Kamakabuzi
JF-Expert Member
- Dec 3, 2007
- 2,904
- 1,364
Haya mambo yanakuwa na uzito kwenye rufaa. Kwenye rufaa mara nyingi huwa hakianzishwi kitu kipya, ndio maana utakuta rufaa inasema ..the judge/court erred in fact and in law..... Maana yake ni kuwa kitu kilishakuwa tabled kwenye mahakama lakini kikaamuliwa tofauti na matakwa ya sheria, hivyo unaomba kwenye rufaa....Adhabu yake ni shahidi kukataliwa, na shahidi akikataliwa madhara yake kwenye mwenendo wa kesi unayajua. Ndiyo maana upande wa mashtaka, Jaji na serikali wasingeweza kukubali shahidi huyu awekwe pembeni.
Imekua ni bora kusema "Hakuna ushahidi kwamba alikisoma kielelezo hicho wakati wa kutoa ushahidi kizimbani"
Hii hata kwa tusio wanasheria ina ukakasi. Wao wanasheria wanajua zaidi.
Usione hakimu anatoa uamuzi wanasimama na kuendelea, si kwamba wanakubaliana na uamuzi bali wanakubaliana kuendelea, kwa sababu wasipokubali kuendelea then kipengele hicho tu kiende kwenye rufaa kwanza. Ukienda hivyo utajikuta hadi mwisho huna cha kupeleka kwenye rufaa na rufaa yako inaweza kukosa muunganiko.