Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
Mbunge wa Viti Maalum (Anayewakilisha Wafanyakazi Nchini) Anayetokea Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Janejelly James Ntate amewaasa wazazi na walezi kuwa makini na malezi ya watoto hasa watoto wa kike kwa kuwa watoto hao wapo hatarini sana kutokana na kukumbana na vishawishi vya kila aina tofauti.
Mhe. Janejelly James Ntate ameyasema hayo katika mahafali ya kidato cha nne yaliyofanyika Shule ya Sekondari ya Buyuni Zavala ambapo alialikwa kama mgeni rasmi.
Akizungumza na Wazazi na Walimu wa Buyuni, Mhe. Janejelly James Ntate ametaka pia wazazi wasipuuze malezi ya watoto wa kiume kwani hata nao wamekuwa wakiharibiwa sana na masuala ya unajisi na mtindo wa kisasa na kuwataka washirikiane na walimu kuhakikisha watoto wa jinsia zote wanafikia malengo yao.
Aidha, Mhe. Janejelly James Ntate aliahidi kuchangia idadi ya Viti 20, Meza 5 za Plastiki na Vyeti kwa ajili ya wanafunzi waliofanya vizuri kwenye usafi na taaluma.
Mhe. Janejelly James Ntate ameyasema hayo katika mahafali ya kidato cha nne yaliyofanyika Shule ya Sekondari ya Buyuni Zavala ambapo alialikwa kama mgeni rasmi.
Akizungumza na Wazazi na Walimu wa Buyuni, Mhe. Janejelly James Ntate ametaka pia wazazi wasipuuze malezi ya watoto wa kiume kwani hata nao wamekuwa wakiharibiwa sana na masuala ya unajisi na mtindo wa kisasa na kuwataka washirikiane na walimu kuhakikisha watoto wa jinsia zote wanafikia malengo yao.
Aidha, Mhe. Janejelly James Ntate aliahidi kuchangia idadi ya Viti 20, Meza 5 za Plastiki na Vyeti kwa ajili ya wanafunzi waliofanya vizuri kwenye usafi na taaluma.