Uzuri wa magari ya automatic na manual...!!

Hapa kuna contradictions kidogo mkuu. Unachosema nimewahi kumsikia dada mmoja wa Kijerumani akikisema pia. Lakini ni kinyume hake kwa Japani. Maana ukiingia hata kwenye mitandao ya wauza magari wote wa kijapani utakuta kuwa magari ya manual ni ghali kuliko automatic, hapa sasa sielewi.. Huenda Ulaya wamefanya hivyo ili kuwa-discourage watu kununua magari automatic ambayo wanajua matatizo yake (ni mawazo yangu tu haya).

Mi sio mtaalam wa hizo tofauti za bei Ulaya au Japan. Ila hapo kwenye red sijaelewa: nani anapanga bei za magari? Naamini anayetengeneza au anayefanya biashara ndio mpangaji mkubwa wa bei. Sasa iweje mtu atengeneze kifaa chake halafu aweke bei kubwa ili ku-discourage watu kununua? Kwa nini kama anajua kina madhara asiache kutengeneza hicho chenye madhara atafute kutengeneza kilicho salama, naomba unifafanulie kidogo hapo Mazingira
 
Dunia inakwenda inabadilika wandugu..kama una pesa nunua AT,maana bei yake imechangamka kuliko manual
AT hazina usumbufu kabisa kama watu wanavyosema,hata ukitaka ya masafa marefu we chukua engine kubwa....hapa UK magari yote ya police ni AT na mabus yote ya public transports ni AT.

Hapa bongo magari yote ya vigogo ni manual, tumeambiwa humu!
 
Jamaa yangu anayo Subaru Forester ya manual. Hivi karibuni alikuwa anataka kuiuza ili anunue gari ya manual. Lakini kuna Singa Singa fulani ambae hushiriki mbio za magari na ambae ni fundi wa magari alimshauri asiuze gari yake ya manual kwa kuwa ni imara kuliko automatic. Alimpa mfano kuwa nusu ya Forester zilizoingingizwa hapa nchini za automatic, zimekufa gear box na haziko barabarani sasa hivi. Mimi sio mtaalam lakini nilimwani kwa kwamba magari ya manual ni mazuri hasa kwenye nchi zetu hizi ambazo barabara zake nying ni za vumbi na makorongo.
 
Gearbox za Automatic zinahitaji umakini zaidi kwenye service & maintenance. Ukizembea kwenye kufanya service kwa wakati huwa zinaanza magumashi na ikifikia hapo jiandae na maumivu ya kununua gearbox mpya!!
 
Asilimia karibu 80 ya magari yote madogo yanayotengenezwa sasa ni AT.

Kuna viwanda vya magari vimeacha kabisa kutengeneza manual, wao ni AT tu

Baada ya miaka kadhaa mbeleni magari yote madogo yatakuwa AT na manual itabaki hadithi tu

Dunia inasonga mbele na teknolojia inakuwa, manual inapitwa na wakati sasa.
Watu wanasumbua vichwa kurahisisha maisha na si kupigana kubadilisha gia,
Unaweka kitu kwenye D unaondoka na si mara klachi,mafuta na kuingiza gia kila mara


Ninakuunga Mkono.
Dunia Inaendelea na teknolojia inakua na soon, magari ya manual yatakuwa-phased out.
Kwa nini? Kanuni kuu ya uvumbuzi wa magari ilikuwa ni kumsafirisha binadamu kutoka point A kwenda Point B kwa njia rahisi na nyepesi bila usumbufu mkubwa kadri inavyowezekana.
Tukumbuke kwamba hawa wanaotuletea AT sasa hivi ndio walianza na farasi, wakavumbua mikokoteni inayovutwa na ng'ombe na farasi, wakavumbua yale mastage-coach tuliyokuwa tukiyaona kwenye sinema za Cowboys na ndio waliovumbua magari ambayo mwanzo hayakuwa na tairi zenye upepo bali matairi magumu tu ambayo yalipkanyaga jiwe dogo tu yangeweza kupindua gari!
Hawa ndio ambao magari yao ya mwanzo ilibidi kupigwa 'hendel' ili kuwaka lakini sasa unaweza kuiwasha hata ukiwa nje hujaingia ndani ya gari! Yote haya ni maendeleo ya kumfanya binadamu asafiri kwa raha kutoka point A kwenda B kwa tabu ndogo kadri inavyowezekana.
Ni wazi kwamba katika muda mchache ujao watu hawa watataka binadamu kusafiri bila haja ya kutoka jasho na mapovu kugombana na gia na klachi za gari!
Pale ujerumani kuna mji ambao jina lake limenitoka kidogo ambao umetengwa maalumu kwa ajili ya majaribio ya kumuwezesha mmiliki wa gari kutoka ndani nyumba kuingia ndani ya gari na kusema tu "TO THE OFFICE" ama kuminya kuingiza tu data kwenye comp na gari hilo likakata mitaa kumpeleka ofisini huku yeye akiwa amekaa nyuma ya gari akisoma gazeti bila kuhangaika kufanya kitu chochote! Ndiko tunakoelekea.
Kuna mdau amesema kuwa kama makampuni ya magari yalikuwa yanataka ku-phase out Manual basi wangeishafanya hivyo maana magari ya AT yameanza miaka ya 80!
Tukumbuke kwamba tofauti na sisi ambao mipango yetu haivuki miaka 10 mbele, wenzetu hawa wanaweza kupaga jambo hata miaka 40 ama 100 mbele!
Isingekuwa rahisi katika kipindi cha miaka 30 tu kuanzia miaka ya 80 waweze kuyatoa barabarani magari yote ya Manual lakini ukweli wanafanya hivyo taratibu kiasi kwamba wakati mwingine inachukua muda kutambua hili.
Tukumbukeni tu kuwa miaka 20 tu nyuma tulikuwa na mabasi ya Leyland Albion ambayo dereva wake alipaswa kuwa na kifua kutokana na sukani yake na gia yake (ambayo ilikuwa inaanzia mgongoni kwa dereva!) kuwa ngumu na nzito kama zege! sasa mabasi haya ni historia na vijana wanaendesha scania na yu tong zenye vigia unavyoweza kubadilisha kwa ncha za vidole kama sio za kucha!
Mifano ipo mingi. Tulikuwa na treni za mvuke unaotokana na makaa, zikaja za dizeli na sasa wenzetu wana si tu treni za kasi za umeme bali kuna hata za sumaku ambazo treni haina magurudumu lakini inavutwa na vipande vya sumaku na kuwa 'inaelea' kwenye njia zake badala ya magurudumu ya vyuma!
Tulianza na 'glamaphone' ambazo ilibidi uweke 'ufunguo' ndipo icheze santuri zako, ikaja 'changer' ambazo tulipanga santuri sita zikawa zinadondoka moja moja na kucheza lakini sasa ninaamini kuna nyumba chache sana ambazo zina kitu kinachoitwa Record Player wakati watoto wetu sasa wanatunza hata nyimbo 100 kwenye IPod IPad na I nini sijui zao na kuzicheza wakati wowte na mahali popote wapendapo!
Na Remote Control je? Katika vifaa mbavyo mwanzo nilivipiga vita kwa kuona ni kwa ajili ya Wavivu tu,ilikuwa ni remote control! Lakini imebidi nikubaliane tu kwamba haya ni maendeleo ambayo yananifanya niweze kubadilisha stesheni, kupandisha na kupunguza sauti nikiwa nimelala kivivu kwenye kochi bila kulazimika kunyanyuka ama kumuita mtu anifanyie hivyo!!

Kwa hiyo tutake tusitake, miaka si zaidi ya 25 tu ijayo magari ya Manual yatakuwa kwenye majumba ya makumbusho na pengine tutakuwa tunabishana kuhusu Uzuri wa magari kati ya yale ya AT na yanayoendeshwa kwa kupewa amri tu na mdomo; "Kata kushoto!", "Simama!" "Piga hon!" "Ongeza Spidi!" na kadhalika na kadhalika!
Mabadiliko ni lazima. Tujiandae tu kuyapokea.
 
Jamaa yangu anayo Subaru Forester ya manual. Hivi karibuni alikuwa anataka kuiuza ili anunue gari ya manual. Lakini kuna Singa Singa fulani ambae hushiriki mbio za magari na ambae ni fundi wa magari alimshauri asiuze gari yake ya manual kwa kuwa ni imara kuliko automatic. Alimpa mfano kuwa nusu ya Forester zilizoingingizwa hapa nchini za automatic, zimekufa gear box na haziko barabarani sasa hivi. Mimi sio mtaalam lakini nilimwani kwa kwamba magari ya manual ni mazuri hasa kwenye nchi zetu hizi ambazo barabara zake nying ni za vumbi na makorongo.


...Mkuu, kama NUSU ya Forrester zote zilizoingizwa nchini za Automatic zimekufa Gear Box Nilidhani litakuwa zaidi tatizo ma Manucaturers wa aina hiyo ya gari na sio kwamba kwa sababu ya kuwa AT, au???
 
rafiki yangu ni mnywaji wa pombe, huwa ananiambia bora manual kwani akiwa anaendesha hawezi pata usingizi atakuwa busy kucheza na kirungu tofauti na auto ambayo itamfanya asinzie na pengine kuweza kusababisha ajali
 
mimi sijui magari!!lakini naona watu wamekupa sifa nzuri za MANYO...Nunuaga MANYO Kijana juzi...tupeane lift ukishaweza kulimudu lakini!
 
Automatic transmission zina matatizo yake hujakuta inajiresi yenyewe halafu uko kwenye foleni,usiombe likukute wenyewe wanataaka kuyaondoa
 
Basi kama ni rahisi kutengeneza kama ilivyo kuendesha, hapa kwetu kuna viwanda vingapi? Au unamaanisha hizo auomatic zinatengenezwa nchi gani? Ni huku kwetu bongo ambako hatujaendelea au ni wapi? Mi nilikuwa naamini wenye viwanda vya kufyatua magari wanatengeneza Manual, Automatic na Automanual na kutuachia wenyewe tuchague tunataka nini. Kumbe si kweli nimefahamu leo kuwa jamaa waliopiga hatua wanatengeneza, na kununua manual tu! Asante kwa kunifungua akili. When I 'grow' up na kupata uwezo wa kumiliki na kujifunza kuendesha gari, basi nitajifunz kuendesha manual, na nitajaribu kununua manual coz I dont want to be branded a lazy person...or a girl, which I'm not!

Hizo gari kabla ya hapo ilikuwa ni mpango wa kusaidia vilema. Lakini ndio sasa imekuwa fashion.
 
Ninakuunga Mkono.
Dunia Inaendelea na teknolojia inakua na soon, magari ya manual yatakuwa-phased out.
Kwa nini? Kanuni kuu ya uvumbuzi wa magari ilikuwa ni kumsafirisha binadamu kutoka point A kwenda Point B kwa njia rahisi na nyepesi bila usumbufu mkubwa kadri inavyowezekana.
Tukumbuke kwamba hawa wanaotuletea AT sasa hivi ndio walianza na farasi, wakavumbua mikokoteni inayovutwa na ng'ombe na farasi, wakavumbua yale mastage-coach tuliyokuwa tukiyaona kwenye sinema za Cowboys na ndio waliovumbua magari ambayo mwanzo hayakuwa na tairi zenye upepo bali matairi magumu tu ambayo yalipkanyaga jiwe dogo tu yangeweza kupindua gari!
Hawa ndio ambao magari yao ya mwanzo ilibidi kupigwa 'hendel' ili kuwaka lakini sasa unaweza kuiwasha hata ukiwa nje hujaingia ndani ya gari! Yote haya ni maendeleo ya kumfanya binadamu asafiri kwa raha kutoka point A kwenda B kwa tabu ndogo kadri inavyowezekana.
Ni wazi kwamba katika muda mchache ujao watu hawa watataka binadamu kusafiri bila haja ya kutoka jasho na mapovu kugombana na gia na klachi za gari!
Pale ujerumani kuna mji ambao jina lake limenitoka kidogo ambao umetengwa maalumu kwa ajili ya majaribio ya kumuwezesha mmiliki wa gari kutoka ndani nyumba kuingia ndani ya gari na kusema tu "TO THE OFFICE" ama kuminya kuingiza tu data kwenye comp na gari hilo likakata mitaa kumpeleka ofisini huku yeye akiwa amekaa nyuma ya gari akisoma gazeti bila kuhangaika kufanya kitu chochote! Ndiko tunakoelekea.
Kuna mdau amesema kuwa kama makampuni ya magari yalikuwa yanataka ku-phase out Manual basi wangeishafanya hivyo maana magari ya AT yameanza miaka ya 80!
Tukumbuke kwamba tofauti na sisi ambao mipango yetu haivuki miaka 10 mbele, wenzetu hawa wanaweza kupaga jambo hata miaka 40 ama 100 mbele!
Isingekuwa rahisi katika kipindi cha miaka 30 tu kuanzia miaka ya 80 waweze kuyatoa barabarani magari yote ya Manual lakini ukweli wanafanya hivyo taratibu kiasi kwamba wakati mwingine inachukua muda kutambua hili.
Tukumbukeni tu kuwa miaka 20 tu nyuma tulikuwa na mabasi ya Leyland Albion ambayo dereva wake alipaswa kuwa na kifua kutokana na sukani yake na gia yake (ambayo ilikuwa inaanzia mgongoni kwa dereva!) kuwa ngumu na nzito kama zege! sasa mabasi haya ni historia na vijana wanaendesha scania na yu tong zenye vigia unavyoweza kubadilisha kwa ncha za vidole kama sio za kucha!
Mifano ipo mingi. Tulikuwa na treni za mvuke unaotokana na makaa, zikaja za dizeli na sasa wenzetu wana si tu treni za kasi za umeme bali kuna hata za sumaku ambazo treni haina magurudumu lakini inavutwa na vipande vya sumaku na kuwa 'inaelea' kwenye njia zake badala ya magurudumu ya vyuma!
Tulianza na 'glamaphone' ambazo ilibidi uweke 'ufunguo' ndipo icheze santuri zako, ikaja 'changer' ambazo tulipanga santuri sita zikawa zinadondoka moja moja na kucheza lakini sasa ninaamini kuna nyumba chache sana ambazo zina kitu kinachoitwa Record Player wakati watoto wetu sasa wanatunza hata nyimbo 100 kwenye IPod IPad na I nini sijui zao na kuzicheza wakati wowte na mahali popote wapendapo!
Na Remote Control je? Katika vifaa mbavyo mwanzo nilivipiga vita kwa kuona ni kwa ajili ya Wavivu tu,ilikuwa ni remote control! Lakini imebidi nikubaliane tu kwamba haya ni maendeleo ambayo yananifanya niweze kubadilisha stesheni, kupandisha na kupunguza sauti nikiwa nimelala kivivu kwenye kochi bila kulazimika kunyanyuka ama kumuita mtu anifanyie hivyo!!

Kwa hiyo tutake tusitake, miaka si zaidi ya 25 tu ijayo magari ya Manual yatakuwa kwenye majumba ya makumbusho na pengine tutakuwa tunabishana kuhusu Uzuri wa magari kati ya yale ya AT na yanayoendeshwa kwa kupewa amri tu na mdomo; "Kata kushoto!", "Simama!" "Piga hon!" "Ongeza Spidi!" na kadhalika na kadhalika!
Mabadiliko ni lazima. Tujiandae tu kuyapokea.

Nimependa narration yako, ambayo inawezekana kureflect ukweli wa mambo sambamba na mabadiriko yanavyoenda, ila kwa hili naomba unisaidie kuwa ni ushamba au ni kutaka sifa: hivi inakuwaje kuna traffic lights tena zinawaka lakini unakuta traffic polisi yupo anaongoza magari, thanks
 
Nimependa narration yako, ambayo inawezekana kureflect ukweli wa mambo sambamba na mabadiriko yanavyoenda, ila kwa hili naomba unisaidie kuwa ni ushamba au ni kutaka sifa: hivi inakuwaje kuna traffic lights tena zinawaka lakini unakuta traffic polisi yupo anaongoza magari, thanks

Hakuna kitu kinaboa kama kukalishwa saa zima kwenye foleni na trafk huku taa za kuongozea zinafanya kazi. huku ni kutothamini technology. Inakera
 
Hata tulipoanza kutumia simu mimi nimeanza na mobile yale ya kukoroga hata siyajui na wala sitaki kuyatumia tena, nafikiri hata kwenye gari inabidi iwe hivyo mimi ninyenunua gari leo si lazima ninunue manual ila nakwenda kwenye technology inayotembea sasa.
 
Home kulikua na gari ya manual tangu 1999 badae ikanunuliwa nyingine AT 2005 hadi sasa AT imekufa gearbox karibu mara 6 bt manual bado ipo na matengenezo ya manual ni rahic sn ukilinganisha na AT. Performance ya Manual ni kubwa sana kuliko ya AT. Wazungu wanasema AT ni kwa wavivu kama africans na ndo maana hata zilivyokua zinaingia tz mwanzoni zilikua zinaitwa gari za kike na walemavu japo kwa sasa almost wt twatumia. Kwa ubora manual ni zaidi kuliko AT na ndio maana hata bei zake ziko juu. Tz 2napenda sn cheap ndio maana 2mejaza AT.
 
Hakuna kitu kinaboa kama kukalishwa saa zima kwenye foleni na trafk huku taa za kuongozea zinafanya kazi. huku ni kutothamini technology. Inakera

Yaani wale jamaa huwa siwaelewi na hata sitawaelewa, hivi maana ya zile taa huwa ni nini?
 
Huo ni udhalilishaji wa jinsia ya kike. Unataka kusema wadada ndio hawawezi kutupia hizo 4, 5, ress, clutch au? Come on...naamini hata hao wadada, wapo wanaoendesha magari maunal. Kama ni wachache basi itakuwa ni kutokana na wengi kuanza kumiliki magari kipindi hiki ambacho Auto ndio zime-dominate barabara zetu hapa bongo, na si vinginevyo!
ww unadhani magari ni baiskel hivi ni mwanamke wa wapi anaweza endesha gari yenye gia 12, au umpe gari yenye rediotor unajua mliozaliwa miaka ya Automatic hamzijui FIAT na hakuna mwanamke aliyeweza endesha gari hizo za Italy au Benz siku hizi hata scania umewaona wapi? wanaenda Zambia? Lubumbashi? Kigali au mnawatetea tu tafiti kwanza
 
Hyo sasa ni sequential gearbox kama piki piki tu haina raha kabisa movement za gearstick ni back and forth manual kwa H shifter ndo nzur
 
C kwel kwamba AT zinawah badilisha gear isipokuwa ina depend na kiac gan umekanyaga . Kuna control box ambayo ukikanyaga kdogo inajua kabisa unataka kwenda mwendo wa kawaida hvo itawah badilisha gear around 2800- 3200RPM ila ukikanyaga mpaka mwisho inajua kabisa unataka kwenda mbio hvo itabadilisha kweny rpm ya mwisho
 
kama unafanya kazi ya kukaa sana nakushauri ununue manual kwani inakufanya uwe bize barabarani kuliko ukiwa AT na kingne manual uaribikaji wake huwa ni mgumu sio sawa na AT na vile vile manual hadi upate ajali ni ngumu sana..

Sababu za kingwini hizi, naomba mtoe sababu za kitaalami tafadhali.


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Back
Top Bottom