Vijana wa HALAIKI huwa wananufaika na kipi baada ya mafunzo na shughuli ya kiserikali kupita?

Half american

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
26,356
68,939
Habari zenu wakuu.

Tarehe 02/04/2024 kulikuwa na tukio la kuwasha mwenge wa uhuru mkoani kilimanjaro na mgeni rasmi alikuwa ni waziri mkuu Mh. Kassim Majaliwa.

Kama ilivyo kawaida kwa shughuli yeyote ile lazima yawepo maandalizi mazuri ili kuweza kufanikisha kwa ufanisi mkubwa.

Moja ya maandalizi ni pamoja na mafunzo ya halaiki kwa vijana waliochaguliwa kutoka shule mbalimbali ndani ya mkoa/wilaya husika. Zoezi la mafunzo kwa waliochaguliwa lilidumu kwa zaidi ya miezi miwili.

Je hawa vijana wa halaiki wananufaika na nini kitakachowatofautisha na vijana ambao hawakuchaguliwa baada ya shughuli ya kiserikali kufanyika? Kuna vyeti vitakavyowapa utambulisho kuwa walishiriki mafunzo hayo?

Kama hakuna nashauri kuwe na utaratibu huo wa kuwazawadia hata vyeti maana mpaka sasa naona vijana wameambulia kupewa track suti, raba na miamvuli. Ukizingatia walilazimika kusoma nusu siku na wakati mwingine kutokuingia darasani kabisa ili kushiriki mafunzo hayo ya halaiki.

Mheshimiwa Dkt. Gwajima D wizara yako inahusika na watoto naomba kama unaweza kutoa muongozo/maelekezo yoyote kwenye hili utusaidie. Tunaomba ufikishe na haya mapendekezo yetu kwa faida ya watoto. Ahsante.

NAWASILISHA....
images (27).jpeg
images (26).jpeg
images (21).jpeg
 
Habari zenu wakuu..
Tarehe 02/04/2024 kulikuwa na tukio la kuwasha mwenge wa uhuru mkoani kilimanjaro na mgeni rasmi alikuwa ni waziri mkuu Mh. Kassim Majaliwa.

Kama ilivyo kawaida kwa shughuli yeyote ile lazima yawepo maandalizi mazuri ili kuweza kufanikisha kwa ufanisi mkubwa.

Moja ya maandalizi ni pamoja na mafunzo ya halaiki kwa vijana waliochaguliwa kutoka shule mbalimbali ndani ya mkoa/wilaya husika. Zoezi la mafunzo kwa waliochaguliwa lilidumu kwa zaidi ya miezi miwili.

Je hawa vijana wa halaiki wananufaika na nini kitakachowatofautisha na vijana ambao hawakuchaguliwa baada ya shughuli ya kiserikali kufanyika? Kuna vyeti vitakavyowapa utambulisho kuwa walishiriki mafunzo hayo?

Kama hakuna nashauri kuwe na utaratibu huo wa kuwazawadia hata vyeti maana mpaka sasa naona vijana wameambulia kupewa track suti, raba na miamvuli. Ukizingatia walilazimika kusoma nusu siku na wakati mwingine kutokuingia darasani kabisa ili kushiriki mafunzo hayo ya halaiki.

NAWASILISHA....
View attachment 2963115View attachment 2963116View attachment 2963117
Kitu kizuri sana hiki Kwa watoto, Kwa mazingira yetu watoto wakipata exposure Kama hii kushiriki michezo na activity kubwa Kama hizi huwaongezea confidence na hu unlock potentials zao. Si ajabu kwetu sisi kukuta mtu kamaliza chuo lakini bado ana uoga uoga ila kwa wenzetu mtoto wa 15 ni mkubwa sana maana ameshakuwa exposed sehem mbali mbali. Hata bila vyeti ile tu ku take responsibility inamkuza mtoto ile kuwa sehem ya mafanikio ya jambo flan Ina instill kitu flan Kwa mtoto na kujiamini pia. Watoto wanajifunza mambo mengi sana kwa njia hizi kuliko kukaa tu darasani
 
Hata bila vyeti ile tu ku take responsibility inamkuza mtoto ile kuwa sehem ya mafanikio ya jambo flan Ina instill kitu flan Kwa mtoto na kujiamini pia
Sikatai kuwa wanapata exposure ila vyeti ni muhimu kwao, miezi zaidi ya miwili wanafanya mazoezi alafu kuwapa pongezi ya mdomo tu mi naona haifai na ukizingatia ni tukio ambalo ndani ya mkoa mpaka lije kujirudia inaweza pita miaka mingi.
 
Sikatai kuwa wanapata exposure ila vyeti ni muhimu kwao, miezi zaidi ya miwili wanafanya mazoezi alafu kuwapa pongezi ya mdomo tu mi naona haifai na ukizingatia ni tukio ambalo ndani ya mkoa mpaka lije kujirudia inaweza pita miaka mingi.
Vyeti wavipeleke wapi ? Waende kuombea kazi au kutambulika ili iweje ka tukio kenyewe ni kadogo sana. Sasa mtu si atajikuta ana vyeti 200. Cheti kitolewe kwenye kitu ambacho ni outstanding siyo hiyo michezo ambayo kila mtu anaweza kufanya. Siku hizi hata vyeti vya computer hizi basic skills Kama word na excel havitumiki tena sembuse hiyo michezo

Ma tukio ya namna hii ni mengi mno nchini hata simba day na Yanga say yanafanyika tena kutumia watoto au vijana hao hao kutoka mashule mbali mbali . Vyeti hapo ni unnecessary
 
Sikatai kuwa wanapata exposure ila vyeti ni muhimu kwao, miezi zaidi ya miwili wanafanya mazoezi alafu kuwapa pongezi ya mdomo tu mi naona haifai na ukizingatia ni tukio ambalo ndani ya mkoa mpaka lije kujirudia inaweza pita miaka mingi.
Sasa wapeww vyeti watavifanyia kazi gani

Hapa naona kuna kosa hufanyika, huwezi wafanyisha watoto kazi ya malipo, lakini mkono wa pongezi kwa watoto ingekuwa Bora zaidi plus hayo matruck suit
 
Back
Top Bottom