Anaongoza kutokea Msoga.Kuna hatari fulani nimeanza kuiona, kuna maneno fulani nimeanza kuyasikia na kuna Mipango fulani ya kukomoana na kuhujumiana ndani kwa ndani nimeanza kuisikia pia.
Mimi sina uhakika kuwa kwa sasa Rais Samia ni TV Screen tu ila Rais Mstaafu Kikwete ndiye Remote Control kama watu wasemavyo, ila kama hili lina Ukweli basi kuna Hatari moja Kubwa ndani ya CCM na Serikali naiona inaenda kuja (kutokea)
Na wewe Rais Mstaafu Kikwete kama ni kweli una Ushawishi mkubwa katika Utawala huu wa Rais Samia tafadhali jishtukie upesi, kaa mbali nae na mwachie Mama nae atengeneze Legacy yake kwa huongelewi vyema na Watu wa Kanda ya Ziwa hasa baada ya Tukio Kubwa nchini la tarehe 17 Machi, 2021.
Kuna Taa Nyekundu ninaiona mahala!