Ving'amuzi vya Azam kuanza kusambaa karibuni...

Ving'amuzi vya Azam kuanza kusambaa karibuni...

nasikia harufu ya nanihii vile, hebu ngoja kwanza!
 
Said Salim Bakhresa mungu ampe maisha marefu namkubali sana huyu jamaa
 

Miaka 50 ya Muungano kuna Mtanganyika yoyote aliyevuna MALI ZNZ na Pemba kama BAHRESA alivyovuna Bara?

Siku zote watanganyika ni wavivu, kazi majungu na wivu kwa watu. Tulimchamba sana Bahresa miaka 80 tukamuita lambalamba toto. leo tumejikuta watanzania wote m45 tunamtegemea yeye hakuna asiyemchangia angalau mia tatu kila siku. Huyo ndiyo mjasilia mali aliyekubali fedheha leo anaabudiwa.

TUFANYE KAZI KEYBOARD HAZILIPI
 

Unasema ni Mkombozi, kwa taarifa yako huyu ni bepari amekuja kukumaliza. Kama anatengeneza CHAPATI na sasa hivi akina mama majumbani wamekosa soko kwa sababu ya bidhaa zao kuingiliwa na AZAM kwa AZAM CHAPATI, AZAM TUI LA NAZI huyu anakusaidie wewe Mtanzania au anakuua???

Vitu vingine serikali imemwachia mno familia masikini zimezidi kudidimia kwa sababu yake. Kila kitu anataka yeye, jamani kuwe na breki wengine watafanya nini sasa??? UCHOYO HUO!!!
Wewe kweli ni kilaza unajua Azam wameajiri watu wangapi? wacha ushabiki
 
Tunamkaribisha sana na tunamhitaji sana.

Kaka Simiyu yetu Kwa mara yangu ya kwanza naona umepost nje na siasa. Sasa kwa hii post yako nani atalipa Buku 7 kama ilivyokawaida ya post zako?
 
Hakuna ki2 kibaya na chakuaibisha kama kushabikia mambo ya kusikia, mlianza na mabasi sijui mia 5, mnakuja na vingamuz.... kwani c analeta tu kama wafanyabiashara wengine? alete, asilete, atajua mwenyewe..... hii ndo bongo kila mtu mjanja! nae aseme ataanza na chanel 10 baadae had 60.!
 

Miaka 50 ya Muungano kuna Mtanganyika yoyote aliyevuna MALI ZNZ na Pemba kama BAHRESA alivyovuna Bara?

watanganyika mkienda zenji sheria si zinawabana mnadhani mtaweza kuvuna ivyo?
 
Isijekuwa kulazimishana kuwasikiliza magamba tuu, kwani Bharessa si ni mfuasi wa magamba.
 
Ishu ni hicho king'amuzi kitakuwa na chanels gani...kama kitajaza chaneli za kihindi na kiarabu hata afanye 500 kwa mwezi bado hataikonga audience tarajiwa.

Vinginevyo kama kitakuwa kizuri haya ndiyo mambo yanayotakiwa katika ulimwengu wa leo. Tumechoka na ugomvi na maringo ya akina Startimes na StarTv wanaojifanya kumonopolize biashara hii. Mtu unalipia king'amuzi kwa kujua kuna chanels fulani, kumbe kesho mwenye nayo akiota vibaya anaondoa na kuitesa jamii nzima.
 
Back
Top Bottom