyi pia acheni unafiki ! Gwajima amejitokeza wazi na kumkosoa huyu bwana nyie wenyewe tena mkadai Gwajima hastaili kuitwa mtumishi was Mungu, hana hekima na busara nk. Sasa leo mna support hili bandiko tena!!!???
 
Back
Top Bottom