Yo Yo
JF-Expert Member
- May 31, 2008
- 11,217
- 1,706
Nasikitika kuona kaka zetu wakilalamika dada zao kuolewa na wazungu, wakati wao ndio wanasababisha.
Kwa ufahamu wangu kuanzia miaka10-11 iliyopita kiwango cha wadada wa kitanzania kuolewa na wazungu kimekuwa kikiongezeka kwa kasi kubwa huku kaka zetu wakibaki kusikitika bila kujua tatizo nini. Utasikia, "wewe na uzuri wote huo, umekosa nini kwenda kuolewa na mzungu."lol! Swali langu, ulikuwa wapi wakati niko single?...Unajua, kwa muda mrefu watu wengi wamekuwa wakihisi kuwa mwanamke yeyote anayeolewa na mzungu ana sifa ya umalaya, bila kuangalia upande mwengine wa shillingi kuwa si lazima iwe hivyo kama wengi wanavyofikiria. Hizi fikira hazina utofauti wa msemo wa kabila fulani wanakawaida ya kuwauwa wanaume zao kwa sababu ya mali, au kabila fulani wanakula mbwa! Samaki mmoja akioza basi sio wote hawafahi. Kadri siku sinavyozidi kwenda tumeweza kuona wadada wanaojiheshimu na wenye elimu bora wasio na sifa ya umalaya nao pia wanaoolewa na wazungu.
Kuna sababu nyingi sana za wanasichana wengi kuamua kuolewa na mtu mweupe. Kuna wanaona kuwa pale kuna uhakika wa maisha mazuri au kuna matumaini ya kuondokewa na maisha magumu, wengine wanaona wanajua kujali na wanauvumilivu, wengine lengo la kupata watoto chotala, kama sie kwetu usukumani binti mweupe anathamani ya kuchumbiwa kwa ng'ombe 40. Hivyo basi kila mtu na sababu zake.
Tukirudi kwenye upande wa sababu nyingine kuu ambayo pia kuna uwezekano mkubwa wa wadada wa kitanzania kukimbilia kuolewa na wazungu. Mara nyingi umekuwa ukisikia wavulana (wanaume) wakiwapondea mabinti wakitanzania kwa kuwaita majina mabaya kama vicheche, au hata kuwakosoa kwa kudai kuwa wanatabia mbaya. Ambavyo si lazima iwe kweli, wao usema hivyo kutokana na kujiridhisha nafsi zao, bila kujua dharau hizo zinajenga ukuta mkubwa wa kutenganisha uwezekano wa kukosa mke bora wa kitanzania. Na endapo utokea kuwaowa, bado uwadharau wake zao na kutegemea wao ndio waheshimiwe, bila kujua heshima utokana na heshima.
Unapomweshimu mtu nae hana budi kukuheshimu pia. Binafsi nina mfano hai kabisaaa,-yupo kaka mmoja ambaye anajulikana (superstar wa bongo). Huyu kaka ni mtu anayejiheshimu lakini anakawaida ya kusema "wasichana wa kibongo wote vicheche". Na alishawi kudiliki kuvunja uwezekano wa kuolewa kwa binti mmoja wa kitanzania. Kwasababu aliyekuwa muoaji ni best yake. Na huwa ana kawaida ya kusema hivyo hata kwa marafiki zake wa kike pia na wasichana anayetoka nao ambao wanajiheshimu, lakini kwake ni vicheche. Na na hakika wako vijana wengi wa namna hii, sasa hali hii sijui kama tutafika kama kaka zetu msipojirekebisha. -Oweni au acheni kulalamika!
All I wanna say is that, tujifunze kukubali vya kwetu. Vya kwetu ni vitamu na vizuri kuliko, hakuna sababu ya kuviponda kisa...kufurahisha nafsi zetu.
----
Hayo ni maneno ya Total Knockout!!
Kwa ufahamu wangu kuanzia miaka10-11 iliyopita kiwango cha wadada wa kitanzania kuolewa na wazungu kimekuwa kikiongezeka kwa kasi kubwa huku kaka zetu wakibaki kusikitika bila kujua tatizo nini. Utasikia, "wewe na uzuri wote huo, umekosa nini kwenda kuolewa na mzungu."lol! Swali langu, ulikuwa wapi wakati niko single?...Unajua, kwa muda mrefu watu wengi wamekuwa wakihisi kuwa mwanamke yeyote anayeolewa na mzungu ana sifa ya umalaya, bila kuangalia upande mwengine wa shillingi kuwa si lazima iwe hivyo kama wengi wanavyofikiria. Hizi fikira hazina utofauti wa msemo wa kabila fulani wanakawaida ya kuwauwa wanaume zao kwa sababu ya mali, au kabila fulani wanakula mbwa! Samaki mmoja akioza basi sio wote hawafahi. Kadri siku sinavyozidi kwenda tumeweza kuona wadada wanaojiheshimu na wenye elimu bora wasio na sifa ya umalaya nao pia wanaoolewa na wazungu.
Kuna sababu nyingi sana za wanasichana wengi kuamua kuolewa na mtu mweupe. Kuna wanaona kuwa pale kuna uhakika wa maisha mazuri au kuna matumaini ya kuondokewa na maisha magumu, wengine wanaona wanajua kujali na wanauvumilivu, wengine lengo la kupata watoto chotala, kama sie kwetu usukumani binti mweupe anathamani ya kuchumbiwa kwa ng'ombe 40. Hivyo basi kila mtu na sababu zake.
Tukirudi kwenye upande wa sababu nyingine kuu ambayo pia kuna uwezekano mkubwa wa wadada wa kitanzania kukimbilia kuolewa na wazungu. Mara nyingi umekuwa ukisikia wavulana (wanaume) wakiwapondea mabinti wakitanzania kwa kuwaita majina mabaya kama vicheche, au hata kuwakosoa kwa kudai kuwa wanatabia mbaya. Ambavyo si lazima iwe kweli, wao usema hivyo kutokana na kujiridhisha nafsi zao, bila kujua dharau hizo zinajenga ukuta mkubwa wa kutenganisha uwezekano wa kukosa mke bora wa kitanzania. Na endapo utokea kuwaowa, bado uwadharau wake zao na kutegemea wao ndio waheshimiwe, bila kujua heshima utokana na heshima.
Unapomweshimu mtu nae hana budi kukuheshimu pia. Binafsi nina mfano hai kabisaaa,-yupo kaka mmoja ambaye anajulikana (superstar wa bongo). Huyu kaka ni mtu anayejiheshimu lakini anakawaida ya kusema "wasichana wa kibongo wote vicheche". Na alishawi kudiliki kuvunja uwezekano wa kuolewa kwa binti mmoja wa kitanzania. Kwasababu aliyekuwa muoaji ni best yake. Na huwa ana kawaida ya kusema hivyo hata kwa marafiki zake wa kike pia na wasichana anayetoka nao ambao wanajiheshimu, lakini kwake ni vicheche. Na na hakika wako vijana wengi wa namna hii, sasa hali hii sijui kama tutafika kama kaka zetu msipojirekebisha. -Oweni au acheni kulalamika!
All I wanna say is that, tujifunze kukubali vya kwetu. Vya kwetu ni vitamu na vizuri kuliko, hakuna sababu ya kuviponda kisa...kufurahisha nafsi zetu.
----
Hayo ni maneno ya Total Knockout!!