Uzuri wa magari ya automatic na manual...!!

Uzuri wa magari ya automatic na manual...!!

He! Wanunulie manual wapate uzoefu.
Mimi watoto wangu wote nimewafundisha kuendesha manual. Hata wakinunua automatic lakini wanaweza kuendesha manual. Huwezi kuwa dreva mahiri kama huwezi kuendesha gari ya manual gear.
 
Ivi Manual zinatengenezwa tena kweli...maana nikiingia kwenye mtandao most of them ni AT....
 
binafsi nafagilia sana MANUAL haswa huku mikoani kusiko kua na foleni utaipenda.
1. wese inakula kidogo coz inakupa great control kwenye gia. mfano kwenye kilima kikubwa unapanda na namba 2 na manual lakini ikiwa AT lazma ijiset kwenye gea namba 1 ambayo ina nguvu zaidi na inakula wese.
2. manual ni nzuri kwa sehemu zisizo na foleni kama dar, wakati AT ni nzuri kwenye foleni kali, haupati maumivu ya kucheza na clutch, accelerator na breki kwa wakati mmoja.
3. vyuma vya mjapani vya manual ni cheap kuliko ATs!
4. manual ukiendesha kweli unajiona unaendesha gari na sio AT (kwa kina mama, wadada na watoto!)


hahahaaa, kweli wewe sio dereva!.
kama mlima ni mkali kama ile ya kule kimara bonyokwa au kilungule lazma likushinde, kubalance clutch na accerator its too simple than using the handbrake, maana ukicheza kidogo ikakushinda wakati wa kuachia handbrake lazma gari litazima. sasa pata picha gari ndio limeshazima linaanza kurudi nyuma halafu linatumia hydraulic, means breki hazikamati, stering inakua ngumu vibaya mno!.



uko sawa kabisa mkuu!, foleni za dar ni nuksi, ukifika home mguu wa kushoto unauma balaa kwa kucheza na clutch na breki always si unajua zile daladala linataka kukuchomekea na wewe unalibania kwa hiyo hapo lazma ufanye kazi ya ziada kucheza na clutch na breki!, lakini ukiwa na AT aaah wala haikupi shida.
kuna siku bwana nilikua naendesha manual, sasa kumbe brake fluid ilikua imevuja na ikawa imepungua sana halafu mbele yangu ndio foleni imeanza kila nikikanyaga breki nakuta holaaaa, kilichonisaidia ni kupunguza mwendo kwa kutumia gea, assume ingekua AT hapo nini kingetokea kwa gari ilokua mbele yangu.


karibu asilimia 99 ya magari ya serikali ya JMTz ni MANUAL especially kama limenunuliwa likiwa jipya kabisa!. si unajua lazma wafuate mchakato wa manunuzi, so lazma mzabuni anaeiuzia ataambiwa apeleke kitu cha manual wakijua kuna kukabiliana na barabara mbovu.
mengine yanayotolewa kama misaada au yaliyotumika kwenye miradi ndio wakati mwingine huwa AT


aaah wewe utaua gear box, yani kutoka gea namba tano uingize gea namba wani kweli!??.
unapoingiza gea lazma uingize moja baada ya nyingine KIUSALAMA na UTUNZAJI wa gearbox, hata kushusha gea pia lazma ushushe moja baada ya nyingine (labda kama una dharura endapo breki zitafeli unaweza toa 5 ukashusha mpaka moja kupunguza kasi ya injini ingawa gea itakua NGUMU sana kuingia!).

Hapo utafanyaje sasa mdau GP maana ku-balance clutch na accelerator wakati mwingine kama kigongo ni kikali unaweza clutch inanuka (au akapita nyuki hujafunga dirisha akakudhuru unashangaa unaachia clutch), unapoweka hand brake sio unalizima linakuwa silence kama kawa ila lipo kwenye gia namba moja unakuwa umekanyaga clutch na brake ku-support maana handbrake inaweza fail sometimes (ila unashitua kiana kama hivyo una balance lakini kiaina). Hii naona ni nzuri kuliko hiyo ku-balance kwa sie wa kichina yaani handbrake ukitaka kuondoka unaachia huwa inabadilisha mlio wa injini ndio na wewe unatoa handbrake. kuzima halizimi labda uwe mwanafunzi kabisa hapo kasheshe maana mwanafunzi hata tambarare kuondoka linazima hata mara tatu.
 
Last edited by a moderator:
Ubadilishaji haraka wa Gia ambao unashangiliwa sana na wahuni vijiweni na vijana kwa ujumla yaani kabla mizunguko ya injini inayo hitajika kufika huua Gari. Hivyo kwa matumizi yetu injini ya AT itadumu zaidi ya ile ya Manual.
Jambo tu la kuongezea lakini naona arguments zilizo tangalia toka kwa wadau mbalimbali ni nzuri sana zinaongeza uelewa mkubwa.
 
Mkuu namimi nichangie kidogo. Mi naona kama kazi yako si udereva na upo bize sana na shughuli zako Automatic inakufaa kwasababu huitaji kutumia akili nyingi sana kuendesha, just weka D endesha, kuliko manual ambayo naona utahitaji akili ya ziada ya kubadilisha gia kila wakati. Lakini kama unahitaji kupata ladha ya kuendesha gari then manual ni safi. Otherwise mi naona zote ni sawa tu. MTAZAMO
 
Jambo wana jf
Mimi nina yote manual 4x4 na saloon auto.
Nafaidi manual ninapokua safari za mbali hasa rough road ila kwa mjin auto ndo ideal coz of folen.

Ukweli kwamba yote ni mazuri ila cha msingi ni matumizi ROI (return on investment) na unatumia ktk mazingira gani na kipato chako kikoje na pia hw competent ur r on the wheel?
Manual ni nzuri kwa mtu bahiri ila auto haikopesheki maana kama ni hydrolic imechoka...maana yake gia hazitaingia na itakulazmu ubadilishe. General service ya auto ni ghari compare to manual. Km betri imekufa manual unaweza kushtua, auto huwezi.
 
Jambo wana jf.

Mimi nina zote na mara nyingi kwa safari fupi za hapa town na prefer auto ila kama ni long trip basi manual ndo best coz unakua bize muda. Fuel consumpt: manual is the best maana we ndo unaiendesha wakat auto inakuendesha. Kubwa zaidi auto service yake iko juu maana lazma ubadilishe hydrolic pia while manual ni engine oil tu na ofcoz filter.

Nafikiri cku zote kabla ya kununua kitu chochote ni bora uka fanya a very simple analysis kwa ku compare pros and cons hence decision, mf: ukubwa wa familia? Matumizi yako ni rough road au rami tu? 4wheels au 2wheels maana unaweza kua unaishi sehemu ambayo gari fupi haliwezi kuvumilia shida esp wakt wa masika au barabara ni mbaya sana labda mchanga mwingi au matipo so u must hv a 4x4 au unashuguri za offload eg shamba u need kubeba mbolea, miti etc lkn kubwa pia ni space maana huwezi kufikiria short chasis wakt familia yako ni zaidi ya watu watano.

Kingine ni kipato chako, maana unaweza kukuta gari linatumia zaidi yako wewe na hata ukashindwa kuliendesha labda wiki ya kwanza ya mwanzo au mwisho wa mwezi tu ( hapa nime wagusa wengi wetu) siku zingine mzee unawahi kituo cha basi. Kumbe ungeweza kuchukua stalet au vitz na Mambo yako yakawa shwari tena full mfindi aka kiyoyozi wenzetu wanasema air condotion maana wapo wenye fikra potofu kuwa a/c inakula mafuta hahaha, unakuta mtu anazima ac kisa mafuta wakat bar na guest house anatumia zaidi na mwenziwe au washikaji (hapa pia nimewa...wengi hahaha).

Anyways to make it short manual is more durable maana inatengenezeka wakati auto mara nyingi unatakiwa kunua complete componet eg ingine kumbe tatizo lilikua piston au sleeve tu. Nakaribisha maswali maana hii ndo field yangu.

Kwenye fuel consumption nakukatalia, kwani AT ina program maalumu kwa ajili ya kupunguza matimizi ya mafuta na pia wear and tears. Manual zinagharama ndogo ukilinganisha na AT
 
Manual ni gari imara sana kuliko Automatc. Unabadili gia unapoona inahitajika kufanya hivyo. Matumizi mazuri ya mafuta. Ikikataa kuwaka hauna haja ya kutafuta gari nyingine ili kuboost betri. Change down inafanyika vizuri. In short i prefer manual to automatic

We muongo. Enginw ya deseli ndiyo imara. Siyo Manual.
 
Hapa kuna contradictions kidogo mkuu. Unachosema nimewahi kumsikia dada mmoja wa Kijerumani akikisema pia. Lakini ni kinyume hake kwa Japani. Maana ukiingia hata kwenye mitandao ya wauza magari wote wa kijapani utakuta kuwa magari ya manual ni ghali kuliko automatic, hapa sasa sielewi.. Huenda Ulaya wamefanya hivyo ili kuwa-discourage watu kununua magari automatic ambayo wanajua matatizo yake (ni mawazo yangu tu haya).
siyo kuwa discourage. Maana ya AT ni kuwa na vitu vingi mfano unakuwa na GPS ipo incorporated, n.k.
 
Naomba mjiulize. Je kuna gari lolote la Serikali ya JMTz au SMZ ambalo ni automatic? Je mnaweza tujuza ni kwa nini?

Sababu madereva na abiria wao(soma mabosi) ni BBC (Born Before Bomputers), kwao shida ina raha fulani hivi. kwa hiyo vile wanavyokukuruka na clutch, brake na accelorator, wanaskia raha fulani hivi....ndiyo sababu wanapendelea manual ukilinganisha na Auto.

Kwa sisi madereva wa hii digital age....tunapenda vitu soft touch...ni kwa mantiki hiyo Auto inanoga kuliko Manual.

By the way nadhani waliogundua Auto walikusudia kufanya driving iwe simple than it was before wakati wa akina volkswagen combi/beetle, peugeot 504, landrover 109, bedford, fiat mbaula, scania 111, leyland CD, Benzi mapua etc.
 
Asilimia karibu 80 ya magari yote madogo yanayotengenezwa sasa ni AT.

Kuna viwanda vya magari vimeacha kabisa kutengeneza manual, wao ni AT tu

Baada ya miaka kadhaa mbeleni magari yote madogo yatakuwa AT na manual itabaki hadithi tu

Dunia inasonga mbele na teknolojia inakuwa, manual inapitwa na wakati sasa.
Watu wanasumbua vichwa kurahisisha maisha na si kupigana kubadilisha gia,
Unaweka kitu kwenye D unaondoka na si mara klachi,mafuta na kuingiza gia kila mara
 
Asilimia karibu 80 ya magari yote madogo yanayotengenezwa sasa ni AT.

Kuna viwanda vya magari vimeacha kabisa kutengeneza manual, wao ni AT tu

Baada ya miaka kadhaa mbeleni magari yote madogo yatakuwa AT na manual itabaki hadithi tu

Dunia inasonga mbele na teknolojia inakuwa, manual inapitwa na wakati sasa.
Watu wanasumbua vichwa kurahisisha maisha na si kupigana kubadilisha gia,
Unaweka kitu kwenye D unaondoka na si mara klachi,mafuta na kuingiza gia kila mara

Source??...hapana mkuu,autos zimeanza kutengenezwa toka 80s huko,wangekuwa wana plan ya kuacha wangeacha long t..mimi nimejifunzia auto lakini saivi niko addicted na manual,huwezi kujiita dereva unless umeendesha manual..autos hata mwanangu wa miaka mitano Marcus naweza kumuelekeza akaendesha,you can't take any pride out of it..
 
kama sehemu unayoishi hakuna foleni na ni nje ya mji mkubwa hauitaji kusimama simama, nunua manual, lakini kama ni town, auto ndiyo mpango mzima.
 
siyo kuwa discourage. Maana ya AT ni kuwa na vitu vingi mfano unakuwa na GPS ipo incorporated, n.k.

hapa tunazungumzia automatic transmission bana, haihusiani na vikorombwezo vingine ambavyo hata kwenye gari ya manual vyaweza kuwepo.
 
Back
Top Bottom