Bush Dokta
JF-Expert Member
- Apr 11, 2023
- 12,133
- 20,295
Kwanza nikiri watoto wa vigogo wengi wamesoma sana na wana bidii sana kwenye masomo.
Zamani niliaminishwa vijijini kwamba watoto wa matajiri hawapendi shule na kwamba huwa wanafeli.
Baada ya kusogea mbele ki elimu nikahama mkoa niliokuwa naishi huko vijijini nilikutana na ulimwengu wa tofautu kabisa.
Watoto wa vigogo yaani RC, DC, DAS, Ma generali wa jeshi, Wakurugenzi wa Tasis za serikali kama BOT, NSSF, PSSF, TPDC, TANESCo, bila kusahau watoto wa wenyeviti na makatibu wa ccm ngazi mbali mbali Taifa, mkoa na wilaya niligundua wako serious sana na masomo na ni vichwa sana.
Wanajituma kusoma na wana sapoti nzuri kutoka kwa wazazi wao ikiwemo pesa na matumizi mengine ya kujikimu.
Ilikuwa ni jambo la kawaida mtoto wa kigogo kukuta ana akiba ya pesa kuanzia Laki moja kwenda mbele huku tukiwa Boarding school na kila kitu nakula hapo hapo.
Hali ile nilijua inawapa sana motisha watoto wao kusoma na kutokata tamaa. Na wengi waliongoza kwa ufaulu darasani. Ikitokea mtoto wa kabwela amefaulu kuwazidi basi inakuwa kwa uchache sana.
Richa ya hayo yoote bado linapokuja swala la ajira watoto wa vigogo wenye utajiri na mitaji hatuoni wakijiajiri badala yake Wazazi wao wanapigana vikumbo kuhakikisha watoto wao wanapata nafasi za ajira serikalini.
Majaji, wabunge na mawaziri ndio hivyo hivyo.
Huku wakiwambia watoto wa kabwela kuwa kuajiriwa ni umaskini na kujiajiri ndio mpango mzima.
Je tunapigwa?
Zamani niliaminishwa vijijini kwamba watoto wa matajiri hawapendi shule na kwamba huwa wanafeli.
Baada ya kusogea mbele ki elimu nikahama mkoa niliokuwa naishi huko vijijini nilikutana na ulimwengu wa tofautu kabisa.
Watoto wa vigogo yaani RC, DC, DAS, Ma generali wa jeshi, Wakurugenzi wa Tasis za serikali kama BOT, NSSF, PSSF, TPDC, TANESCo, bila kusahau watoto wa wenyeviti na makatibu wa ccm ngazi mbali mbali Taifa, mkoa na wilaya niligundua wako serious sana na masomo na ni vichwa sana.
Wanajituma kusoma na wana sapoti nzuri kutoka kwa wazazi wao ikiwemo pesa na matumizi mengine ya kujikimu.
Ilikuwa ni jambo la kawaida mtoto wa kigogo kukuta ana akiba ya pesa kuanzia Laki moja kwenda mbele huku tukiwa Boarding school na kila kitu nakula hapo hapo.
Hali ile nilijua inawapa sana motisha watoto wao kusoma na kutokata tamaa. Na wengi waliongoza kwa ufaulu darasani. Ikitokea mtoto wa kabwela amefaulu kuwazidi basi inakuwa kwa uchache sana.
Richa ya hayo yoote bado linapokuja swala la ajira watoto wa vigogo wenye utajiri na mitaji hatuoni wakijiajiri badala yake Wazazi wao wanapigana vikumbo kuhakikisha watoto wao wanapata nafasi za ajira serikalini.
Majaji, wabunge na mawaziri ndio hivyo hivyo.
Huku wakiwambia watoto wa kabwela kuwa kuajiriwa ni umaskini na kujiajiri ndio mpango mzima.
Je tunapigwa?