Uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria ya mama Samia - Singida, 10 Januari, 2024

Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,680
59,801
Kampeni hii ni mahususi kwaajili ya kuwafikia na kutoa msaada wa kisheria kwa Wananchi wote buree, Kampeni hii itahusisha utoaji wa Elimu ya kisheria na kusikiliza migogoro yote ya kisheria ikiwa ni pamoja na mirathi, ardhi, ndoa na usajili pamoja na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa na mengineyo kwa Wananchi wote pasipo gharama yoyote. Mgeni Rasmi; Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana Waziri wa Katiba na Sheria.


View: https://www.youtube.com/live/qFhx_o6FiWY?si=71a1STLVYxTsfztU

Serikali yazindua kituo cha msaada wa kisheria kwa wote Serikali ianzishe Kitengo cha Msaada wa Kisheria kwa Umma, sio Watu wote wanamudu kuwa na Wakili Binafsi
 
Katika kutimiza falsafa ya 4R. Hii ni moja ya hatua zinazochukuliwa na kiongozi wa Nchi yetu hii ya Tanzania.
 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria anaongea sasa.

Anaeleza Kampeni hii itafanyika kwa siku kumi mfululizo ndani ya mkoa wa singida

Kampeni hiyo itafanyika kwenye Kata, Vijiji na mitaa.
 
Kuhakikisha kwamba haki inapatika kwa wakati kwa wananchi wote.

Katika kipindi cha kampeni kutakuwa na kazi ya kutoa elimu za kisheria katika ngazi hizo.

Utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala
 
Huu ni uzwazwa haswa, una mahakama, ofisi ya DPP, TISS, polisi sijui bunge bado huamini vyombo vyako unaanzisha msaada wa kisheria.
 
Wale waliounga mkono kampeni hii ni:-
1. Wajumbe kutoka Tanzania Bara na Zanzibar
2. Ofisi ya Raisi Ikulu
3. Ofisi ya waziri mkuu sera la uratibu
Na wengine wengi wametajwa kuunga mkono kampeni hii.
 
77e659c9-ab5c-4939-8ade-d6189f1e88d4.jpg
 
Watoa huduma ya msaada wa kisheria kisheria wanaongea mbele ya waziri.
Msaada kwa kisheria mkoa wa singida unapatikana kwa bure.
 
Jane Matinde: Mwenyekiti
Kampeni ya msaada wa kisheria imeanza mwaka jana.
Tumeshuhudia:-
Ushirikiano kwa watoa huduma za kisheria
Msaada wa kisheria sasa umekubalika. Wasaidizi wa kisheria wameweza kupata majengo kwenye ofisi za serikali.
Kufikisha msaada wa kisheria maeneo ambayo hawezi kufikiwa.
Migogoro mingi imeweza kufikiwa.
Kuweza namna ya kufikia maeno mengi zaidi.
Majadiliano ya kina na endelevu ya kisheria.
Kuona namna gani mfuko unaweza kuanzishwa (Majadiliano yanaendelea)
 
Wasaidizi wa kisheria wanapewa pongezi.
Kwa mwaka migogoro 70,000 imepokelewa. Na 70% ya migogoro imeweza kutatuliwa.
Sasa ushirikiano ni muhimu ili kuweza kuona mafanikio zaodi.
Wanaahidi kuendelea kushirikiana na serikali ili kuwa na jaami yenye haki na usawa
 
Mwakilishi wa Jeshi la polisi:
Kwaniaba ya Jeshi la polisi mkoani singida. Tunaamini uharifu utapungua kwa kiasi kikubwa sana mkoani singinda. Mtusaidie sisi polisi kuweza kuwabaini waharifu. Tutasaidia mkoa wa singida kuwa na maendeleo
 
Mwakilishi Jeshi la Magereza:
Kampeni ya mama Samia kwetu Magereza inatusaidia sana. Imeongea kasi ya usikilizwaji. Wengine walikuwa ndani mle na wamedondolewa.
Baada ya kujua haki zao utulivu ndani ya magereza umeongezeka. Na kumeongeza uaminifu wa serikali kutokana na waliondani kuona kuwa kumbe nao wanasikilizwa.

Imeongeza hamasa ya watu kuwatembelea magerezani.
Hakika kabisa Mh. Rais ni mdau wa haki. Mahabusu magerezani wamepungua.
Nawapongeza
 
Hongera sana Rais wetu Samia na wasaidizi wako. Hii ni huduma hitajika kwa wengi nchi hii. Katika mambo mema yatakayoutengeneza legacy yake ni hili.
 
Bodi ya kitaifa (Sauno Malauri):
KIla mdau akashiriki ili kila mwananchi apate msaada wa kisheria. Kwa mikoa hii tuliyo pita tumeona imeleta mapinduzi ya kuleta haki.
Taasisi mbalimbali zinaunganisha nguvu pamoja na kuhakikisha aliyekosa haki anarudishiwa haki yake.
Msaada wa kisheria kwa wananchi iwe ajenda ya kila wakati. Wananchi wakiu ya kupata msaada wa kisheria kwa huduma nafuu.

Tunashauri huduma ya msaada wa kisheria uwe endelevu. Kwaniaba ya bodi nawasilisha shukurani katika wizara. Wizara iendelea kuja na mikakati kabambe
 
Mwakilishi wa wabunge(Musa SIma):
Mambo mawili:-
Tumshukuru rais kwa kutoa huduma hii ili mtanzania ajue haki yake.
Niwapmbe wananchi wananchi wa singida na wajimbo la singida mjini. Watumie fursa hii. Itatusaidia kupunguza migogoro mingi.
 
Mbona huelezi ni wapi kampeni hii inafinyika, ungetaja uwanja wa bombardier ungepungiwa nini? Unaandika harakaharaka huku huzingatii kanuni za uandishi
 
Mwenyekiti Kamati ya bunge Sheria:
Leo tunapozindua kampeni hii tunafarijika sisi kama bunge. Mimi kama mwakilishi wa mwenyekiti wa kamati natoka katika mkoa huu wa singida.
Nikupongeze waziri kwaitka suala hili la kutenda haki.
Matarajio utendaji wa kutoa haki uwe bora zaidi. Napenda kuona wizara inaenda mbali zaidi kwa wale wanojitolea.
Migogoro mingi kwetu ni Ndoa, Miradhi, Unyanyasaji na Ardhi.
Miundo mbiu ya kutolea haki imeanza kuboreshwa. Mkoa wetu wa singida imebaki wilaya mbili tu kujengwa majengo ya mahakama.

Tunajenga jengo jumuishi hapa singida. Mahakimu watafanya kazi katika mazingira bora.
Asante kwa kunisikiliza

Naitwa masale kutoka Itigi Singida
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom