Uwezekano wa kuenea kwa salafi jihadi nchini Tanzania

Mengine mengi wanafanya sirini huku yalihodhahiri ni macheche sn
Katika imani, kutenda dhambi manake kwenda kinyume na dini yako. Na nafikiri hakuna dini/kundi lilosalimika na wale wanaotenda dhambi.

Sasa kama wanatenda dhambi zao kisiri siri ni wao na Mungu wao.

Kwaio kama wewe unauhukumu uislam kwa watu laki 2 wakati kuna watu bilioni hawafanyi wanachokifanya hao laki mbili, basi ni vyema ungesoma ukajua nini kinaendelea.

Akili tumepewa tuzitumie na sio tuendeshwe na Medias. Hivi wewe hujiulizi, kwanini Muuaji akiwa jina la kiislam basi media wanamwita gaidi? Kwanini muuaji wa kizungu haitwi gaidi? utasikia alikuwa ana mental issues, au depression. Au huoni yakitokea hata kwa watu weusi?

By the way, kama lipi hufanywa kwa siri ambalo lingekuwa dhahiri basi lingeashiria kitu kibaya?
 
Bado sijaona la maana; halafu unavyojipaisha " Mwanadiplomasia na Mchambuzi wa Masuala ya Ugaidi katika bara la Afrika " rudi darasani
 
Uislamu sio ugaidi .usalafi ndo ugaidi.
Screenshot_20200613-193235.jpg
 
Unachanganya hbr.....bokoharamu, isis, alkaeda, etc wanajitetea na nn? Mbona wote hao wanadoma Quran kabla ya kufanya mauaji? Kwasababu ndivyo ilivyo andikwa
Kusoma Quran ni habari nyengine na kuifanyia kazi habari nyengine. Lililo haswa ni kuifanyia kazi kwani utaishi nayo. Quran inatutaka tujadiliane na watu kwa wema.

Mtume anasema watu wawili Mwenyezi Mungu hatowatizama kwa rehma siku ya Qiyama. Mosi ni mwenye kukata udugu! Pili, jirani muovu!

Uislam unafundisha maadili mema kwa maana tabia! Na tabia njema inafahamika ipoje! Ndiyo wana wa zuoni wa Kiislam wanasema "Aliye na maadili zaidi yako pia ni mwenye imani safi zaidi yako."

Mfano wa hayo iwezekanaje anayefuata hayo awe gaidi? Ikiwa ni gaidi ujue mafundisho anayoyapata si mafundisho sahihi kuhusu Uislam.
 
Maudhui yako ipo sawa Chief

Ila usiegemeze na Usalaf

Inaposemwa neno SALAF
Maana yake kilugha,Waliotangulia
Ama Kisheria
Ni Mtume wa Allah ﷺ na Maswahaba zake na watakaokuja baada yao,huku wakifuata njia sahihi

Mtu anaposema
Mimi ni Salaf
Anamaanisha
Mm namfuata Mtume wa Allah ﷺ(Dini) kwa ufahamu wa Maswahaba na Waliokuja baada yao kwa wema

TANBIH
Kujiita Mtu kuwa ni Salaf,si kigezo kisheria kuwa ni Salaf
Bali kigezo ni
Kufuata Kitabu na Sunna Sahihi kwa ufahamu wa Wema waliotangulia,kuanzia....
1)Itikadi
2)Tabia
3)Njia ya kulingania/kufikisha ujumbe


Shukran sana
بارك الله فيكم
Athari za Salafi -Jihad kuenea katika nchi yetu ya Tanzania, Kwanza ningependa kuchukua nafasi hii kumshukuru MwenyeziMungu mwingi wa Rehma na mwenye Kurehemu, Kabla ya hili janga la Corona tunalopitia hivi sasa mwanzoni mwa mwaka 2019 kulikua kuna matukio mbalimbali ya Ugaidi yaliyokua yanajitokeza katika pande mbalimbali za Africa. Ukiachana na nchi kama Mali, Burkina Faso na Libya ambazo zipo mbali kidogo na ukanda huu wa Africa Mashariki , kuna nchi katika upande wa Afrika Mashariki ambazo zina chembechembe za Ugaidi.

Inajulikana kua Tanzania ilikua moja ya nchi ambazo zilitoa au “kurecruit” wanamgambo wa Al Shabab kule Somalia. Mikoa iliyoongoza kutoa wanamgambo wengi ni Tanga, Mwanza na Dar es Salaam. Katika kipindi kile tulishuhudia kijana wa Kitanzania akihusishwa na mashambulizi ya Garissa. Kijana mstaarab alieyetoka katika familia ya kitajiri ya MBERESERO. Naam nipende kushukuru jeshi la Polisi kipindi kile wakishirikiana na Intelligency kupambana na janga lile sanasana ningependa kumshukuru DCI wa kipindi kile CP Diwani Athumani.

Ukiachana na hayo, mwanzoni mwa mwaka 2020 kuna matukio mengi ya Kigaidi yalikua yanatokea saana katika ukanda wa Afrika ya mashariki pamoja na Kusini , specifically nchini Msumbiji (Mozambique) pamoja na Kenya. Hii inatokana na uwepo wa makundi ya Waislam wenye Itikadi kali za Salafi.

Hii inaleta picha mpaka kule Africa ya Kati ambapo mpaka saiv bado kuna kavuguvugu ka udini kanatawala baina ya “Seleka” na “Anti Balaqa”. Makundi ya Salafi yaliyopo Mozambique yanafanya harakat zake karibia na mpaka wa nch iyetu ya Tanzania na hivo bas kuhatarisha usalama wa Raia kwa ujumla. Hofu yangu kubwa ni kuona baadhi ya Vijana wa Kiislamu kushawishika kuingia katika makundi hayo ya kigaidi kama ilivyotokea miaka iliyopita kule Somalia.

Hivyo bas vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama vinapaswa kuzingatia hayo mambo yasijurudie tena. Bado tunahitaj nguvu kazi katika Taifa letu na hivyo bas VIjana wakiiIslam tusishwawishike katika kuyaendea hayo mambo. Mikoa iliyo hatarini zaidi ni ile iliyopo kusini ikiwemo LIndi na Mtwara na ni mikoa ambayo Idadi ya wakazi wengi wao ni waislam .

Na kwa jinsi Serikali ilivyofocus kwenye suala la Corona unawapa muda zaidi kujipanga na kuandaa mikakati madhubuti. Sitoshangaa baada ya kuisha kwa Janga la Corona, janga la Ugaidi kuchkua nafas kama vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama havitatilia mkazo dalili hizi.

ABDULKARIM MZEE

Mwanadiplomasia na Mchambuzi wa Masuala ya Ugaidi katika bara la Afrika


rucotz98@gmail.com
 
Kuna hadithi siikumbuki vizuri nadhani ni wakati mtume anaelekea ukingoni alisema “jihadi ya vita vita imeisha, jihadi iliyobaki pekee ni baina ya mtu na nafsi yake tu”

Sasa ndugu zangu hawa wanaoenda pigana hovyo huwa sijui wanawaza nini, nadhani haya ni madhara ya kusoma dini pekee bila kusoma vingine(kujua dunia inaendeshwaje) mtu anakuwa ni rahisi saana kuwa brainwashed hasa kama uwezo wake wa kufikiria na kupambanua mambo ni mdogo.

Asilimia kubwa ya wanaopigana jihadi wanaenda kuwatumikia makafiri(marekani bila kujijua) wanaenda kuwa sehemu ya kukamilisha mipango ya watu bila kujijua.


Atleast kidoooogo jihadi wapigane wapalestina maana imeandikwa

Aya ya kwanza ya Jihadi ndogo, mapambano ya silaha, ambayo ilishuka kwa wakati huo, imo kwenye Sura ya 22 ya Qur’an Tukufu, aya ya 39-40. inaelezea wazi kabisa lengo la hii Jihadi ndogo:

“Imeruhusiwa (kupigana) kwa wale ambao wanapigwa, kwa sababu wamedhulumiwa, na kwa hakika Mwenyezi Mungu anao uwezo wa kuwasaidia, wale ambao wametolewa majumbani mwao bila sababu ya haki………”

Halafu tena ikizungumzia kuhusu wale makafiri wa Makkah ambao walipigana vita baada ya vita dhidi ya Mtume na wafuasi wake huko Madina, Qur’ani Tukufu katika sura ya 2, aya ya 190 inasema:

“Na wapigeni vita katika njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanakupigeni vita, wala msiruke mipaka, hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wanaoruka mipaka.”


Reasoning kubwa saana inahitajika katika mambo haya.
Jihadi ipo, na Mtume hakusema kuwa imekwisha. Isipokuwa Mtume aliita hii ni jihadi ndogo. Mfano wa jihadi hiyo ni aliyopigana Mtume na waliyopigana maswahaba. Au mfano wa vita aliyopigana mwana wa zuoni aliyeitwa Abuu Qudamah. Jihadi hii ni jihadi ambayo lengo si kuleta vurugu, uhasama, chuki na ubaguzi na umwagaji wa damu kwenye jamii. Bali hii ni kuletaamani,utulivu umoja na haki kwenye jamii. Ni jihadi ambayo haibagui.

Masikitiko ni kuwa jihadi hii wapo miongoni mwa madhehebu ndani ya Uislam wanaielewa vibaya mno!

Mfano mzuri wa usahihi wa hii jihad ni Khalifa Umar Ibn Al Khatwaab aliombwa msaada na wakristo wa Syria dhidi ya ufisadi na umwagaji wa damu wanaofanyiwa na Dola ya wa-Roma. Amani haipo! Utulivu wa nafsi haupo! Uislam ukaenda kuwasaidia Wakristo wa Syria na Dola ya Kirumi ikashindwa. Huu ni sehemu ya mfano wa historia ili kuonyesha jihadi ya kugharimu uhai wa mtu ipoje. Hii jihadi Mtume ameiita jihadi ndogo.

Hii ni pindi Mtume na Maswhaba waliporejea kutoka katika vita vya Tabuk, vita vilivyoitwa “Vita vigumu” kutokana na
asili yake magumu yaliyopatikana ndani yake, Mtume- rehema na amaniziwe juu yake- aliwageukiwa maswahaba zake na kuwaambia, “Sasa hivitumetoka kwenye jihad ndogo na tunaelekea kwenye jihad kubwa”. Maswahaba walistaajabishwa na hivyo wakamuuliza Mtume- rehema na amani ziwe juu yake, “Je jihad ipi kubwa zaidi ya hii?”, Mtume- rehema na amani ziwe juu yake- akajibu, “Kwa hakika kwa sasa tumetoka kwenye jihad ndogo na tunaelekea kwenye jihad kubwa...jihad dhidi ya nafsi”

Jihadi kubwa ni jihadi ambayo wengi wa Waislam wameiacha, ndiyo jihadi ambayoitakayo mpeleka kwa Mungu salama. Kwa sababu ni jihadi ambayo mtu anapambana na nafsi yake. Ni usafi wa moyo mbele ya Mola wako. Ni usafi wa kuulinda moyo dhidi ya matamanio yote dhidi ya dunia. Usafi huu ndiyo umebeba msingi mkubwa wa imani! Kushindwa kutekeleza matendo ya ibada kwa moyo safi na kuruhusu nafsi kukuendesha kutaleta madhara makubwa.

Jihadi hii ni kuusafisha moyo, moyo ukitakasika nafsi nayo inatakasika. Nafsi ikitakasika mtu anakuwa na maadili. Mwenye maadili anakuwa na moyo wa huruma, huyo mtu anakuwa muadilifu, ni mwenye tabia njema.

Asili ya moyo ni kwamba umefunikwa na utukufu wa Mwenyezi Mungu; kwa maneno mengine, ni sehemu ambayo Mola wetu anapatazama wakati wote, na hivyo moyo uko wazi kupokea maamrisho matakatifu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa sharti kuwa uwe umesafishwa dhidi ya matamanio ya kidunia na ubinafsi. Moyo ambao umegubikwa na matamanio haya unakuwa hauko safi kiimani na hivyo hauwezi kupokea ufunuo kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Binafsi mimi nilichagua kuchukua hii njia miaka 2 iliyopita. Masheikh wenye elimu ya kulea nafsi wanapewa majina mabaya kabisa na Waislam wenyewe. Nilivyoamua kwenda kwao sikuenda kwa fikra ya kuwa wao ni wakosefu bali nilikwenda na fikra ya kutaka kuujua ukweli. Hawa Masheikh ni Masheikh wa Kisufi! Wa ki-Twariqah! Allah ni shahidi juu hili; Hawa Masheikh ndiyo wameibeba dini ya Uislam. Kukaa nao kote hawajanifundisha kumchukia mtu! Hata aliyenitendea ubaya wanasema nisimchukie?!

Binafsi ni Sunnih! Madhehebu ya Shafii ninayefuata Twariqah ya Imamul Auliyaa Sheikh Abdul Qadir Al Jaylaan.

Imenifunza nisiishi na hate au kujiona ni bora, kudharau mtu wa aina yoyote, hekima itangulie zaidi. Nisiwe na roho ya kwa nini, imenifunza mwenzangu akipata chema nifurahi, niishi na watu kwa wema. Kufanya bila kutizamia watu watakufikiriaje! Kuwa mnyenyekevu na kufanya kwa ajili ya Mungu,ukiangalia mema yote tuliyoamrishwa ni kuleta mahaba ndani ya jamii yasiyobagua. Ustadhi huwa anasema "Kabla ya dini yatangulie mahaba". Huwezi kumfuata Mtume kabla haujampenda.

Indonesia walikwenda Waislam 9 tu ambao hata kiindonesia hawakijui. Walizungumza nao kwa lugha ipi? Kwa lugha ya mahaba(Upendo)! Ndivyo Mtume na Maswahaba walivyoishi! Mtume alikuwa ni mpole sana. Upole ambao maswahaba wanasema ulikuwa ni wenye kutisha! Kwa maana alikuwa ni mpole mpaka mtu kufanya jambo baya kwake unaogopa!

Hii ndiyo jihadi kubwa ambayo Waislam wanapaswa kupambana nayo. Jihadi ya nafsi! Ni jihadi baina yako wewe na nafsi yako na sheytwaani.
 
Jihadi ipo, na Mtume hakusema kuwa imekwisha. Isipokuwa Mtume aliita hii ni jihadi ndogo. Mfano wa jihadi hiyo ni aliyopigana Mtume na waliyopigana maswahaba. Au mfano wa vita aliyopigana mwana wa zuoni aliyeitwa Abuu Qudamah. Jihadi hii ni jihadi ambayo lengo si kuleta vurugu, uhasama, chuki na ubaguzi na umwagaji wa damu kwenye jamii. Bali hii ni kuletaamani,utulivu umoja na haki kwenye jamii. Ni jihadi ambayo haibagui.

Masikitiko ni kuwa jihadi hii wapo miongoni mwa madhehebu ndani ya Uislam wanaielewa vibaya mno!

Mfano mzuri wa usahihi wa hii jihad ni Khalifa Umar Ibn Al Khatwaab aliombwa msaada na wakristo wa Syria dhidi ya ufisadi na umwagaji wa damu wanaofanyiwa na Dola ya wa-Roma. Amani haipo! Utulivu wa nafsi haupo! Uislam ukaenda kuwasaidia Wakristo wa Syria na Dola ya Kirumi ikashindwa. Huu ni sehemu ya mfano wa historia ili kuonyesha jihadi ya kugharimu uhai wa mtu ipoje. Hii jihadi Mtume ameiita jihadi ndogo.

Hii ni pindi Mtume na Maswhaba waliporejea kutoka katika vita vya Tabuk, vita vilivyoitwa “Vita vigumu” kutokana na
asili yake magumu yaliyopatikana ndani yake, Mtume- rehema na amaniziwe juu yake- aliwageukiwa maswahaba zake na kuwaambia, “Sasa hivitumetoka kwenye jihad ndogo na tunaelekea kwenye jihad kubwa”. Maswahaba walistaajabishwa na hivyo wakamuuliza Mtume- rehema na amani ziwe juu yake, “Je jihad ipi kubwa zaidi ya hii?”, Mtume- rehema na amani ziwe juu yake- akajibu, “Kwa hakika kwa sasa tumetoka kwenye jihad ndogo na tunaelekea kwenye jihad kubwa...jihad dhidi ya nafsi”

Jihadi kubwa ni jihadi ambayo wengi wa Waislam wameiacha, ndiyo jihadi ambayoitakayo mpeleka kwa Mungu salama. Kwa sababu ni jihadi ambayo mtu anapambana na nafsi yake. Ni usafi wa moyo mbele ya Mola wako. Ni usafi wa kuulinda moyo dhidi ya matamanio yote dhidi ya dunia. Usafi huu ndiyo umebeba msingi mkubwa wa imani! Kushindwa kutekeleza matendo ya ibada kwa moyo safi na kuruhusu nafsi kukuendesha kutaleta madhara makubwa.

Jihadi hii ni kuusafisha moyo, moyo ukitakasika nafsi nayo inatakasika. Nafsi ikitakasika mtu anakuwa na maadili. Mwenye maadili anakuwa na moyo wa huruma, huyo mtu anakuwa muadilifu, ni mwenye tabia njema.

Asili ya moyo ni kwamba umefunikwa na utukufu wa Mwenyezi Mungu; kwa maneno mengine, ni sehemu ambayo Mola wetu anapatazama wakati wote, na hivyo moyo uko wazi kupokea maamrisho matakatifu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa sharti kuwa uwe umesafishwa dhidi ya matamanio ya kidunia na ubinafsi. Moyo ambao umegubikwa na matamanio haya unakuwa hauko safi kiimani na hivyo hauwezi kupokea ufunuo kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Binafsi mimi nilichagua kuchukua hii njia miaka 2 iliyopita. Masheikh wenye elimu ya kulea nafsi wanapewa majina mabaya kabisa na Waislam wenyewe. Nilivyoamua kwenda kwao sikuenda kwa fikra ya kuwa wao ni wakosefu bali nilikwenda na fikra ya kutaka kuujua ukweli. Hawa Masheikh ni Masheikh wa Kisufi! Wa ki-Twariqah! Allah ni shahidi juu hili; Hawa Masheikh ndiyo wameibeba dini ya Uislam. Kukaa nao kote hawajanifundisha kumchukia mtu! Hata aliyenitendea ubaya wanasema nisimchukie?!

Binafsi ni Sunnih! Madhehebu ya Shafii ninayefuata Twariqah ya Imamul Auliyaa Sheikh Abdul Qadir Al Jaylaan.

Imenifunza nisiishi na hate au kujiona ni bora, kudharau mtu wa aina yoyote, hekima itangulie zaidi. Nisiwe na roho ya kwa nini, imenifunza mwenzangu akipata chema nifurahi, niishi na watu kwa wema. Kufanya bila kutizamia watu watakufikiriaje! Kuwa mnyenyekevu na kufanya kwa ajili ya Mungu,ukiangalia mema yote tuliyoamrishwa ni kuleta mahaba ndani ya jamii yasiyobagua. Ustadhi huwa anasema "Kabla ya dini yatangulie mahaba". Huwezi kumfuata Mtume kabla haujampenda.

Indonesia walikwenda Waislam 9 tu ambao hata kiindonesia hawakijui. Walizungumza nao kwa lugha ipi? Kwa lugha ya mahaba(Upendo)! Ndivyo Mtume na Maswahaba walivyoishi! Mtume alikuwa ni mpole sana. Upole ambao maswahaba wanasema ulikuwa ni wenye kutisha! Kwa maana alikuwa ni mpole mpaka mtu kufanya jambo baya kwake unaogopa!

Hii ndiyo jihadi kubwa ambayo Waislam wanapaswa kupambana nayo. Jihadi ya nafsi! Ni jihadi baina yako wewe na nafsi yako na sheytwaani.
Mkuu
umenena mazuri sana
Ila kuna sehemu kwa bahati mbaya umeteleza

Uislam unafunza Tabia njema,na miongoni mwa Tabia njema,ni kusamehe na kutoweka chuki hususan kwa ndg yako Muislam

Lkn
Uislam hausimami,isipokuwa kwa mambo makuu mawili
1)ITIKADI SAHIHI
2)TABIA NJEMA(Ambayo ndani yake kuna njia Sahihi)

Kosa lako lipo sehemu moja tu Mkuu
Uliposema kuhusu Masheikh wa Kisufi
Masheikh wengi wa Kisufi,wamepomoka mno katika Itikadi(wameharibu sana)
Na hili ni kosa kuu

Fuatilia hili kwa ukaribu na uadilifu,utakuja kuniunga Mkono siku moja,ikiwa ww ni Mtu wa Elimu

Shukran sana
بارك الله فيك
 
Kosa lako lipo sehemu moja tu Mkuu
Uliposema kuhusu Masheikh wa Kisufi
Masheikh wengi wa Kisufi,wamepomoka mno katika Itikadi(wameharibu sana)
Na hili ni kosa kuu
Weka mfano hai katika hili. Kupomoka kwao ni kwa vipi!

Karibu.
 
Akhuy
Allah akubaarik sana,wengine sisi,hatuna uweledi wa kuandika saana

Nakuomba hili ulifuatilie kwa ukaribu sana,nataraji utapata majibu sahihi
Namuomba Allah atujaalie ni wenye kusikia haki na kuweza kuifuata
Nafikiri itakuwa ni vizuri ukielezea kwa uwazi. Yaani isiwe kiujumla.
 
Katika imani, kutenda dhambi manake kwenda kinyume na dini yako. Na nafikiri hakuna dini/kundi lilosalimika na wale wanaotenda dhambi.

Sasa kama wanatenda dhambi zao kisiri siri ni wao na Mungu wao.

Kwaio kama wewe unauhukumu uislam kwa watu laki 2 wakati kuna watu bilioni hawafanyi wanachokifanya hao laki mbili, basi ni vyema ungesoma ukajua nini kinaendelea.

Akili tumepewa tuzitumie na sio tuendeshwe na Medias. Hivi wewe hujiulizi, kwanini Muuaji akiwa jina la kiislam basi media wanamwita gaidi? Kwanini muuaji wa kizungu haitwi gaidi? utasikia alikuwa ana mental issues, au depression. Au huoni yakitokea hata kwa watu weusi?

By the way, kama lipi hufanywa kwa siri ambalo lingekuwa dhahiri basi lingeashiria kitu kibaya?
Acha porojo, futeni vifungu vinavyohamasisha na kuhalalisha mauaji kwa waliotofauti na uislamu....
 
Hakuna Kifungu chenye kuhalalisha kuuliwa asiekuwa Muislam
Hakuna
Hakuna
Hakuna

Bali
Vifungu,vinabebana vyenyewe kwa vyenyewe,
Kwamfano
Atauliwa mtu asiekuwa Muislam,Ikiwa ni wa mwanzo katika kuupiga Vita Uislam,
Na kama ameupa amani Uislam na Waislam,Ni Haraam mtu huyu kuuwawa,na iwapo atatokea Muislam atamuuwa mtu huyu,Adhabu ni kutosikia hata harufu ya Pepo,si kuingia tu Peponi,Bali hatonusa hata Harufu nzuri ya Pepo.

Kila jambo limewekewa Sababu kisheria Chief
Kuwa na amani sana
Acha porojo, futeni vifungu vinavyohamasisha na kuhalalisha mauaji kwa waliotofauti na uislamu....
 
Akhuy
Allah akubaarik sana,wengine sisi,hatuna uweledi wa kuandika saana

Nakuomba hili ulifuatilie kwa ukaribu sana,nataraji utapata majibu sahihi
Namuomba Allah atujaalie ni wenye kusikia haki na kuweza kuifuata
Unachonisihi nimelifuatilia kwa miaka ila nilichogundua ni kuwa kuna baadhi ya Waislam na Masheikh wenye kuitakidi hivyo pia wana wazungumzia Sufi pasipo kuwajua.

Hii inatokana na wao wenyewe kuwazungumzia kwenye baadhi ya vitabu vyao kisha wanajihitimishia kuwa Sufi wapo hivi: Kuwa Sufi ni grave worshippers (Waabudu Makaburi), Sufi ni washirikina n.k. Inafika pahala wana watuhumu na kuwatukana Sufi mpaka wanawatukana na Maimam ambao Sufi wanafuata mienenendo yao. Usimpe sikio pekee anayelalamikia kadhia fulani, mpe sikio na anayelalamikiwa kisha utajua uhakika wa mambo jinsi ulivyo.

Imam Ibn Hajar Al Asqalani kwenye Fat'h Al Baari 2nd volume na Sahihi chain kutoka kwa Imam Al Bayhaqi na Al Haakim na Ibn Khuzayma imepokewa kwamba: Bilal Ibn Al Haarith alikwenda kwenye kaburi la Mtume kipindi cha Aamu rramada Ukhalifa wa Umar na akisimama kwenye kaburi la Mtume akasema; " Yaa rasuulallah! Ardhi na mimea imenyauka, tafadhali tuombee kwa Mungu atunyeshelezee mvua kwa ummah wako"

Unaielewaje hii?

Imam Malik anasema: " Whoever studies tafaqaha and didn't study Sufism will be corrupted, and whoever studied Sufism and didn't study tafaqaha will became a heretic, and whoever combined both will be reach the truth. [The Scholar Ali Al Adawi volume.2 p 195]

Imam Ahmad Ibn Hambal: O My son, you have to sit with people of Sufism, because they are like a fountain of knowledge and they keep the remembrance of Allah in their hearts. They are the ascetics and have the most spiritual power [ Tanwir Al Quluub p. 405]

Imam Shafii kawazungumzia pia kwa wema mzuri watu wa Sufi na akasema amekaa kwao na amepata kujifunza dini kwao. ImamAbuu Hanifa kadhalika naye ni vivyo hivyo kuwa ni watu wema kwenye Ad Dur Al Mukhtar vol. 1 p. 43.

Unawazungumzia vipi hao Maimam kwa walichokisema ama kuwazungumzia Sufi?

Nimesoma Tawhiid ndugu, itikadi sahihi naijua. Kadri nilivyozidi kusoma ndivyo kadri nilivyozidi kujua na naandika kwa wema na siyo chuki. Wanaowapinga sufi wengi wao ni Salafi! Na salafi kielimu wamejifunga! Hawaamini wala hawamfuati Imam yoyote wa Sunnih wal Jamaa bali wanawafuata Maimam wenye Itikadi ya kwao. Ikiwa kama wakimfuata Imam wa Sunnih wal Jamaa basi wanachukua kipande kinachoendana na kile kinachokwenda sambamba na kile wanachokipigania wao. Ni watu waliyoivishwa itikadi ni watu wenye uchache wa elimu.

Kadri nilivyozid kutafuta ukweli nikakuta wana wa zuoni wakubwa wote wa Madhehebu ya Hambali walikuwa ni Sufi. Hambal Saudi Arabia wanajinasibu ni dhehebu lao lakini wanakataza Tasawwuf,Kutembelea makaburi n.k. Sikutanguliza itikadi. Nilitanguliza kuujua ukweli.

Ninasoma kwa Sheikh wa kisufi na nahudhuria hafla mbalimbali na hata siku moja sijawahi kushuhudia Sufi wakimuabudu mwengine zaidi ya Allah! Watu wanasema wanamuabudu Mtume sijawahi kuona hill! Watuwanasema wanawaabudu Mawalii sijawahi kuona hili! Watu wanasema wanaabudu makaburi sijawahi kuona hili! Na kuna mengine yanazungumzwa hata sijawahi kuyasikia zaidi ya kutoka kwa hao wanaowatuhumu.

Mimi ni Sunni, madhehebu ya Imam Shafii na nimeridhia kufuata twariqah ya Sheikh Abdul Qaadir Al Jaylaan.
 
Hakuna uhusiano Kati ya ugaidi na uislam huu uzi wako ulioambatisha neno ugaid na uislam ni miendelezo wa propaganda za kuuchafua uislam, yule mkristo Alie wauwa waislam zaid ya 15+ kwa bunduki aliitwa muuaji tu, ila akiskika jina lake anaitwa Abdillah, Abdulmaleek au Hamza utaskia anaitwa gaidi mwenye itikadi kal ya kiislam,
Msiuchafue uislam kwa kuuwekea taswira za ugaid, wengi mnao waita magaidi wenye itikadi za kiislam mlishawafanyia dhulma wameaamua kulipa kisas wao Kama wao lakin matokeo yake mnatangaza kuwa uislam ndo unafanya ugaid kisa iman zao ni waislam
 
Hhhhhhh
Masha Allah
Chief,Mola akubaarik sana
Labda nikuambie jambo moja tu
Quraan pekee,ndio Kitabu Sahihi kisichokuwa na Shaka ndani yake,ama vilivyobaki,ni lazim vitazamwe na kuangaliwa Usahihi wake
Tujifunze kuchunguza kauli hizi tunazozinukuu juu ya usahihi wake,Je!kweli Imam fulani amesema hili....?!!!nk
Kisha
Huwezi kusoma kwa mtu fulani,kisha ukajua kasoro zake,ikiwa ww ni mchanga kielimu,ndio maana nikasema,Tafuta Elimu na Soma ukweli

Twariqa uliyokuwa nayo ya Qaadiriyyah,wengine wetu tulikuwepo huko,kisha tukatoka kwasababu ya kusoma na kuujua ukweli
Bro
Allah akulipe kheri ya Dunia na Akhera
Tusome Dini yetu,Tufuate njia za Wema waliotangulia
Maimam Wanne
Abuu Hanifah
Maalik
Shaafiy
Hanbaly
رحمهم الله
Hakuna hata mmoja aliekuqa Sufi au kusisitiza mtu kusoma au kuwa Sufi,
Lau utafuatilia juu ya usahihi wa maandishi na ukweli wake,utajua hili
Shukran sana
Allah akubaarik
Unachonisihi nimelifuatilia kwa miaka ila nilichogundua ni kuwa kuna baadhi ya Waislam na Masheikh wenye kuitakidi hivyo pia wana wazungumzia Sufi pasipo kuwajua.

Hii inatokana na wao wenyewe kuwazungumzia kwenye baadhi ya vitabu vyao kisha wanajihitimishia kuwa Sufi wapo hivi: Kuwa Sufi ni grave worshippers (Waabudu Makaburi), Sufi ni washirikina n.k. Inafika pahala wana watuhumu na kuwatukana Sufi mpaka wanawatukana na Maimam ambao Sufi wanafuata mienenendo yao. Usimpe sikio pekee anayelalamikia kadhia fulani, mpe sikio na anayelalamikiwa kisha utajua uhakika wa mambo jinsi ulivyo.

Imam Ibn Hajar Al Asqalani kwenye Fat'h Al Baari 2nd volume na Sahihi chain kutoka kwa Imam Al Bayhaqi na Al Haakim na Ibn Khuzayma imepokewa kwamba: Bilal Ibn Al Haarith alikwenda kwenye kaburi la Mtume kipindi cha Aamu rramada Ukhalifa wa Umar na akisimama kwenye kaburi la Mtume akasema; " Yaa rasuulallah! Ardhi na mimea imenyauka, tafadhali tuombee kwa Mungu atunyeshelezee mvua kwa ummah wako"

Unaielewaje hii?

Imam Malik anasema: " Whoever studies tafaqaha and didn't study Sufism will be corrupted, and whoever studied Sufism and didn't study tafaqaha will became a heretic, and whoever combined both will be reach the truth. [The Scholar Ali Al Adawi volume.2 p 195]

Imam Ahmad Ibn Hambal: O My son, you have to sit with people of Sufism, because they are like a fountain of knowledge and they keep the remembrance of Allah in their hearts. They are the ascetics and have the most spiritual power [ Tanwir Al Quluub p. 405]

Imam Shafii kawazungumzia pia kwa wema mzuri watu wa Sufi na akasema amekaa kwao na amepata kujifunza dini kwao. ImamAbuu Hanifa kadhalika naye ni vivyo hivyo kuwa ni watu wema kwenye Ad Dur Al Mukhtar vol. 1 p. 43.

Unawazungumzia vipi hao Maimam kwa walichokisema ama kuwazungumzia Sufi?

Nimesoma Tawhiid ndugu, itikadi sahihi naijua. Kadri nilivyozidi kusoma ndivyo kadri nilivyozidi kujua na naandika kwa wema na siyo chuki. Wanaowapinga sufi wengi wao ni Salafi! Na salafi kielimu wamejifunga! Hawaamini wala hawamfuati Imam yoyote wa Sunnih wal Jamaa bali wanawafuata Maimam wenye Itikadi ya kwao. Ikiwa kama wakimfuata Imam wa Sunnih wal Jamaa basi wanachukua kipande kinachoendana na kile kinachokwenda sambamba na kile wanachokipigania wao. Ni watu waliyoivishwa itikadi ni watu wenye uchache wa elimu.

Kadri nilivyozid kutafuta ukweli nikakuta wana wa zuoni wakubwa wote wa Madhehebu ya Hambali walikuwa ni Sufi. Hambal Saudi Arabia wanajinasibu ni dhehebu lao lakini wanakataza Tasawwuf,Kutembelea makaburi n.k. Sikutanguliza itikadi. Nilitanguliza kuujua ukweli.

Ninasoma kwa Sheikh wa kisufi na nahudhuria hafla mbalimbali na hata siku moja sijawahi kushuhudia Sufi wakimuabudu mwengine zaidi ya Allah! Watu wanasema wanamuabudu Mtume sijawahi kuona hill! Watuwanasema wanawaabudu Mawalii sijawahi kuona hili! Watu wanasema wanaabudu makaburi sijawahi kuona hili! Na kuna mengine yanazungumzwa hata sijawahi kuyasikia zaidi ya kutoka kwa hao wanaowatuhumu.

Mimi ni Sunni, madhehebu ya Imam Shafii na nimeridhia kufuata twariqah ya Sheikh Abdul Qaadir Al Jaylaan.
 
Back
Top Bottom