"Nafasi hizo zimepangwa kulingana na muda na zamu. Kushindwa kuzitumia husababisha kutozwa faini. Mamlaka ya uwanja wa ndege itakabidhi kwa kampuni nyingine mwaka ujao. Hii inaweka mashirika ya ndege katika hatari ya kupoteza sehemu yao ya soko," Gonzalez alisema.
Chama cha Wanasheria wa Viwanja vya Ndege Duniani kilisema kuwa kuna ushindani kati ya mashirika ya ndege wa zamani na wapya, lakini wanawahimiza kuzingatia sheria hata kama watalazimika kuruka bila kitu.
Mashirika ya ndege ambayo yanatawala soko yanaendesha ratiba bora zaidi kwa sababu ndio ghali zaidi. Wanafika katika viwanja vya ndege wakati muhimu na kwa urahisi," Gonzalez alisema.
Mashirika ya ndege ambayo yanatawala soko yanaendesha ratiba bora zaidi kwa sababu ndio ghali zaidi. Wanafika katika viwanja vya ndege wakati muhimu na kwa urahisi," Gonzalez alisema.
Mkurugenzi wa Chama cha Kimataifa cha Usafiri wa Anga Willie Walsh alisema baadhi ya ndege hulazimika kufanya kazi na abiria wachache au bila ili zisipoteze nafasi iliyopangwa kwa ajili ya kuruka.
Mtoa huduma anayeendesha safari za ndege kati ya viwanja viwili vya ndege ataomba ruhusa kutoka kwa viwanja vyote viwili vya ndege wakati hana uwezo wa kuendesha huduma hiyo. Vinginevyo tutalazimika kurusha ndege," alisema Walsh.
Hata hivyo, watu kutoka sekta hiyo wanasema kuwa badala ya kuendesha safari hizo za ndege zikiwa tupu, ni bora kuchukua abiria kwa nauli ndogo na kuendesha huduma hizo. Kwa kweli ni jambo la kuzingatia.
Kanuni kama hizo katika sekta ya anga pia zinaathiri mazingira. Sekta ya usafiri wa anga inachangia takriban asilimia 2 ya uzalishaji wa kaboni duniani. Sekta hii inachangia asilimia 3.5 ya ongezeko la joto duniani kutokana na shughuli za binadamu.
Kanuni kama hizo katika sekta ya anga pia zinaathiri mazingira. Sekta ya usafiri wa anga inachangia takriban asilimia 2 ya uzalishaji wa kaboni duniani. Sekta hii inachangia asilimia 3.5 ya ongezeko la joto duniani kutokana na shughuli za binadamu.
Kulingana na Shirika la Kimataifa la Nishati (IEA), tangu 2000, uzalishaji huu umeongezeka kwa 50%. Sekta hiyo inatarajiwa kukua kwa zaidi ya 4% kila mwaka kwa miongo miwili ijayo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.