HERY HERNHO
Member
- Mar 4, 2022
- 70
- 313
Siku ya jana Jumanne video ya kutisha ilianza kusambazwa kwenye mitandao ikionesha mwanaume aliyevaa magwanda ya kijeshi huku akiwa amevaa utepe mweupe (ambao kwa kawaida hutumiwa kama utambulisho wa mwanajeshi wa Urusi nchini Ukraine) akimkata kichwa mwanaume aliye hai aliyekuwa amevaa sare ya jeshi la Ukraine.
Nyuso za watu katika video hiyo ya dakika moja na nusu zilifunikwa na barakoa. Mmoja anayeaminiwa kuwa ni mwanajeshi Mrusi anaonekana akizungumza kupitia radio ya mawasiliano na kutoa maagizo kwa mwanajeshi wa pili (ambaye anatekeleza mauaji kwa kutumia kisu).
Picha hiyo pia inaonesha jinsi watu wawili wanavyoelezea mbele ya kamera jinsi wanavyomvua mwanajeshi wa Ukraine fulana ya kujikinga na risasi, Utepe wa rangi ya manjano unaonekana kwenye sare ya jeshi ya mtu ambaye anauawa (utepe wa rangi ya manjano hutumiwa na wanajeshi wa Ukraine vitani).
Video hiyo inaonesha majani ya kijani kibichi, kwahiyo huenda ilirekodiwa nyakati zilizopita, kwani kwa sasa hali ya hewa ni ya baridi kali.
Nyuso za watu katika video hiyo ya dakika moja na nusu zilifunikwa na barakoa. Mmoja anayeaminiwa kuwa ni mwanajeshi Mrusi anaonekana akizungumza kupitia radio ya mawasiliano na kutoa maagizo kwa mwanajeshi wa pili (ambaye anatekeleza mauaji kwa kutumia kisu).
Picha hiyo pia inaonesha jinsi watu wawili wanavyoelezea mbele ya kamera jinsi wanavyomvua mwanajeshi wa Ukraine fulana ya kujikinga na risasi, Utepe wa rangi ya manjano unaonekana kwenye sare ya jeshi ya mtu ambaye anauawa (utepe wa rangi ya manjano hutumiwa na wanajeshi wa Ukraine vitani).
Video hiyo inaonesha majani ya kijani kibichi, kwahiyo huenda ilirekodiwa nyakati zilizopita, kwani kwa sasa hali ya hewa ni ya baridi kali.