Katika maisha ya kila siku yawezekana umewahi kukutana na mtu ambaye ukiwa karibu naye akiongea au kutoa pumzi kinywani au puani utasikia harufu mbaya.
Kwa kawaida mdomo na pua huweza kutoa pumzi nje ambayo huwa na harufu asilia ambayo haiwezi kumkera mtu mwingine, lakini mara zingine hali hiyo inaweza kujitokeza kutoa pumzi yenye harufu mbaya.
Watu wa karibu au wanaokutana na mwathirika wa hali hii wanaweza wakadhani kuwa ni mchafu mwenye tabia ya kutopiga mswaki au kutosafisha kinywa chake vizuri.
Pasipo kujua kuwa upo uwezekano mtu huyo akawa na tatizo linalojulikana kitabibu kama Halitosis,maana yake ni kutoa pumzi aidha kwa mdomoni au puani yenye harufu mbaya isiyo vumilika.
Muathirika anaweza kupatwa na tatizo la woga/hofu iliyopitiliza anapokuwa kwenye kundi la watu, anaweza akajiondoa kutoka katika kundi hilo na kujitenga na vilevile, baadaye huweza kupata sonona (depression).
Tatizo hili linalowakumba asilimia 20 ya wajamii duniani, ni moja ya tatizo linalowafanya kufika katika huduma za afya kuwaona madaktari wa kinywa na meno.
Si wagonjwa wote wenye kutoa pumzi yenye harufu mbaya wana tatizo halisi la halitosis, kati ya asilimia 5 hadi 72 wanaofika katika huduma za afya hugundulika kuwa hawana tatizo hilo moja kwa moja.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.