Kwema Wakuu,
Ujenzi umekua gharama sana sababu ya kuongezeka kwa bei za bidhaa kunakoendana na ongezeko la bidhaa zingine zisizo za ujenzi pia.
Kwa aliejenga miaka 10 nyuma gharama hizo hizo akitaka kujenga sasa kwa nyumba ya aina ile ile anaweza asifike hata 60% ya nyumba aliojenga mwanzo kutokana na kupanda huko kwa gharama za Ujenzi.
Lakini sio kupanda kwa bei tu ambako ni "involuntary" kunakochangia kuongezeka kwa gharama za Ujenzi, bali pia uwepo wa wafanyabiashara na madalali wenye tamaa ni changamoto ingine.
Hivyo basi kupitia uzi huu tusaidiane kujulishana gharama mbalimbali za bidhaa mbalimbali za ujenzi kuanzia ufundi mpaka materials ambapo unadhani vilikua nafuu. Viwe ni vifaa halali tu ili tusileteane matatizo baadae.
Najua kuna kitu kinaitwa soko huria ambapo muuzaji akitoa bei na mnunuzi akaridhika nayo inakua halali yao wote wawili. Na pengine labda kuna wanunuzi wenze wako na wauzaji wao maalumu lakini kupitia uzi huu basi mnunuaji anaweza kufaidika kwa kujua bei ya kitu ili akienda kwa muuzaji wake ajue ana bargain vipi.
NB;
Lengo kuu la uzi huu sio kumtangazia mtu biashara ili afaidike yeye mfanyabiashara au mtoa huduma, bali kumsaidia consumer.
Karibuni.
Ujenzi umekua gharama sana sababu ya kuongezeka kwa bei za bidhaa kunakoendana na ongezeko la bidhaa zingine zisizo za ujenzi pia.
Kwa aliejenga miaka 10 nyuma gharama hizo hizo akitaka kujenga sasa kwa nyumba ya aina ile ile anaweza asifike hata 60% ya nyumba aliojenga mwanzo kutokana na kupanda huko kwa gharama za Ujenzi.
Lakini sio kupanda kwa bei tu ambako ni "involuntary" kunakochangia kuongezeka kwa gharama za Ujenzi, bali pia uwepo wa wafanyabiashara na madalali wenye tamaa ni changamoto ingine.
Hivyo basi kupitia uzi huu tusaidiane kujulishana gharama mbalimbali za bidhaa mbalimbali za ujenzi kuanzia ufundi mpaka materials ambapo unadhani vilikua nafuu. Viwe ni vifaa halali tu ili tusileteane matatizo baadae.
Najua kuna kitu kinaitwa soko huria ambapo muuzaji akitoa bei na mnunuzi akaridhika nayo inakua halali yao wote wawili. Na pengine labda kuna wanunuzi wenze wako na wauzaji wao maalumu lakini kupitia uzi huu basi mnunuaji anaweza kufaidika kwa kujua bei ya kitu ili akienda kwa muuzaji wake ajue ana bargain vipi.
NB;
Lengo kuu la uzi huu sio kumtangazia mtu biashara ili afaidike yeye mfanyabiashara au mtoa huduma, bali kumsaidia consumer.
Karibuni.