Vimini makanisani

Wana JF kuna jambo limekuwa likinisumbua sana kwa siku nyingi. Kila niendapo kanisani huwa najaribu kuangalia dada zetu wanavyovaa na huwa najiuuliza maswali mengi sana. Nashindwa kuelewa kama wanaenda kuuza sura kanisani au wanaenda kusali. Mfano mzuri ni kanisa la chuo kikuu cha Dsm. Hapa kuna mabinti wanaovaa vimini na wanakaa viti vya mbele. Wanapofika huwa wanajitahidi kubana miguu na kuvutavuta vijimini vyao lakini kipindi kinafika wanachia waziii wananika mapaja na viskintight vyao na wengine skintight hazionekani kwa maana watakuwa wameva bikini. Sasa naomba wenye uwezo wa kutoa onyo kwa hawa kina dada watusaidie. Nafikiri makanisa yote yangeweka sheria kwamba ni marufuku mwanamke kuingia kanisani na nguo zinazovuka magoti. Hebu angalia kina mama wa kiislamu wanapoenda msikitini wanajifunga mahijabu na makanga mengi tu. Kwa nini wakristu wasiwe na kanuni na taratibu za mavazi ya kuvaa siku za ibada. Waache kuwatia Ibilisi wachungaji na mapadre kwa kupanua mapaja yao kwenye viti vya mbele. Naomba tusaidiane kupambana na hili. Thanks in advance. May Almighty Father guide you and bless you so that you can come up with good and reasonable ideas on how to handle this damned matter.
Ni kweli kuna wale wageni wasiojua kweli bado wanavaa isivyo, ila nawe maelezo yako inaonekana unachungulia kabisa na sio kuepusha macho usione ubaya wake. Jifunze hata ukiwa nje ya kanisa kuepusha macho yako kuangalia maeneo uliyotaja hata kama kavaa vizuri. Mfano unaweza hitajika kumhudumia dada, mama au ndugu wa kike asiyekuwa na fahamu na nguo zimemtoka au zinamtoka sasa wewe kama unajenga hii hulka utapata matatizo bure, tazama pembeni kabisa hata wao wakiona wanapuuzwa utaona wanaacha wenyewe.
 
Unajua kuwa watu hawajaenda kwenye nyumba za ibada kwa muda mrefu sana.
kwa hiyo siku anapoamua kwenda anashidwa kujua avae nini na afanye nini anavaa anavyotaka, lakini kwa sababu ndo muumini mchanga anapokelewa anapewa mafundisho mazuri analielewa neno, taratibu anaanza kubadilika mwenyewe bila kushurutiswa( hapa naongelea makanisa ya waliookolewa) na anaanza kufuata taratibu za kanisa.
 
Huyu jamaa wa hoja hamjamtendea haki hata kidogo. Hivi kwa akili zenu zote na madegree unaona kuvaa nguo inayovuka magoti kanisani ni sawa? Sasa hapa tusiongee uhuru wa mtu tuangalie fact. Kuna sehemu ngapi za starehe ambazo mtu anaruhusiwa kufanya anavyotaka au kuvaa vyovyote anavyotaka??

Kama hutamaniki mtaani kanisani ndiyo utaonwa? I like Musilims na sheria yao ya kufunika mwili hasa wanawake. Huu ubwege huukuti misikitini wala wapi? Utakuta kwa westernized church.

Mtake msitake hii hoja ni muhimu na msitetee ujinga, ukimuona mtu kavaa mini kanisani mpe live, hakuna uhuru hapo.
 
Unajua kuwa watu hawajaenda kwenye nyumba za ibada kwa muda mrefu sana.
kwa hiyo siku anapoamua kwenda anashidwa kujua avae nini na afanye nini anavaa anavyotaka, lakini kwa sababu ndo muumini mchanga anapokelewa anapewa mafundisho mazuri analielewa neno, taratibu anaanza kubadilika mwenyewe bila kushurutiswa( hapa naongelea makanisa ya waliookolewa) na anaanza kufuata taratibu za kanisa.


Kama hajui avae nini kwenda kanisani basi asivae kabisa huko kanisani napo watamfundisha kuvaa nguo.

Mbona wanaume hawavai kaptura wakiingia kanisani? Vipi wanawake wavae nguo fupi?

wanaovaa nguo fupi wanakwenda kanisani kuwakaza wenzao. ni mashetani lazima wakemewe
 
Unajua kuwa watu hawajaenda kwenye nyumba za ibada kwa muda mrefu sana.
kwa hiyo siku anapoamua kwenda anashidwa kujua avae nini na afanye nini anavaa anavyotaka, lakini kwa sababu ndo muumini mchanga anapokelewa anapewa mafundisho mazuri analielewa neno, taratibu anaanza kubadilika mwenyewe bila kushurutiswa( hapa naongelea makanisa ya waliookolewa) na anaanza kufuata taratibu za kanisa.

Kama hajui avae nini kwenda kanisani basi asivae kabisa huko kanisani napo watamfundisha kuvaa nguo.

Mbona wanaume hawavai kaptura wakiingia kanisani? Vipi wanawake wavae nguo fupi?

wanaovaa nguo fupi wanakwenda kanisani kuwakwaza wenzao. ni mashetani lazima wakemewe
 
Ni kweli maneno yako, naongezea hapo... Ukitazama na kutamani, umezini...!

Lakini vipi yule mwenye kumtamanisha mwingine... mpaka yule mtazamaji akajikuta akitamani kwa kule kutamanishwa na mtamanishaji!?

Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa
mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
1Tim 2:9
aha aha tujitahid kumshinda shetan
 
We Mateso! Sentensi yako umeianza vibaya, ukienda kanisani unakwenda kusali na kumwomba Mungu, sasa wewe unapata muda wapi wa kuangalia wasichana? Hayo mambo ya Macho hayana pazia ni excuse ya kizamani sana. Kama nia yako ni kusali huwezi kuangalia angalia wasichana, unless wewe pia unakwenda kuangalia madada.

Kuhusu wakina dada kuvaa nguo fupi mie naomba tu kusema kwamba, kila vazi lina mahali pake. Beach, disco, kazini, kanisani, etc. Kila mahali kuna mavazi rasmi, basi tujitahidi kuvaa kuendana na mazingira tunayokuwemo!
 
We Mateso! Sentensi yako umeianza vibaya, ukienda kanisani unakwenda kusali na kumwomba Mungu, sasa wewe unapata muda wapi wa kuangalia wasichana? Hayo mambo ya Macho hayana pazia ni excuse ya kizamani sana. Kama nia yako ni kusali huwezi kuangalia angalia wasichana, unless wewe pia unakwenda kuangalia madada.

Kuhusu wakina dada kuvaa nguo fupi mie naomba tu kusema kwamba, kila vazi lina mahali pake. Beach, disco, kazini, kanisani, etc. Kila mahali kuna mavazi rasmi, basi tujitahidi kuvaa kuendana na mazingira tunayokuwemo!
Maelezo yako niliyoya-highlight kwa rangi za blue na nyekundu yanajichanganya yenyewe. Tupe msimamo wako badala ya kumshambulia Bwana Mateso
 
Unaenda kuangalia wanawake kanisa la UDSM kwani ile TBS siku hizi imekufa? Pale ATB kwa nyuma,unatazama kule chini library, kwa mbele kuna kanjia kakuelekea kule faculty of law, kwa huku kuna pahali wanapanda ngazi wanakuja ARD etc, kwa kule kuna kanjia kanaelekea darajani then Daruso/posta. Kakae TBS uoshe macho mpaka uchoke sio kanisani bana!
Mkuu unanikumbusha mbali wewe
Nway tuyaache tu tuendelee na mada
Dah! Ila pale kweli ni TBS na hizi nguo zao
 
Ni mojawapo ya mitihani ya kuepuka dhambi.
just imagine hawakupo-hawavai vimini dhambi ya kutamani isingekuwapo.
piga moyo konde na utashinda
 
Pretty hao wa ughaibuni hawako sahihi kwa kila kitu.Hivyo basi siyo watu wakujilinganisha nao;kwasababu na wao wanakosea pia kama wewe unavyokosea halafu unataka kwenda nao sawa wakati na wao wanachemsha/kutokota kabisa.Naomba tuache kuwa wanafiki,sidhani kama kuna mahali katika maandiko na maadili katika sehemu husika yanakubaliana na hilo vazi!

lakini hao wa ughaibuni ndio wenye uwezo wa kubadilisha na kuvipitisha hivyo vipengele vilivyokuwa ndani ya Bible amabavyo wanavihisi haviendi na maisha ya kileo, huku kwetu ni kufuata mamuzi yao kwani hatuzimi wala hatuwashi ,hebu angalia masister wa miaka hiyo iliyopita mpaka kufikia mapema miaka ya Tisini 90 walivyokuwa wanajistiri mili yao leo utaona kuna masista wamekuwa wanaintateni ,angalia nini Bible hasa inasema kuhusu Gays and lizibiana halafu rudi jiulize nini imekuwa hadi jamaa hawa wanabadilisha hicho kipengele kwa amri zao ,ndani ya ukiristo zina imekatazwa lakini leo imefanywa kama vile sehemu moja wapoiliyokubaliwa ndani ya ukiristo ,sasa na hizo vimini tukubali walio tuletea dini sasa wanatuletea na hivi vivazi , itafika wakati watu wataigina na bikini ikiwa kisingizio ni joto.
 
Naona hujaelewa ninachozungumza wewe. Wewe ukiwa hata kwenye kikao huwezi kuona watu walivyovaa? Kama huna la kuchangia kaa kimya.
 
Siku hizi wanasali new lecture theatres nyuma ya library ATA & ATB sidhani kama zinatumika tena.
 
Hii ni RC. Nashukuru kama Lutheran wamefanyia kazi hilo. Haya ni maudhi japo wengine wanakejeli kuwa tunaenda kuangalia vimini au kusali. Inaniuma sana.
 
Hii ni tabia mbaya na lazima viongozi wetu wa dini na waumini wakemee na ikiwezekana wanaovaa vimini makanisani wafukuzwe.
 
Ningekuwa nafurahia nisingeandika hili. Natumaini wewe bado mtoto mdogo unayewazia ngono tu. Mimi huko siko kabisa. Jina la mateso halina uhusiano na mada husika. Think twice or more b4 replying to any post.
 
Vimini church ni kitu ambacho hakiingii akilini kabisaaa!
Unless kama wanaenda tafuta mabwana uko church.
Uongozi wa kanisa nao hauko makini as makanisa mengine kama RC sinza kuna akina mama wanakaa mlangoni ukija na kimini chako wanakupa kanga special ambayo ukiivaa watu wanajua umeshaharibu.

Alafu na nyinyi mnaosupport,hamjui nini maana ya kanisa ofcourse na kusali.
Huwezi concentrate kabisa kama huu mwanaume alafu umekaa na mdada mipaja nje unless kama umehasiwa bse icho ni kikwazo na Yesu anasema ingekuwa kheri uyo mtu afungwe jiwe la kusagia na atupwe baharini.
Akina dada mubadilike ofcourse na kina kaka pia as wapo ambao wanajilipua na pamba za kuexpose miili yao.
Church ni mahara patakatifu pa sala so whatever you do and dress should match with that theme not otherwise
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom