Ulishagundua kuwa ukiwa umekosa usingizi unatamani kula vitu vya sukari sukari? Kuna sababu kubwa ya hilo. Kukosa usingizi kuna uhusiano wa moja kwa moja na kula kupita kiasi na kunenepa ovyo.
Kuna homoni mbili ndani ya mwili wako zinazosimamia hali ya kujisikia njaa na kushiba. Ghrelin husisimua hamu ya kula na leptin hupeleka ishara kwenye ubongo pale unapokuwa umeshiba.
Pale unapokosa usingizi unaouhitaji, kiwango cha ghrelin hupanda na kukufanya upate hamu ya kula kuliko kawaida wakati huo huo leptin inashuka na kukufanya usijisikie kushiba na kukufanya uendelee kula
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.