Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

!
!
Habari wadau wa jukwaa hili!
Mnisamehe sana kama nitawakwaza na swali langu.
Hivi haya mabegi ya mgongoni ambayo watu wanakuja nayo hadi kwenye sehemu za starehe huwa wanabeba vitu gani?

Hasa ndugu zetu wa dar ambao huombea mvua inyeshe ili wavae masweta yenye Kofia.
Kama hutoki namtumbo wewe ni bahati...!
 
Mabrazamen wa Dar huenda kusaga unga nashineni kisha kuuweka kwenye begi!
 
Kwanini unataka kujua wanavyoweka humo?

Mimi huwa naweka beto, maji ya kunywa na nguo za dojo.
 
Mazoea jombaa; watu tumeanza kubebeshwa mabegi mgongoni tangia tukiwa chekechea...

Chekechea... mabegi
Primary... mabegi
Primary tuition... mabegi
O-Level... mabegi
O-Level tuition... mabegi
A-Level... mabegi
A-Level tuition... mabegi
Chuo... mabegi!

Remember, kwa mwanafunzi wa Dar hawezi kwenda/kurudi shule/chuo bila begi kutokana na kashikashi ya usafiri.

Probably ukiwa mkoa, unaweza kuchukua madaftari yako mawili matatu ya masomo husika, ukayabana kwapani kisha huyooo, skonga! Dar ukifanya hivyo, hayo madaftari utayaacha kwenye kituo cha daladala!

Sio siri, nikitembea bila begi huwa najiona mwepesi ile mbaya... not normal na siwi comfortable.
 
Mabegi ni personal zaidi unaweka chochote kunawengine mafundi wanaweka vifaa vyao na wengine sidhani kama inatakiwa kufuatilia kuna nn....!!
 
Sijui wanaweka nini humo ndani, maana ni kama fashion kwa sasa.
Juzi wakati nipo Taifa kuna kijana nilikaa nae jirani wakati anafungua nikachungulia, Ajabu katoa headphone ya simu na hamkuemo na kitu kingine cha ziada ndani nilichoka sana.

Binafsi naona kama ni ushamba fulani hivi ambao vijana wanalimbukia bila kujielewa.
He mkuu kumbe wanabeba hamna kitu? Mimi nilidhani kuna madaftari au laptop. Mimi siyo kijana lakini naweka laptop na nisipoenda na gari naweka begi mgongoni na ndani mna laptop. Basi vijana ni washamba. Begi ni kuhifadhi vitu siyo urembo.
 
Wengine ndio office jamani kasoro hao wakurupukaji
 
Begi muhim sana hata kama huna ulichobeba unaweza kupata mzigo mbele ukaubeba inaepusha kuwa na mizigo mingi
Unaenda kazini begi empty ukirudi umebeba vizaga zaga vya nyumbani kifupi bila begi hakuna mtoko
 
Sijui wanaweka nini humo ndani, maana ni kama fashion kwa sasa.
Juzi wakati nipo Taifa kuna kijana nilikaa nae jirani wakati anafungua nikachungulia, Ajabu katoa headphone ya simu na hamkuemo na kitu kingine cha ziada ndani nilichoka sana.

Binafsi naona kama ni ushamba fulani hivi ambao vijana wanalimbukia bila kujielewa.
siku hizi vijana WA DAR
utakuta powerbenk
pafyumu
laptop
ipad
n.k
asipate tabu kwenye miangaiko yake
 
''Vijana wa Dar"

Ok, ni kwa kiasi gani kubeba kwao mabegi wewe kunakuadhiri? Ok, we suruali unayovaa hope ina mifuko 4, yote kuwa unaweka nini ... si ungebali na mfuko mmoja tu!

Waacheni vijana wa Dar waishi maisha yao

😡😡😡😡😡😡😡😡
 
Tunakuwa tumebeba bangi tunaenda kuuza.Acha kufuatilia vijana wenzako wamebeba nini,fanya mambo yako.Shenzi
 
Back
Top Bottom