Wote hao ni misukule yenye kazi maalum.Ijuma Kareem ndugu zetu Waislamu na Heri ya siku hii pia kwa Wana-jamiiforums wote. Katika mihangaiko yangu ya kusaka 'ngawila' nimebahatika kufanya kazi na watu mashuhuri na wakubwa mbali mbali hapa nchini.
Miongoni mwa hao wakubwa basi Mwamposa na BM ni miongoni mwao. Ila naomba nijikite kwa huyu Mwamposa kwa muktadha wa huduma yake.
Kwa Jumapili siyo chini ya tatu nilizokwenda kanisani kwake pale Kawe, nimebahatika kukutana na MAMIA ya mabinti ambao wanakwenda kuomba wapate waume wa kuwaoa.
Mabinti wengi niliowakuta ni warembo, warefu wa vimo, wana maumbo ya kutamanisha, weupe na wana nyuso za furaha na ukarimu sana.
Sasa nikakumbuka humu kuna vijana wengi hawajaoa, sasa nikaona niwaambie vijana, jisogezeni pale Kawe mkajichagulie wanawake wa kuoa, hivi hamuwaoni wale pisi kali kwenye Arise And Shine TV kila Jumapili?
Yaani wanaume ni wachache sana mpaka watoto wazuri kama wale wanakosa wa kuwaoa. Aisee hali ni ngumu mno.
Achilia mbali hilo, hata mitaani huku wapo mabinti wengi tunaishi nao wanatafuta waume wa kuwaoa vijana mpo wapi? Mfano kuna binti ana gari, nyumba, elimu n.k, yeye anatafuta mume tu, mpaka kwa waganga ameshakwenda sana ili mambo yake yakae sawa.
Huyu binti hivi wakware hawamuoni? Vijana mnashindwa wapi nyie? Kawe kwa mwezi yaani Jumapili nne, zaidi ya pisi kali mia nne zinaripoti kutafuta waume. Zimekosa waume wa kuwaoa.
Zipambanieni zile pisi kali za Kawe vijana oeni wekeni ndani mpate familia. Mnaziangaliaje na kuziacha tu hivi hivi huku mkila kwa macho?
Telecommunication Engineer.Nilikumis sana mhandisi upo?Wote hao ni misukule yenye kazi maalum.
Wajinga ndiyo waliwao.
Sasa shida ipo wapi?Hakuna binti mzuri wa sura umbo na tabia anaekosa mume
Hili la ushuhuda wa uongo linakuwa kwa kasi sana siku hizi.Utakuja kubeba mke mwenye itikadi za hovyo na utayajutia Maisha yako, utakuja kubeba mke mgonjwa aliyeshindikana amekuja kutoa ushuhuda wa uongo kuwa amepona
HakikaUsiwaone hapo kwa mwamposa kuna siri nzito mno zimejificha.....
Hujakosea upo vizuri kuna mmoja ana tabia hiyoyaani watafuta kuolewa lakini wanapiga wanaume wengi chini lakini wana vigezo vikali sana mfano pesa nyingi n.k....
JichanganyeOoooh kumbe
Wanachagua wanataka wenye pesaDuuuh basi kama wapo hivyo na hawana wa kuwaoa basi wajitafakari au basi wanachagua wenye pesa.
Usisahau doctor au engineerWanataka wa BOT,TRA,TRL,UBALOZI, TPA
Mchana wavaaa sketi ndefu , usiku. Nusu mini sketi ,
..chunguza
Haya yanajiropokea tu ukiyafatilia unakuta n mahuni ya mtaaan yalifeli form 4Labda Kwa wale ambao hawajasoma hadi chuo kikuu.
kwa nini mkuuKuoa mwanamke anae sali kwa mwampo#a ni kuweka maisha yako rehani.. sijui vijana mmenisikia
Ndiyo nafananishwa na wewe? Jinga kabisa