UVCCM yamvaa Lowassa, wasema watamnyosha

UVCCM yamvaa Lowassa, wasema watamnyosha

Mnaweka fisadi ikulu akishaanza kufanya vitu vyake mnaanza kulia lia kama watoto wadogo. Mtu alijiuzuru kwa ufisadi na tangia hapo hajawahi toa utetez wowote wa maana kujitetea lakin midanganyika ina mwona shujaa. Kha!
 
Najaribu kutazama jinsi kenyata na ruto walivyoandamwa na kashfa kibao za matukio ya mauaji ya mwaka 2007

baadae namuangalia kenyata na kashfa yake na baba yake kwa kuwanyang'anya wakenya wengi ardhi huko kikuyu highland lakini sasa ndiye raisi

pamoja na kuwa na kashfa kibao namuona kama rais pekee aliyeipeleka puta kenya katika maendeleo zaidi ya marais wote waliotangulia huku uchumi wao ukikua maradufu

kwa mantiki ndogo kama hiyo niko radhi lowasa aingie madarakani hata kama ni fisadi ili

1) kuondoa utawala wa ccm madarakani na kisiwepo chama kinachoamini kuwa kitatawala milele kama ccm wanavyodhani

2) kubadilisha uongozi wa nchi utaifanya hata ukawa itakayoingia madarakani itende mambo kwa umakini huku ikijua baada ya miaka mitano inaweza ondolewa madarakani


nb: Nataka asiwepo mtawala wa milele kama ccm na Lizaibon wanavyoamini kuwa wao hawawezi kuanguka na hilo litafanya kila atakayepewa madaraka kufanya mambo kwa uhakika huku akijua akilegalega miaka mitano inayofata ataondolewa


kura yangu ni ukawa




kalichumbage
 
Ukimtaja lowasa kuwa ni fisadi ujue yeye alikuwa ni cha mtoto wenye ufisadi wamo ndani ya nyumba (CCM). Bado majambazi hawa wanatutawala ee Mola waangamize maficcm
Hii kitu inaitwa ufisadi kama ndio sera ya CHADEMA basi hawafai kuongoza nchi hii. Mnatakiwa kabla ya kuiunga mkono CHADEMA mjue itatatua vipi matatizo ya watanzania. UFISADI siyo kitu ya CCM tu ni kitu watanzania wote tunayo. Hawa mafisadi wakubwa wapo kwa sababu tu wamepata nafasi ya kufanya ufisadi mkubwa. Lakini amin amini nawaambia watanzania wengi ikiwepo nyie mnaopiga makelele fisadifisadi ni vifisadi vidogovidogo. Unamwajiri Mtanzania dukani kwako ukimwacha mwezi hujamkagua tu ukija kupiga hesabu amekuliza. Unaenda dukani kwa Kanjubai kununua vitu mfanyakazi anakwambia bosi hii kitu nitakuletea kwako nipe namba ya simu nikutuletee nitakuuzia kwa nusu ya bei, tayari Kanjubai kalizwa. Unakwenda bandarini kodi unajua kabisa ni 5m mtu anakwambia nipe 1.5m nikufanyie kodi yote 3m; watanzania hawahawa tena wengine ni CHADEMA wakeleketwa kabisa na wengine CCM wakeleketwa kabisa tatizo ni watu sio CCM. Unaenda dukani kununua kitu muuzaji anakuambia unataka risit au nikupe risiti ya kutembea na mzigo, ukikubali tayari wote mmefanya ufisadi. Mkipewa dili ya mabilioni mtafanya kama hao manaowalalamikia tu. Mtu anakuja kukuuzia gold ukienda kuuza unaambiwa gold fake wote huu ni ufisadi na unafanywa na watanzania wa vyama vyote. Sijui kama wafanyakazi wote wa serikali, mashirika na binafsi ni wanaCCM kuna makesi mengimengi ya wizi wa mali za umma na za binafsi unaofanywa na wafanyakazi wa serikali na wa kampuni binafsi ambao wengine ndio nyie wengi mnaopiga kelele za fisadifisadi. CHADEMA wamekuwa wapokea misaada mingi toka kwa vyama rafiki na pia ruzuku hamjiulizi kwa nini mpaka leo hata ofisi ya hadhi wameshindwa kuwa nayo. Ukichunguza utakuta fedha ya ujenzi wa jengo kubwa lenye hadhi ya CHADEMA imetolewa lakini imechakachuliwa huu wote ni ufisadi na hauko CCM. Ugomvi wa kina zito na CHADEMA halafu baadae na CCM ulitokana na kuhoji kwa nini akaunti zao zisikaguliwe na mkaguzi mkuu wa serikali wote waliogopa kwa sababu kuna viufisadi. Kwa hiyo suala la viufisadi limo miongoni mwa watanzania wote na sio upande mmoja yaani CCM kama wanasiasa wanavyojaribu kuingia ndani ya vichwa vyenu. Sikatai kuwa kuna wanacCCM ni mafisadi lakini msikatae pia kuna wanaCHADEMA ni mafisadi. Hawajapata chance to ya kufanya ufisadi mkubwa kwa kuwa hawako kwenye utawala. Watupe mkakatu mahsusi watapambanaje na ufisadi wa watanzania na sio wa CCM. Maana ukiondoa wa wanaCCM tu bado tatizo halitaisha wataibuka wa CHADEMA. Hii kitu mtu anaoneshwa 10billion anavunja katiba ya chama chake na kuvunja mtazamo wa chama chake ni dalili tosha akiingia kwenye raslimali atazishughulikia tu. Najua kuna watu wana hasira na CCM kwa sababu mbalimbali. Yeyote anayekuwa madarakani lazima ataonekana mbaya na baadhi ya watu na mzuri na watu wengine. Tujaribu kutafuta mtu anayeweza kupata suluhu ya hayo matatizo na sio kukimbilia ufisadi ufisadi. Kwa sehemu kubwa sera za CHADEMA zimechotwa kutoka CCM na hata vitabia vingi vya CCM CHADEMA amevichota na hata hotuba za waasisi wa CCM ndio CHADEMA anazitumia ikiwepo kumpokea mgombea wake wa urais wa sasa. Hivyo tegemea "mvinyo wa zamani kwenye chupa mpya" Chupa zikiwa ni CHADEMA na CCM. Mimi nadhani badala ya kuifanya siasa kama yanga na simba tutambue siasa ni kitu kinachogusa maisha. Wanasiasa wanatafuta zaidi ulaji wao na familia zao. Kwa kuwa sioni jipya kwa CHADEMA bado nadhani CCM iendelee kupewa dola huku tukitafuta Chama kitakachojipambanua kutatua matatizo ya watu kuliko inavyofanya CCM. Chama cha kuirithi CCM na kuleta mabadiliko kwa sasa sikioni; labda kama anatolewa tu kwa chuki binafsi. UKAWA imebeba vyama vyote vya upinzania na kuviingiza shimoni. Haya mwanzilishi wa UKAWA huyoooo. Mnabaki kutafuta sentesi za kuperemba; ukweli hiyo kitu si sawa. Ila iko siku wale wazuri kutoka CCM, CHADEMA na vingine vidogodogo wataungana na kuleta chama cha kuibadili CCM kama haitarekebisha baadhi ya mapungufu yanayolalamikiwa na wananchi.
 
Tumemsikia yule mbutwa alietolewa nje na Dr.Shein kwa kukosa heshima ndani ya mkutano wa CCM akibwabwaja na kutoa vitisho kuwa vijana wa CCM wapo tayari kuilinda CCM na utawala wake kwa bei yeyote ile ,nawa ndio lile kundi lisemalo halitoi madaraka kwa kutumia vikaratasi ,wanaichomekea falsafa hiyo katika mkmbo mmoja na Tanganyika ,hao ni vijana wa CCM.

Ela huku Tanzania Bara hakuna vijana wa Ukawa Pemba najua wapo na vijana wa CCM hawathubutu hata kwenda huko kwani Pemba ni maarufu.

Vijana wa UKAWA kutumia majukwaa ya siasa ni lazima mutumie muda mwingi kujibu na kuwajibu wachovu hawa wanaotegemea vyombo vya dola kwamba mara hii wazee wataekwa pembeni na dalili mmeshaziona katika chaguzi ndogo ,huu si wakati wa kuwanyamazia hawa wanaojiita vijana wa CCM ,mwaka huu CCM imekata tawi walilolikalia ni lazima waanguke.
 
Kijana wa UKAWA 1anapiga vijana wa ccm 

Unajua Seif Sharif Hamad aka Maalim Seif ameshamkata ng;ombe kamba ya pua aka ujamu ,sasa ni vijana kujihami popote pale hao wanaokiita vijana wa CCM wakitokeza pua basi liwalo na liwe ,ila haya sio kwa sasa kunasubiriwa kashkash za mikutano zianze ,yaani jamaa wanakisasi kibaya na wanaojiita vijana wa CCM ,haswa wale wanaokaa barabarani kusubiri wanaorudi kwenye mikutano ,safari hii mtazisikia habari rediona ,wacha wao wajipange na upande wapili wajitayarishe ,lazima miccm itakubali kama samaki haishi nchi kavu.
 
Unajua Seif Sharif Hamad aka Maalim Seif ameshamkata ng;ombe kamba ya pua aka ujamu ,sasa ni vijana kujihami popote pale hao wanaokiita vijana wa CCM wakitokeza pua basi liwalo na liwe ,ila haya sio kwa sasa kunasubiriwa kashkash za mikutano zianze ,yaani jamaa wanakisasi kibaya na wanaojiita vijana wa CCM ,haswa wale wanaokaa barabarani kusubiri wanaorudi kwenye mikutano ,safari hii mtazisikia habari rediona ,wacha wao wajipange na upande wapili wajitayarishe ,lazima miccm itakubali kama samaki haishi nchi kavu.

Tuombe Mungu Mh Lowassa achukue nchi kwa amani, maana hawa ccm wakishindwa hawatakubali.
 
shaka hamdu shaka alikua mfanyakazi wa ndani wa Shadia karume, hilo ni bwabwa 100%
 
NImependa apo anapotaja waliohama chama na CCM ikawa inasonga mbele.
Ni namna fulani ya kujipa moyo big up
 
Tuliiiieni kimyaaaaaa kura zitaongea mengi ya nini maccm hili mccm lakungoaaaaseeee
 
Back
Top Bottom