Loading failed
JF-Expert Member
- Sep 14, 2023
- 1,945
- 5,849
Wana Jf natumaini mko poa kabisa.
Ndugu zangu kuna wimbi la vijana na mabinti chipukizi wanao dhurura hovyo nyakati za jioni kwanzia mida ya saa kumi na mbili jioni (18:00) mpaka saa tatu usiku ( 21:00) wakiwa wanaelekea huku na huko, vijana wengine wakiwa magenge kwa magenge kwenye mabaraza zinapotolewa huduma za mahitaji muhimu na kwenye madisco uchwara mtaa kwa mtaa, kijiji kwa kijiji, mji kwa mji ndani ya nchi
hawa vijana na mabinti wamekua wakiogopa sana moja ya haya maradhi ikiwemo Gono , UT.I sugu. Wengine wamekua wakiogopa sana kubebesha /kubeba mimba au vyote kwa pamoja bila kujali kuna gonjwa hatari la UKIMWI linaloweza kujificha ndani ya mtu na ambalo halipimwi kwa macho wala kwa maneno ya kuapizana, hawa vijana wamekua kama waliochanganyikiwa na kukata tamaa na maisha yao, wameweka utani kwenye afya zao huku wakiwaka tamaa za ngono uzembe.
Ndugu zangu kwa masikitiko utasikia wakiambiana wao kwa wao huku wakiapizana hata kwa majina matakatifu kulingana na imani zao mbaya zaidi wamefikia kuaminishana kwamba hawana UKIMWI na kuhimizana wewe ni amini tufanye hivyo hivyo bila kinga maana zina washa, wengine wanafika mbali na kupigana mikwara huku kwa kuambiana moja ya hizi kauli:-
1: Kama una mashaka na mimi ni ache tafuta mwingine utakaye muamini, ingekua mimi mgonjwa hata rafiki yako angesha kufa mapema tuu
2: Kama uniamini basi wewe nenda zako utakulaje pipi na maganda yake peleka utoto huko
3: Wewe vipi kati ya mimba na ukimwi unaogopa kipi acha ushamba
4: Acha ushamba UKIMWI au ui dawa zipo, situmii condom zinawasha sitosikia raha
5: Mwingine anafikia hatua ya kujiapiza kabisa huku akitoa ushuhuda bandia kwa kusema nimepima miezi sita iliyopita niamini sijashiriki popote pale (anamalizia kwa kutaja majina matakatifu)
6: Achana na mimi peleka utoto huko UKIMWI haupo Gono na U.T.I ndiyo habari ya mjini
7:Kama uniamini tume tongozana ya nini mimi sipimi UKIMWI pita hivi hutaki tuachane
Balaa hili kwa sasa ni baya sana kijana au binti anaogopa kuachika au kuachwa na mwenzake pindi atakapo gusia maswala ya kupima afya zao, mambo yamekua magumu bila mashaka wala kuchukua tahadhari wanaingiliana hovyo hovyo tuu ndugu zangu. Wa meweka maisha yao rehani ili kutoa kitu na kupata kitu , vijana kwa mabinti wamekua busy kuhangaika na ghonoreah (Gono) pamoja na U.T.I sugu na kusahau kuna janga la UKIMWI , ndugu zangu, hawana tahadhari wamekata tamaa wameamua kupoteza mwelekeo wa maisha yao na kuweka Roho zao rehani.
Najiuliza sana elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi ipo wapi kwa sasa na kama ipo je inatolewa mashuleni na kwenye nyumba za ibada pamoja na vituo vya afya kwa usahihi au ni wanatoa tuu matangazo ya kutumia dawa na siyo kujilinda dhidi ya janga hili baya huku wakisingizia ugumubwa maisha na ujio wa utandawazi
Je, hawa vijana na mabinti wadogo ni kwamba hawana elimu yeyote au ni ulimbukeni na haraka zao za hovyo zinazopelekea kuhatarisha maisha yao, nani wa kulaumiwa kati ya wazazi, walimu, serikali ,mashirika au hata wataalamu wa afya, je wana habari nao tuwalaumu au tufanyaje ndugu zangu, vijana wamepote wana pimana kwa macho na kuapizana kwamba wapo salama kuendelea na game.
Nb: NGUVU KAZI YA TAIFA INAPOTEA KWA KASI SANA, VIJANA NA MABINTI WAMEWEKA MAISHA YAO REHANI WANAOGOPA GONO NA U.T.I KULIKO HATA HIV/AIDS.
UKIMWI UPO ,UKIMWI UNAUA JALI AFYA YAKO , MLINDE NAE ATAJILINDA ASIPO JILINDA ACHANA NAE UHAI NI MARA MOJA
Ndugu zangu kuna wimbi la vijana na mabinti chipukizi wanao dhurura hovyo nyakati za jioni kwanzia mida ya saa kumi na mbili jioni (18:00) mpaka saa tatu usiku ( 21:00) wakiwa wanaelekea huku na huko, vijana wengine wakiwa magenge kwa magenge kwenye mabaraza zinapotolewa huduma za mahitaji muhimu na kwenye madisco uchwara mtaa kwa mtaa, kijiji kwa kijiji, mji kwa mji ndani ya nchi
hawa vijana na mabinti wamekua wakiogopa sana moja ya haya maradhi ikiwemo Gono , UT.I sugu. Wengine wamekua wakiogopa sana kubebesha /kubeba mimba au vyote kwa pamoja bila kujali kuna gonjwa hatari la UKIMWI linaloweza kujificha ndani ya mtu na ambalo halipimwi kwa macho wala kwa maneno ya kuapizana, hawa vijana wamekua kama waliochanganyikiwa na kukata tamaa na maisha yao, wameweka utani kwenye afya zao huku wakiwaka tamaa za ngono uzembe.
Ndugu zangu kwa masikitiko utasikia wakiambiana wao kwa wao huku wakiapizana hata kwa majina matakatifu kulingana na imani zao mbaya zaidi wamefikia kuaminishana kwamba hawana UKIMWI na kuhimizana wewe ni amini tufanye hivyo hivyo bila kinga maana zina washa, wengine wanafika mbali na kupigana mikwara huku kwa kuambiana moja ya hizi kauli:-
1: Kama una mashaka na mimi ni ache tafuta mwingine utakaye muamini, ingekua mimi mgonjwa hata rafiki yako angesha kufa mapema tuu
2: Kama uniamini basi wewe nenda zako utakulaje pipi na maganda yake peleka utoto huko
3: Wewe vipi kati ya mimba na ukimwi unaogopa kipi acha ushamba
4: Acha ushamba UKIMWI au ui dawa zipo, situmii condom zinawasha sitosikia raha
5: Mwingine anafikia hatua ya kujiapiza kabisa huku akitoa ushuhuda bandia kwa kusema nimepima miezi sita iliyopita niamini sijashiriki popote pale (anamalizia kwa kutaja majina matakatifu)
6: Achana na mimi peleka utoto huko UKIMWI haupo Gono na U.T.I ndiyo habari ya mjini
7:Kama uniamini tume tongozana ya nini mimi sipimi UKIMWI pita hivi hutaki tuachane
Balaa hili kwa sasa ni baya sana kijana au binti anaogopa kuachika au kuachwa na mwenzake pindi atakapo gusia maswala ya kupima afya zao, mambo yamekua magumu bila mashaka wala kuchukua tahadhari wanaingiliana hovyo hovyo tuu ndugu zangu. Wa meweka maisha yao rehani ili kutoa kitu na kupata kitu , vijana kwa mabinti wamekua busy kuhangaika na ghonoreah (Gono) pamoja na U.T.I sugu na kusahau kuna janga la UKIMWI , ndugu zangu, hawana tahadhari wamekata tamaa wameamua kupoteza mwelekeo wa maisha yao na kuweka Roho zao rehani.
Najiuliza sana elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi ipo wapi kwa sasa na kama ipo je inatolewa mashuleni na kwenye nyumba za ibada pamoja na vituo vya afya kwa usahihi au ni wanatoa tuu matangazo ya kutumia dawa na siyo kujilinda dhidi ya janga hili baya huku wakisingizia ugumubwa maisha na ujio wa utandawazi
Je, hawa vijana na mabinti wadogo ni kwamba hawana elimu yeyote au ni ulimbukeni na haraka zao za hovyo zinazopelekea kuhatarisha maisha yao, nani wa kulaumiwa kati ya wazazi, walimu, serikali ,mashirika au hata wataalamu wa afya, je wana habari nao tuwalaumu au tufanyaje ndugu zangu, vijana wamepote wana pimana kwa macho na kuapizana kwamba wapo salama kuendelea na game.
Nb: NGUVU KAZI YA TAIFA INAPOTEA KWA KASI SANA, VIJANA NA MABINTI WAMEWEKA MAISHA YAO REHANI WANAOGOPA GONO NA U.T.I KULIKO HATA HIV/AIDS.
UKIMWI UPO ,UKIMWI UNAUA JALI AFYA YAKO , MLINDE NAE ATAJILINDA ASIPO JILINDA ACHANA NAE UHAI NI MARA MOJA