Jana baada ya mihangaiko ya kutwa nzima, kabla ya kwenda geto niliamua kuvinjari mjini ambako nilipata "usafiri" wa kukodi. Baada ya kuukodi huu usafiri niliamua kwanza niende "Uvinza chumvini" kisha nikitoka huko kama muda utaruhusu basi nitembelee na "makundu-chi" zenji. Basi wana mmu, nilianza safari ya kuelekea uvinza, kule kukaribia tu nilikutana na harufu mchanganyiko za ajabu sana. Nyingine za vitunguu swaumu, malimau, vitunguu maji, pilipili, tangawizi n.k. Kwa kweli nilipata kichefu chefu cha ajabu na asubuhi ya leo nimeamka nikiwa na mafua makali sana. Baada ya kuona usafi wa "uvinza" hauridhishi, niliahirisha safari ya "makunduchi" na ikabidi nilipe gharama za kukodi usafiri na nirejee geto haraka iwezekanavyo. Nawaasa vijana wenzangu wanaopendelea kutembelea uvinza kwamba wakati huu wa joto kali wapunguze safari za huko maana hapako shwari, vinginevyo wataishi kupata vipindupindu.