Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,502
- 4,408
Wasalaam,
Viongozi wetu wakuu wanapoteua vijana ambao pengine hawana uzoefu wala ujuzi mkubwa sio kwamba tunastahili sana ila ni kwa sababu tunatengenezwa mazingira ya kuaminiwa kwa nafasi za juu na pengine siku moja vijana ndio washike hatamu ya uongozi wa Taifa hili. Kinachoendelea sasa, badala ya vijana kujenga imani kwa kuongeza maarifa, ujuzi na uwezo tumegeuka kuwa wajenga hofu kwa kufanya siasa za kibabe na zisizo na tija. Ningependa ubabe huo tungeutumia kutafuta fursa za uwekezaji na ujasiriamali kwa ajili ya ukuaji wa uchumi wetu.
Siku chache zijazo Rais wetu atafanya mabadiliko kwenye nafasi za ukuu wa wilaya na ukurugenzi wa halmashauri na pengine katika nafasi hizi tutaona sura mpya nyingi za vijana. tutapewa nafasi nyingine muhimu ya kuaminiwa kwa nafasi za uongozi, tutumie nafasi hizi kujijenga na kuonesha imani kwa wananchi. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetengeneza mazingira mazuri kwa vijana wengine kuaminiwa.
Tabia aliyoionesha Sabaya na vijana wengine, inasikitisha na hazifai kuwa tabia ya kiongozi awe kijana ama mzee, hivyo tabia hizi tuepukane nazo na kuachana nazo kwa sababu ni doa kubwa. Tuchukue hii kama ni changamoto hivyo tusahihishe, kwa kufanya hivi hakika vijana ni mabadilio. Tumsaidie Rais wetu anatuhitaji sisi vijana.
Viongozi wetu wakuu wanapoteua vijana ambao pengine hawana uzoefu wala ujuzi mkubwa sio kwamba tunastahili sana ila ni kwa sababu tunatengenezwa mazingira ya kuaminiwa kwa nafasi za juu na pengine siku moja vijana ndio washike hatamu ya uongozi wa Taifa hili. Kinachoendelea sasa, badala ya vijana kujenga imani kwa kuongeza maarifa, ujuzi na uwezo tumegeuka kuwa wajenga hofu kwa kufanya siasa za kibabe na zisizo na tija. Ningependa ubabe huo tungeutumia kutafuta fursa za uwekezaji na ujasiriamali kwa ajili ya ukuaji wa uchumi wetu.
Siku chache zijazo Rais wetu atafanya mabadiliko kwenye nafasi za ukuu wa wilaya na ukurugenzi wa halmashauri na pengine katika nafasi hizi tutaona sura mpya nyingi za vijana. tutapewa nafasi nyingine muhimu ya kuaminiwa kwa nafasi za uongozi, tutumie nafasi hizi kujijenga na kuonesha imani kwa wananchi. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetengeneza mazingira mazuri kwa vijana wengine kuaminiwa.
Tabia aliyoionesha Sabaya na vijana wengine, inasikitisha na hazifai kuwa tabia ya kiongozi awe kijana ama mzee, hivyo tabia hizi tuepukane nazo na kuachana nazo kwa sababu ni doa kubwa. Tuchukue hii kama ni changamoto hivyo tusahihishe, kwa kufanya hivi hakika vijana ni mabadilio. Tumsaidie Rais wetu anatuhitaji sisi vijana.