Vicky Ntetema ajificha baada ya ripoti BBC

Hili suala linahitaji userious from so called decision makers, kama wachuna ngozi wa Mbeya walimalizwa kwanini hao wa maalbino washindikane?sema kwa sababu haiko katika mikakati ya ushindi wa 2010 ndio maana yanafumbiwa macho.Hii inafanya ile style Mzee mstaafu Mahita ionekane ndio bora zaidi (Shoot ask questions later)
 
INVESTIGATIVE JOURNALISM inafundishwa kwenye VYUO vyetu VIKUU vinavyotoa SHAHADA ya UANDISHI? Polisi na wengine wanaohangaikia USALAMA wetu, VICKY amewaonyesha pa kuanzia, endeleeni sasa.
 
Uchawi,uchawi,uchawi,uchawi,kila kona .



Hirizi yasitisha kwa muda mwenendo wa kesi Dar
Na Elizabeth Suleyman

HIRIZI iliyorushwa mezani kwa waendesha mashitaka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kinondoni, jana ilizua mshangao na gumzo huku Hakimu akiwapiga mkwara waliofanya hivyo kwamba hatishwi hata kama wakitupa 10.


Hirizi hiyo iligundika juu ya meza wakati kesi ya kutekwa nyara kwa mtoto wa Kisomali (2) ilipokuwa ikisikilizwa mahakamani hapo jana.


Pamoja na waendesha mashikata mahakamani, meza hiyo pia hutumiwa na mawakili na tukio hilo lilitokea chumba namba tano cha mahakama.


Kitendo cha kukutwa hizi hiyo katika meza ya wakili na waaendesha mashitaka kilionyesha kuwashangaza watu waliokuwa wakisikiliza kesi na wengine kujiuliza mahali ilipotoka hirizi hiyo ambayo ilikuwa imesokotwa kwa kitambaa cheupe na kuzungushiwa kamba nyeupe.


Mara baada ya kuona hirizi hiyo, Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Eliminius Mchauru, alisema kwamba anashangaa katika dunia ya sasa kama kuna watu ambao wanaamini hirizi.


"Wale wote wanaoamini mambo ya hirizi mpaka sasa hivi, haya ni mambo ya kizamani, kama hali hii itaendelea wanao uwezo wa kurusha hata hirizi kumi kwa jinsi wanavyotaka. Hirizi haziwezi kututisha sisi tutaendelea na kazi," alisema.


Naye mwendesha mashitaka katika kesi hiyo, Isaya Mwanga, alisema kwamba kitendo cha watu kurusha hirizi bila kujulikana ilikotokea inasikitisha.


"Wakati nikimuhoji mshitakiwa nikaona hirizi ikiwa mezani, sijui ilitokea wapi, mimi nilishangaa kuona hirizi ikidondoka mezani bila kujua aliyetupa ni nani," alisema.


Hata hivyo, kesi hiyo iliendelea kusikilizwa huku hirizi ikiwa mezani hadi mahakama ilipofungwa jana.


Kesi ya kutekwa nyara kwa mtoto wa Kisomali inayoendeshwa na Hakimu Mchauru, iliendelea kusikilizwa jana katika mahakama hiyo, ambapo shahidi wa sita alitoa ushahidi wake.


Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa wa tano katika utekeji nyara wa mtoto huyo, ina mashahidi 15.


Tuma maoni kwa Mhariri

source.mwananchi.
 
nimesema nyie ngojeni tu.. hili Taifa linakoelekea..

Mwanakijiji taifa lielekee wapi zaidi ya hapa. Kila kitu kiko ovyo, kuna kitu kama anarch, sasa hivi unasikia vitu vya ajabu tu, et rais alivalia njuga suala la miba shule za msingi, wakati kuna issue nzito zinazohitaji kushughulikiwa. Wapi zaidi ya hapa, au tukifika kama Zimbabwe kwenye inflation ya asimili milioni 2?
 
nimesema nyie ngojeni tu.. hili Taifa linakoelekea..
MMKJ taifa linakoelekea ni giza tupu mpaka inakuwa vigumu kutabiri nini hatima yetu kama Taifa.
Hili linatokana na kufumbia macho yale masuala makubwa na yenye athari kwa Taifa na viongozi wetu kuleta blabla bila hata ya aibu.
Ni taifa la wapumbavu tu ndilo ambalo linaweza kudharau mauaji ya jamii fulani ya wananchi wake wenye ulemavu wa kiafya kwa sababu za kishirikina.
Tumeona jinsi Dunia ilivyopiga kelele suala la mauaji ya Darfur yanayofanyika kwa jamii fulani. Jee sisi viongozi hawachukui hatua madhubuti kwa mauaji haya mpaka mataifa ya nje yaingilie kati kukomesha? wao wapo kwa ajili ya nini ilihali mambo ya aibu kama haya yanageuka kuwa ya kawaida?
Vicky hongera kwa kazi nzuri, Bora kufa kwa kufanya jambo la heshima kuliko kuishi na kufanya ya fedheha.
Taifa letu linapoteza mwelekeo.
 
...trick kama ya vick ntetema ..USALAMA WA TAIFA NA CID...HAWAKUWAHI KUIFIKIRIA......maana wangewashika waganga kama kuku..na ushahidi wa kumwaga....sasa kuna haja gani ya USALAMA WA TAIFA [aka . usalama wa kuku ,usalama wa vyura wa kihansi,usalama wa mafisadi] KUTENGEWA BAJETI YA BILIONI 140 KWA MWAKA!!!!!!???? ITS TIME NOW THERE BUDGET COME UP FOR SCRUTINY...THE NO GO ZONE SHELTER THEY PUT IT NDIO INAONGEZA UFISADI......

wanashindwaje na mwandishi wa habari ambaye simply hana hata elementary training ya UJASUSI...???

Sifikiri kama "usalama wa taifa" wanalipa hili priority.
 
Vitendo vya ushirikina vimezidi nchini kwasababu viongozi wengi wanashiriki.Sitashangaa kama na vipande vya albino vinaenda kwao!!
 
Chakaza,

Yaelekea taifa na wananchi wake wamepoteza muelekeo kama sio kuchanganyikiwa. Haya mauaji ya albinos kwa imani za kishirikina si jambo dogo na sioni hata kidogo serikali ikifanya juhudi zozote za kukomesha hii hali. Nadhani angalau kiongozi mmojawapo wa ngazi ya juu kama president, vice au PM angekuwa na mtoto albino then akakumbwa na hili balaa la kuuwawa kishirikina huenda wangechukua hatua.

Hali inatisha hawa wa-tz wenzetu wenye haki ya kuishi wataichukia nchi na viongozi wake kwa sababu za kufumbia macho mambo maovu dhidi yao. Ni kweli Vicky Ntetema ametoa mwanga kuwa haya mambo yapo si porojo au udaku......Serikali ifanye kazi jamani.
 
Bravo Vicky.You did a brave deed and we hail you for that.Dont ever regret what you did for you mother country.I believe BBC wana fedha za kutosha to provide 24 Hour Security Surveillance for you and your family.

Yaelekea taifa na wananchi wake wamepoteza muelekeo kama sio kuchanganyikiwa. Haya mauaji ya albinos kwa imani za kishirikina si jambo dogo na sioni hata kidogo serikali ikifanya juhudi zozote za kukomesha hii hali. Nadhani angalau kiongozi mmojawapo wa ngazi ya juu kama president, vice au PM angekuwa na mtoto albino then akakumbwa na hili balaa la kuuwawa kishirikina huenda wangechukua hatua.

Wewe siyo MTz Mkuu?
Dont wish evil on you fellow being coz it might befall you as well.
 
unajua hii vita ngumu kwasababu wateja wa hao "sangoma" ndio hao hao walinda na watunga sheria wetu! tunaposema usalama wetu uko mikononi mwa polisi, nao vigogo wa polisi wanasema usalama wao uko mikononi mwa "sangomas"!

So sangoma akitoa amri lazima kigogo wa nchi/ polisi atekeleze! Ushahidi upo, kuwa "kigogo" wa nchi hii anaabudu sana mambo hayo!
 
Katika mchakato wa kulisafisha taifa...kila uovu utawekwa hadharani kabla usafishaji wa kina haujatengamaa.... ! Kila kile kilichokuwa kichafu na kiovu kilichojificha ndani ya taifa tanzania kitakuwa hadharani kabla ..Kitafuna taifa hakijabwagwa chini na ukombozi kupatikana....stay tuned..!
 
Nyie ni watu wa ajabu kweli. Unajua kama kuna wanaokuza ushirikina ni hawa hawa viongozi wetu maana wengi wao bila kificho wako kwenye nafasi walizonazo baada ya kupitia kwa hao wakina sangoma.
Mnajua nini? kuna waganga wengi wametushagaza sana maana baada ya uchaguzi tu wanaendesha magari ya kifahari hata unaweza kushangaa mwenyewe. Lakini unajua wameyapata wapi?
Asikiaye na afahamu.
 
Yaani wakati hatukajapoa kitu.....Hii aibu kubwa wajameni viongizi wetu ndio wateja wakubwa wa vigagula hivi.....

albino mwingine auwawa biharamulo
HABARI ZIMEINGIA SASA HIVI ZINASEMA ALBINO MMOJA AMEUWAWA KIKATILI KATIKATI YA JUMA HILI NA VIUNGO VYA MWILI WAKE KUCHUKULIWA HUKO BIHARAMULO, MKOA WA KAGERA.
MAREHEMU AMBAYE AMETAMBULIKA KWA JINA LA JOVIN MAJALIWA MWENYE UMRI WA MIAKA 46 NA MKAZI WA KIJIJI CHA NYAKATARA ALIKUWA AMEJIPUMZISHA NYUMBANI KWAKE BAADA YA KAZI KWENYE SHAMBA LAKE KABLA YA KUKUMBWA NA HILO BALAA.

INASEMEKANA MNAMO MAJIRA YA SAA NANE HIVI KUNDI LA WATU WALIOBEBA MAPANGA WALIMVAMIA NA KUMKATA MGUU WAKE WA KULIA NA SEHEMU ZAKE ZA SIRI NA KUTOKOMEA

MKE WA MAREHEMU, ALIYETAMBULIKA KAMA SARAH JOVIN, NA AMBAYE PIA NI ALBINO, ALIPOSIKIA PURUKUSHANI WAKATI AKIANDAA MAAKULI YA JIKONI ALIPIGA KELELE, AMBAPO WAUAJI HAO WAKAMVAMIA NA YEYE PIA NA KUMJERUHI VIBAYA. JIRANI WALIPOKUJA KUTOA MSAADA MAJAMAA YAKAKIMBIA NA HIZO SEHEMU ZA MWILI WA MAREHEMU, WAKIMWACHA SARAH HOI.


KAMANDA WA POLISI MKOA WA KAGERA, HENRY SALEWI, AKITHIBISHA TUKIO HILO LA KINYAMA ALISEMA KWAMBA SARAH AMELAZWA HOSPITALI YA WILAYA YA BIHARAMULO NA KWAMBA HALI YAKE INAENDELEA VYEMA.

KAMANDA SALEWI AMESEMA JUHUDI ZA KUWASAKA WAUAJI HAO ZINAENDELEA INGAWA HADI SASA HAKUNA MTU ALIYETIWA MBARONI KUHUSIANA NA TUKIO HILO LA KINYAMA.


MAREHEMU NA MKEWE WAMEJAALIWA KUPATA WATOTO WATATU WENYE UMRI KATI YA MIAKA 4 NA 15 NA MAJIRANI SASA WANA WASIWASI NA HAO WATOTO, KWANI WAWILI KATI YAO NI ALBINO PIA.

HII NI MARA YA TATU KWA WILAYA YA BIHARAMULO KUKUMBWA NA MKASA WA KUSIKITISHA KAMA HUO. MWAKA JANA MAALBINO WAWILI WALIUWAWA KIKATILI NA SEHEMU ZA VIUNGO VYAO KUCHUKULIWA


From Michuzi Blog
 
kama mwandishi anaweza yote haya jeshi la polisi linashindwa nini?
 
Hata hivyo kuna sehemu nisikia police are involved... kumbe ni polisi kama mtu sio kama taasisi, kwani nani asiyejua idadi kubwa ya polisi ni watu waliokataa shule.

By the way tunaifanya nchi iwe na uongozi mbovu kwa sababu... tunamtwisha rais kufanya kila kitu hali ya kwamba tunajua wazi kuna taasisi zilizopo kisheria na kikatiba kulinda usalama wa raia...

Shame on those whom to do not target the exact institution supposed to work.

Kasheshe,
Hata mie nilikuwa nafikiri kama wewe hadi KUHANI alivyonishambulia na nikaamua kuisoma KATIBA YA NCHI. Ukisoma katiba na tena ipo humu ndani JF misstari michache tu juu ya RAIS NA MADARAKA YAKE na SERIKALI au Mawaziri pamoja na PM utaona kuwa RAIS ndiyo BOSS wa kila kitu na Serikali/Mawaziri (+PM) wako pale kama WASAIDIZI au WAWAKILISHI. Sasa maadamu kikatiba yeye ni BOSS na hataki kugawa madaraka kwa watu wengine kama yamemzidia, kwa nini wewe unaona ni VIBAYA watu wakiyapeleka malalamiko kwa BOSS badala ya WASAIDIZI au WaWAKILISHI?
Ndiyo maana unaona kila riport ya serikali inakwenda kwa RAIS na siyo PM au POLISI na ikifika kwa MKWERE inadoda......
Badala ya KULAANI waganga au Sangomas, naungana na wale wote wanaolaani BOSS mwenye uwezo wa kukomesha haya ila HATAKI au ANAZUIWA na DHAMIRA kwani ni hao SANGOMAS wamemuweka hapo.
Jamani hamuwezi amini juzi NIMECHEKWA na MATAIFA mengine waliosoma hii habari kwenye BBC. Kungelifanyika mpango Kikwete akienda nje basi BBC na CNN waiweke hii LIVE na yeye aulizwe.
 
Nimemsikia asubuhi waziri Lawrence Masha akihojiwa na BBC kuhusu mauaji ya Albino alikuwa mkali sana anadai swala lina kuzwa hili na hao wauaji wanashughulikiwa kama kesi zingine.Huyu jamaa sikumwelewa.

Lazima awe mkali yaelekea nae huyu ni mmoja wa wateja wa huyo sangoma
 
nyie ngojeni tu.. kwa kadiri wanaendelea kuwafumbia macho mafisadi wakubwa ndivyo wale wadogo nao wanavyokuwa wanathubutu zaidi. Hivi Kikwete anaruhusiwa hata kusoma magazeti? isije kuwa jamaa is shielded from all outside contacts.. yawezekana yeye analetewa tu vipande vya habari na hana access ya kitu anachojua yeye mwenyewe.
Mwanakijiji ,
ulishasema kuhusu hili na ukawaandikia ole wao ila wao hawakutaka kukuunga mkono hata baada ya kutoa mchango wako kwa ajili ya kukomesha suala la mauaji ya Maalbino.wenyewe wanafikiria yaliyobora ni kulinda akaunti za viongozi.

Hotuba ya wapinzani leo imempongeza Ntetema, hotuba ya waziri wa serikali haijasemea jambo hili.

Amesfanya kazi nzuri,ila alitakiwa apongezwe mwanakiji kwanza ,sababu aliandika makala kuhusu hili.ila na lenyewe ni sawa

Lazima awe mkali yaelekea nae huyu ni mmoja wa wateja wa huyo sangoma
Ndiyo hakika umenena iliyo kweli,na huyo ndiyo mmoja wao
 
Back
Top Bottom