Utotole
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,604
- 4,259
Hapa kuna contradictions kidogo mkuu. Unachosema nimewahi kumsikia dada mmoja wa Kijerumani akikisema pia. Lakini ni kinyume hake kwa Japani. Maana ukiingia hata kwenye mitandao ya wauza magari wote wa kijapani utakuta kuwa magari ya manual ni ghali kuliko automatic, hapa sasa sielewi.. Huenda Ulaya wamefanya hivyo ili kuwa-discourage watu kununua magari automatic ambayo wanajua matatizo yake (ni mawazo yangu tu haya).
Mi sio mtaalam wa hizo tofauti za bei Ulaya au Japan. Ila hapo kwenye red sijaelewa: nani anapanga bei za magari? Naamini anayetengeneza au anayefanya biashara ndio mpangaji mkubwa wa bei. Sasa iweje mtu atengeneze kifaa chake halafu aweke bei kubwa ili ku-discourage watu kununua? Kwa nini kama anajua kina madhara asiache kutengeneza hicho chenye madhara atafute kutengeneza kilicho salama, naomba unifafanulie kidogo hapo Mazingira