Masikini watoto wa ccm wanasukumizwa kuandika mambo ambayo yako juu ya umri wao, dah! Wanapaswa kuelewa kwamba mtu hawi mkosefu milele. Kama alikosea na amekiri kwamba aliwajibika kuinusuru serikali nzima na sio kumaanisha kuwa anakubali kuwa mwizi, unataka nini zaidi? Huyo baba yenu amepona hadi leo kwa sababu Lowasa alimkinga. Ukikaa na watu wazima kijana, kama mkubwa kwako ameharibu hewa unatakiwa wewe mdogo uombe radhi kwa kuharibu hewa na unaondoka kwa adabu ili kumnusuru mkubwa kwako aliyeharibu hewa asiaibishwe. Wenzenu tulifundwa hivyo wakati wa udogo wetu. Sasa poleni sana siku hizi watoto hamna muda wa kufundwa na wakubwa wenu maana mko busy na waya masikioni, whatsapp, telegram, viber, BBM na kadhalika. Hata wazee wenu wako busy kukusanya fedha ya wizi na kupora viwanja vya wanyonge ingawa hawaviendelezi. Ni ajali mbaya kwenu.
Kule kuambiwa Lowasa ni fisadi zamani zile ni sahihi, lakini ametubu na kuokoka lakini ujeuri wa baba zenu hawakutaka awe salama, walichukuwa nafasi ya Mungu kutomsamehe, ni kwa sababu wanajua mlokole huyu wa kisiasa akaona aende kwao walioelewa uzito wa toba yake maana ndio waliomwona na aliwaudhi sana. Wamemrudisha kundini. Ubaya uko wapi hapo? Binadamu usilipize kisasi kwa mwenzio, mwachie Mungu maana wewe huna haki ya kulipiza kisasi ila Mungu. Naye Mungu sio binadamu, anasamehe wote wamrejeaye kwa toba. Ukichukuwa nafasi ya Mungu anakukong'oli tu, unakufa na chuki zako. Lowasa huenda kaongea na Mungu wake naye kasamehewa, wewe ni nani ukamzuia riziki aliyopewa na Mungu wake (kama amepewa)??? Chuki mbaya vijana huenda msielewe leo lakini mkikua mtaelewa tu.