Paris St-Germain imeanzisha mazungumzo na kiungo wa kati wa Manchester United Marouane Fellaini. Kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 inakamilika mwishowe wa msimu huu. (Le10Sport - in French)
Mkufunzi wa zamani wa West Ham Slaven Bilic amekataa mwaliko kutoka kwa West Brom kuzungumzia kuhusu wadhfa ulio wazi wa mkufunzi wa klabu hiyo. (Daily Mail)
Stoke, West Ham, Everton na Southampton wana hamu ya kumsajili mshambuliaji wa Watford Odion Ighalo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alielekea katika klabu ya ligi ya Superleague nchini China Changchun Yatai mwezi Januari. (Tutto Udinese, via Stoke Sentinel)
Kiungo wa kati wa Uhispania Juan Mata, 29, anataka kuongeza kandarasi yake katika klabu ya Manchester United na amesema kuwa anaweza kucheza hadi kufika miaka 40.. (ESPN)
Mshambuliaji wa Ubelgiji Eden Hazard, 26, amesema kuwa atasalia hadi mwisho wa msimu kutathmini hatma yake katika klabu ya Chelsea (Canal+ via Independent)
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.