CYBERTEQ
JF-Expert Member
- Feb 11, 2012
- 7,341
- 4,076
Inategemea, wengine kweli ni "swaga" tu. yaani ni trend ambayo inakuja mtu kuwa na begi na headphones ni kama fasheni, tusiwacheke hata ujana wa enzi zetu ilikuwa na vituko pia, hata huo mtindo wa vibegi mgongoni ulikuwepo sana miaka ya themanini, inajirudia tu. Mimi nimeshavuka rika la "vijana", lakini nikitoka mara nyingi lazima nibebe kibegi (siyo cha mgongoni), inaweza kuwa messenger bag ndogo ya kuenea laptop moja, smartphone na makabrasha ya muhimu, kama siendi ofisini na ninakoenda hakuhiaji laptop wala makabrasha mengi nabeba clutch bag ndogo ambayo naweka vitu vya msingi kama simu, kindle, tablet, funguo, na vitu vingine vidogovidogo kulingana na sehemu nayokwenda, kama nakwenda sehemu mara moja tu na kurudi basi sibebi kitu zaidi ya nokia yangu ya tochi.
Engineer akiwa anakwenda kazini lazima awe tooled up!
GraphicDesigner lazima abebe zana zake za kazi!
Mwalimu na yeye lazima abebe maandalio ya somo.
Wengine wajasiriamali alfajiri anaenda kukamata viatu kongo, mchana anatembelea wateja wake.
Mjini mihangaiko, ukifuatilia sana mtu kabeba nini utapoteza muda bure!
Engineer akiwa anakwenda kazini lazima awe tooled up!
GraphicDesigner lazima abebe zana zake za kazi!
Mwalimu na yeye lazima abebe maandalio ya somo.
Wengine wajasiriamali alfajiri anaenda kukamata viatu kongo, mchana anatembelea wateja wake.
Mjini mihangaiko, ukifuatilia sana mtu kabeba nini utapoteza muda bure!