Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Wa kwangu Mwaka 1.7 hampendi Kunguru akimuona tu lazima amponde kwa mawe, Akilala usiku alafu Mvua akiwa inanyesha anaanza kulia "Mama Kunguru anakuja, Baba Kunguru anakuja" basi atalia weee mpaka Mvua iishe ndio analala! Najiuliza Hivi Kunguru alimfanya nini?mpaka leo sijapata jibu!

Alikuwa hafahamu kutamka vizuri neno Kikombe alikuwa anatamka "Kitombe"

Hapendi Ugali, Ukipika Ugali unaula mwenyewe. Yeye mpe wali hata kama ni kidogo kwake ni sawa tu!
 
mie wangu ana 6months,yeye tangazo likitokea lazima ainuke kichwa kulitazama,awe amelala lazima ataamka,likiisha tu anaendelea kulala.
 
Mtoto wa mama mwenye nyumba anampenda sana demu wangu akija lazima na chenyewe kitie timu.. kinanikoseshaga na kunicheleweshea mzigo
 
Wangu 2 years Jana anaangalia juu akaniambia (Baba nani anafua kule juu ona mapovu ni mengi)
Note: mapovu-mawingu
 
367991a0885520e4c6dfd019e4184ba3.jpg
 
Huyu dogo an 3Yrs

#1. Siku moja aliniambia "Baba nataka kuolewa"... Nikamuuliza unataka kuolewa na nani akanijibu " na wewe"..... Nikapigwa na butwaa.


#2. Siku nyingine akaniambia "Baba nina mimba".... Nikajifanya kama sijamsikia.


#3. Siku nyingine akaja na ua anaiambia "Baba ua la bibi harusi".

#4. Siku moja nilienda naye nyumbani akamuuliza baba yangu " Babu wazazi wako wapi?.... Baba akamjibu " wamefariki"... Dogo akasema "unaishi vipi bila ya wazazi".


Hayo ni machache

hahahaha jamani eti na ww atakuwa anakupenda sana babaake... they are so innocent yaani
 
Watoto katika hatua zao za ukuaji na kujifunza wanakuwa na mambo flani flani ya kufurahisha sana yaani mwanao anaweza kukuvunja mbavu balaa.
Mfano
1. Mwanangu (1.5years) anaweza kuwa anatazama TV akisikia unaongea na simu au umeweka music kwenye simu anakimbia kuja kuangalia simu hata kama TV ilikuwa na TV program ya katuni nzuri kiasi gani

2. Ukitaka alale we nenda kitandani weka music kwenye simu yako atakuja mwenyewe hata kama alikuwa anakwepa kulala

3. Anaheshimu simu yangu kama kituo cha polisi ila ya mama yake kashaipasua ukiiona utajua mama yake anafanya kazi idara ya miamba (geology)

4.Kupenda safari akiona mtu anatoka tu anaanza kuaga bye bye akijua nayeye anahusika na safari

5. Chakula kikiwa tayari, kabla sijaitwa kula yeye akiona mambo yako tayari anakuja kunipigapiga mgongoni(hajajua kuongea) akiashiria msosi tayari basi ukipotezea anaenda anarudi mpaka utakapoinuka

6. Mwanangu anatabia flani kama wivu, akiona naongea na mama yake mara nimemshika mkono tunaongea kama jambo la siri anakuja fasta analia anataka mama yake ambembe
Nadhani hajajua kwamba mama yake ni mke wangu

Hivi ni baadi ya vituko vya watoto mdau ongeza vya mwanao
Watoto wanaleta raha sanaaa
View attachment 521347
Wangu ni 3yrs now amewah kuniuliza nilimtoa wapi nkamdanganya nilimnunua dukan akakaa kimya kama dk 3 akanirushia swali tena "sasa baba mbuzi anapata wapi hela ya kununua mtoto".nlijikausha kama vle cjamsikia bahat nzur mama yake akamwita akanywe maziwa
 
Were mtoto nani kakhukwaruza hapa karibu na jicho?
Sijui.
Wangekutoboa jicho!
Shindwa baba sitoboki jicho. (5 yrs)
 
Wangu ni 3yrs now amewah kuniuliza nilimtoa wapi nkamdanganya nilimnunua dukan akakaa kimya kama dk 3 akanirushia swali tena "sasa baba mbuzi anapata wapi hela ya kununua mtoto".nlijikausha kama vle cjamsikia bahat nzur mama yake akamwita akanywe maziwa

Uongo una kikomo mkuu
 
Mwanangu 2.5 anapenda kujiremba akimuona mama yake kapaka poda mwenzangu anatafuta ngano ilipo
 
wa kwangu ana 3 yrs kila kitu kizuri kanunua baba yake yaani hata ukiwa unamlisha ukisema chakula kizuri atakwambia baba yake kapika yeye na babake hadi raha sijui ndio ule msemo mtoto wa kike na baba na wakiume na mama.
 
mtoto wa shemeji yangu miak 2 ni balaaa
anapenda niita dogo badal ya ba mdogo
Ukimkuta katoka kuoga tuu anajificha papuchi anakusemea mama dogo ananchungulia au utasikia mama kaka anamchungulia dada ake
ana vituko balaa kuna kitoto cha jiran anakipenda balaa anakiita mchumba kula lazm amtafte kuoga pia lazm
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom