Mnamo mwaka wa 1989, timu ya mamluki wa Uingereza, ikiongozwa na Mskoti Peter McAleese, walisafiri hadi katikati ya himaya ya uhalifu ya mtu hatari zaidi duniani kwa lengo la kumuua.
Genge lake liIlikuwa mtengenezaji na msambazaji mkubwa zaidi wa kokeini ulimwenguni, wakati huo ilithibiti hadi 80% ya biashara ya kimataifa ya dawa hiyo.
McAleese,ajenti wa zamani wa SAS - kikundi cha kikosi maalum cha Jeshi la Uingereza - aliajiriwa na kundi pinzani la dawa za kulevya ili kumuua Escobar.
Katika filamu ya Killing Escobar , iliyoonyeshwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2021, hadithi ya misheni hiyo - ambayo iliishia kutofaulu - na mtu aliyehusika inasimuliwa.
Alihudumu huko Borneo na SAS, akishiriki katika vita vikali vilivyopiganwa msituni, kabla ya kustaafu kutoka kwa Jeshi la Uingereza mnamo 1969, uamuzi aliouelezea kuwa jambo baya zaidi kuwahi kufanya .
Alipopata tena uhuru wake, McAleese alitaka kuunda upya "msisimko" wa kazi yake ya Jeshi kwa kutafuta kazi kama "mlinzi" katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Angola na baadaye huko Rhodesia (Zimbabwe ya sasa), na pia katika Afrika Kusini.
Jorge Salcedo, ambaye alikuwa sehemu ya kundi la Cali - kundi pinzani la ulanguzi wa dawa za kulevya nchini Colombia - alikuwa akiratibu shambulio hilo na alitaka Tomkins kuajiri timu kutekeleza hilo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.