Ving'amuzi vya Continental kumbe hovyo kabisa!!

Ving'amuzi vya Continental kumbe hovyo kabisa!!

Habari zenu wakuu.
Nimevumilia sasa nimechoka aisee. Continental kama mmechoka basi tangazeni kufilisika na mfunge kurusha matangazo na kudanganya wateja.

Mlitoa ving'amuzi bila kadi. Baadae mkatangaza kuwa kadi ni bure. Ukifika kwenye ofisi zenu kadi mnauza 11,800/.

Hiyo inaweza kuwa sio ishu sana maana tunajua mnasaka hela.

Baada ya kutuuzia kadi siku hizi hapa Kibaigwa ndio hakuna kabisa matangazo yenu kwa antennae (external). Mwezi wa pili sasa mara muwe na channels mara hampo hewani.

Wakipigiwa simu hazipokelewi, emails hawajibh. Sasa sijui nini maana ya costomer care kwenu.

TCRA hawa jamaa sasa ishatosha. Maana sisi wenye ving'amuzi vyao badala ya kufurahia tunasikitika na kujutia kuwa navyo.

Naomba kuwasilisha.
Nisaidie namba zao mkuu
 
mi continental nliwasanukia kipind ile wanasema et ukishanunua huhitaj kuwa unanunua vfurush tena, et n bure... Mi nlijua tu haya yangetokea sabab dialo n mbabaishaji, kama star tv inamshnda kuendesha king'amuz ndo atakieza? af channel nyingi kwenye iko king'amuz et kaanzisha yeye, si ni uhun uo, Continental sio king'amuz
 
Najuta kugawa star times yangu.
Niligawa star times nikanunua continental, aisee hii kitu n majanga,
Channels



Well said mkuu,
Hata hii inatokea kila siku.
Kunasiku ntakipasua potelea mbali
Mi nnayo star times na nipo dar,anayekitaka aje pm nimpe,hawa jamaa ovyo kabisa,hamna bbc,cnn,citizen,sa wanataka tuangalie ma tangazo cha chama kwenye tv ya taifa!
 
Waliuza kwa ahadi ya ukishakinunua, hakuna haja tena ya kulipia channels, baadae wakaja na msemo, kakisajili ili upewe kadi, usipokisajili hautayaona matangazo yao.

Kwenda kukisajili, kadi inauzwa 12,000/= nikaona sawa (si unajua waTz tunamuachia Mungu tu), nikalipia kadi nikakisajili pale.

Ingawa bado tena channel zikawa shida kuonekana, kuwapigia simu, hawapokei, baada ya kusumbuka kuwapata siku 2 baadaye, wakanielekeza niende ofisini kwao Dsm - Wakakifanyia wajuavyo, kikaonyesha chaneli.

Nipo naangalia, baada ya wiki, wakaanza kutangaza kulipia kwa hiari vifurushi vyao kuanzia cha siku hadi cha mwezi, heee tooba baada ya siku 3 wanani-sms 'kifurushi chako kitaisha tarehe 03/03/2016' nikajiuliza kulikoni tena wakati sijalipia kifurushi chochote.

Tarehe 02/03/2016 jioni, nawasha tv holaa, na-search kwa njia ya manual kuanzia namba 424000--- haziji chaneli. Basi hadi leo kipo tu kila nikikiwasha labda walikosea, hakisomi.

Nilivyoelewa ni, WANALAZIMISHA KULIPIA CHANELI, wakati walituaminisha ni BURE ukishakisajili.

Bahati nzuri nina Startimes sebuleni, continental, kipo chumbani tu, ili nisisumbue wengine nikitaka kuangalia nikipendacho.

Hawa jamaa (continental decoder) HOVYO KABISA.

Ahsante!
 
duh bora ununue startimes dishi mkuu kwan kuna ndugu yangu anayo tangu anunue mwaka jana hajawah lipia na kuna channel 30 anatizama bure
 
Mimi nina uchungu nao hawa jamaa, najuta kununua king'amuzi chao
mimi nashauri leseni sheria na taratibu zinazosimamia mambo haya ziangaliwe upya. Kuna thread nyingine inawahusu Azam pia. TCRA kuweni makini vinginevyo mtakuwa mnashirikiana nao ktk uovu huu. Simaanishi wote ila inawezekana kuna vishoka au wafanyakazi wanaofaidika na utoaji mbovu wa huduma hizo.
 
Hawaendi na kasi ya maguful walizoea ila ya mzee wa msola
 
Tunawaomba TCRA watupe muongozo kama wanapitia post hizi za ving'amuzi tofauti tofauti mitandaoni ama kuzisoma na kusikiliza malalamiko kwenye vyombo vya habari.

Muongozo mdogo tu, tujue kama ni lazima kulipia hadi local channels ama la.

Maana watanzania wengi hatujui na kuishia kulalamika tu mitandaoni na kwenye vyombo vya habari tv, radio, na magazeti, bila kujua wapi pa kupeleka malalamiko haya, zaidi kama kawaida yetu huwa TUNAMUACHIA MUNGU TU.

Mamlaka ya Mawasiliano, tafadhali mtupe muongozo wananchi tujue, na siku zote mjue hata WAJINGA kuna muda unafika wanachoka kuwa WAJINGA.

Ahsante!
 
Mamlaka Ya Mawasiliano, siyo ya kuwa nawasakama binafsi, ila mtupe wananchi sisi, elimu juu ya ving'amuzi hivi kama tunavyolalamika humu na kwingineko huko.

Naamini mnasoma haya, mnayasikia haya, ila sielewi sijui kwa nini mnakaa kimya. Sitaki kuamini kama nanyi mnataka hadi mshtukizwe na kutumbuliwa ndiyo m-react.

Tunasubiria Majibu yenu, kwa karibu sana.

Ahsante!
 
Hii vita ya biashara inaenda kubaya sasa. Kila siku zinaibuka nyuzi za kuponda kisimbuzi kingine.
Jana nilisoma uzi wa kisimbuzi cha Azam, nadhani kesho nitasoma cha TING au Startimes au hata Easy au DStv.
Ni mwendo wa kuharibiana biashara tu hadi kieleweke.

Ova
 
Ooh ni Ile Ile ohhhh ni Ile Ile mtaisoma namba si ndio huyu aliyekuwa anaonesha mikutano ya mh?.
 
Hii vita ya biashara inaenda kubaya sasa. Kila siku zinaibuka nyuzi za kuponda kisimbuzi kingine.
Jana nilisoma uzi wa kisimbuzi cha Azam, nadhani kesho nitasoma cha TING au Startimes au hata Easy au DStv.
Ni mwendo wa kuharibiana biashara tu hadi kieleweke.

Ova
Ila mkuu umechunguza ukagundua kuwa yanayosemwa sio kweli au umeamua tu kutizama hili jambo kwa mtizamo huo? Kwahiyo watu wache kusema kuhusu king'amuzi A kwasababu tu jana kilisemwa king'amuzi B?

Tutaendelea kuibua madudu ya kila king'amuzi (kulingana na kila mtu anvoguswa) bila kujali kama kuna kingine kimekwishajadiliwa na hapa hakuna vita ya kibiashara ni kutafuta mtosheko kwa mteja.

Kuna ubabaishaji mwingi kwenye hivi ving'amuzi na TCRA tusaidieni walaji kupata huduma bora.
 
Ila mkuu umechunguza ukagundua kuwa yanayosemwa sio kweli au umeamua tu kutizama hili jambo kwa mtizamo huo? Kwahiyo watu wache kusema kuhusu king'amuzi A kwasababu tu jana kilisemwa king'amuzi B?

Tutaendelea kuibua madudu ya kila king'amuzi (kulingana na kila mtu anvoguswa) bila kujali kama kuna kingine kimekwishajadiliwa na hapa hakuna vita ya kibiashara ni kutafuta mtosheko kwa mteja.

Kuna ubabaishaji mwingi kwenye hivi ving'amuzi na TCRA tusaidieni walaji kupata huduma bora.

Mtosheko? Sidhani kama kuna kitu au mtu anayeweza mtosheleza kila mtu kwa wakati mmoja.
Kuna mtu alilalamikia channel za kisimbuzi cha Azam zinarudia movies sana.
Wakati hata DSTV nao ni mabingwa wa kurudia movies sana kuanzia za Hollywood hadi za Afrika.
Acha nikuache uendelee kutafuta mtosheko kwa hivi vifaa. Kila la kheri mkuu.

Ova
 
Nauliza kama naweza nikatumia antena nikadaka chanel bila shida kwa decoda iliyokuwa ya dish? antena bei gani? nipo mwanza meco.
 
Nauliza kama naweza nikatumia antena nikadaka chanel bila shida kwa decoda iliyokuwa ya dish? antena bei gani? nipo mwanza meco.
 
Achana na hao wahuni channels zina scratch na sasa hata zile channels tano za bure mpaka ulipie wamekuwa kama pay tv sijui tcra wanafanya kazi gani.
 
Hili tangazo na ndugu zangu wa Sahara Media Group linanichekesha sana.

Kama kuna tangazo linalopigwa zaidi kupitia station televisheni, basi hili limevunja rekodi.

Cha kusikitisha zaidi hawajui kwamba wamewauzi wateja wao kwa kuwazimia station zote mpaka zile zisizostahili kufungiwa yaani local chanel.

Wengi wetu tumerudi Startimes. Hasa sisi tulionunua ving'amuzi vile vya Startimes vya mwanzo kabisa, Ambavyo Local chanel ni Free.

Contnental Mwende mkajipange upya, tamaa zenu zimewaponza, kutaka kuwatesa wateja wenu kwa kuwafungia hata station za local?

Ndiyo maana mnapiga sana katangazo kenu kuwahamasisha wateja wenu, kwa sababu wamewachunia.

Kwisha habari yenu!
 
Back
Top Bottom