Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,275
18,351
Watoto katika hatua zao za ukuaji na kujifunza wanakuwa na mambo flani flani ya kufurahisha sana yaani mwanao anaweza kukuvunja mbavu balaa.

Mfano

1. Mwanangu (1.5years) anaweza kuwa anatazama TV akisikia unaongea na simu au umeweka music kwenye simu anakimbia kuja kuangalia simu hata kama TV ilikuwa na TV program ya katuni nzuri kiasi gani

2. Ukitaka alale we nenda kitandani weka music kwenye simu yako atakuja mwenyewe hata kama alikuwa anakwepa kulala

3. Anaheshimu simu yangu kama kituo cha polisi ila ya mama yake kashaipasua ukiiona utajua mama yake anafanya kazi idara ya miamba (geology)

4.Kupenda safari akiona mtu anatoka tu anaanza kuaga bye bye akijua nayeye anahusika na safari

5. Chakula kikiwa tayari, kabla sijaitwa kula yeye akiona mambo yako tayari anakuja kunipigapiga mgongoni(hajajua kuongea) akiashiria msosi tayari basi ukipotezea anaenda anarudi mpaka utakapoinuka

6. Mwanangu anatabia flani kama wivu, akiona naongea na mama yake mara nimemshika mkono tunaongea kama jambo la siri anakuja fasta analia anataka mama yake ambembe. Nadhani hajajua kwamba mama yake ni mke wangu

Hivi ni baadi ya vituko vya watoto mdau ongeza vya mwanao

Watoto wanaleta raha sanaaa
 
Hahaaa. I could talk about my kids the whole day.

Yule mkubwa wa almost 5 years ni mpole na ana hurumaaa. Pia anapenda sana ufugaji na ameshajua kuchanganya vyakula vya kuku. Anawajua kuku wake wakiumwa, anajua kuandika numbers kwenye kila yai linalotagwa na kuliondoa bandani. Pia anajua kufatilia aina ya kinyesi cha kuku kama ni cha kawaida ama ni cha kuumwa.

Mdogo wake anaekaribia miaka 3 ni mtundu na mbabe. Yeye anapenda magari na ufundi. Yaani umuoneshe video ya magari kwenye simu imekula kwako huna jinsi ya kujitoa atakavyotupa tantrums.

Wengi hupenda kusema nampendelea yule mkubwa lakini sio kweli. Ni rahisi kumuonea kutokana na sura yake ya kipole na huruma aliyonayo so nikisikiaga nywiiii amelia basi nageukaga chui. Because the lil man can surely take care of himself.
 
Wangu ana 4yrs last week walikuwa kwenye exam ya midterm kwa elimu yake ya kindergarten sasa mwalimu akaandika vitu amabvyo hawajawahi kusoma aisee aligoma kuufanya huo mtihani mpaka akaenda mama yake siku iliyofuata ikabidi afanye kama special mbele ya mama yake na kumbembeleza kwa sana tu.
 
Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
 
Wangu ana 4yrs last week walikuwa kwenye exam ya midterm kwa elimu yake ya kindergarten sasa mwalimu akaandika vitu amabvyo hawajawahi kusoma aisee aligoma kuufanya huo mtihani mpaka akaenda mama yake siku iliyofuata ikabidi afanye kama special mbele ya mama yake na kumbembeleza kwa sana tu.
Kamanda in the making.. Safi sana.
 
Mi wangu aliona utabiri wa hali ya hewa kwamba mji tuliopo kesho utakuwa na mvua kesho yake ilipofika asubuhi ananiambia mama ule utabiri unadanganya mbona hakuna mvua wakati jana walisema kutakuwa na mvua.

Ikabidi nimwambie mji mkubwa huu hivyo mvua haiwezi kunyesha mji mzima kwa wakati mmoja.
 
Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
Mkuu dna yako imekaaje aisee hahaha ukija kuleta zako zipi watakupiga sana japo ni baba yao ila jiandae kwa kesi za kupiga wenzie
Napenda watoto wa aina hii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom