Diehard
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 472
- 361
FMES,
Nikuombe jaribu kuficha hasira zako kwa Lowassa. Haki na Uhuru wa mimi kumuunga mkono LOWASSA akitangaza NIA, na KUTEULIWA na chama changu ni haki yangu ya Kikatiba kama ilivyokuwa haki yako mwaka 2005 kumuunga mkono Mzee Malecela.
Nikuombe uheshimu haki yangu ya kutoa maoni yangu kama wewe ulivyotoa maoni yako ukitaka wagombea wajitokeze..
Leo mimi nimejitokeza openly na kusema ninachokiamini sijaongelea suala la whether Lowassa ana tuhuma ama hapana, tukianza kufukua tuhuma hata mzee wako ana tuhuma za kupokea fedha za EPA kupitia Jeetu Patel lakini hakuna aliekutuhumu kwa wewe kumuunga Mkono 2005 na pale Morogoro zilipoporwa na wezi wakati mama Anne Malecela akizileta kugawia wapiga kura.
Leo hapa nimesema ninachokiamin, come out sema kama Lowassa hana sifa niliyotaja then utakuwa na hoja ukinipa sababu za yeye kutokuwa na uwezo wa kuchapa kazi na ukajenga hoja nitakuelewa.
Tusipige porojo eti Lowassa alimfata Rais na kubembeleza, go and ask Mr. Malecela and he will give u the facts ambazo wengi hawapendi kusikia. Kama Lowassa anahusika na Richmond apelekwe mahakamani, hakuna anayemtetea na wala hilo halina mjadala; mahakama itaamua, kama Lowassa ni mwizi basi ni udhaifu wa mamlaka kutowakamata wezi na kuwapeleka mahakamani. Kama una ushahidi peleka katika authority uje hapa utueleze umepeleka ushahidi wa wizi wa Lowassa na hata mimi nitakuona hero! Tujadili facts mkuu, tusiingilie uhuru wa mtu kuchagua. Nimesema wazi kama chama kitamteua nitampigia kura na nimetoa sababu yangu, na si Lowassa pekee, same applies kwa CDM, wakisimamisha mgombea hawezi kuwa mkamilifu wa kila kitu lakini kila mmoja atahakikisha anampigia kura.
FMES na Wana JF,
Tusipoteze muda mwingi kujadili LOWASSA, huyu kama ana madhambi yake mamlaka husika zitachukua hatua zinazostahili. Nchi yetu ina bahati mbaya tumekumbwa na ugonjwa wa unaoitwa LOWASSA, tujadili issues za maendeleo.
Nikutoe shaka juu ya jambo moja: Ssina historia ya kuficha wala kutafuna maneno katika jambo ninaloliamini, kama wewe ulifanya kazi ya kutafuta ushahidi juu ya mkataba mbovu wa Richmond, nikupe hongera ulitekeleza wajibu wako kama RAIA mwema. Kama utaongelea UADILIFU, wewe mwenyewe ni zao la UKOSEFU wa UADILIFU wa Viongozi wetu. Suala la RICHMOND ni udhaifu wa mfumo wetu, jambo ambalo mpaka leo linatugharimu kama Taifa. Tumelalamika, tumetuhumu, tumekosoa lakini hatujajadili ufumbuzi wa tatizo lililoleta RICHMOND. Leo ni mwaka wa sita bado tatizo lipo lakini bado tunajadili RICHMOND na LOWASSA.
FMES, don't fool people here, tunafahamu why unakuwa na hasira when it comes to LOWASSA. Ni tatizo la familia yenu na ni makovu ya 2005. Nimalize kwa kusema LOWASSA akiteuliwa na kupitishwa na chama nitamuunga mkono asipoteuliwa na asipopitishwa na chama pia nitaheshimu na kufanya maamuzi kutokana na wakati na mazingira ya wakati huo, hiyo ni imani yangu. Mimi nimesema msimamo wangu na kwa jina langu, wewe come out and sema msimamo wako. Kila mmoja wetu atakuwa na maamuzi yake tuyaheshimu, akini kwa sasa tujadili masuala ya NCHI yetu na tutimize wajibu wetu. Wewe binafsi huna moral authority kuongelea uadilifu bcs your background inaonyesha, lakini hatukuangalii kwa Background yako tunakuangalia wewe na unachosema kwa sasa.
Hussein
Like father like son
Nakumbuka Lowassa wakati anaachia uwaziri mkuu alijaribu kusema kwamba mjengoni ni wengi ila wanamtosa akijaribu kupata huruma ya wabunge na wananchi kwamba wengi ni wachafu yeye asitolewe kama mbuzi wa kafara.
Hapa Bashe naye kaja na gia ya kuonyesha uchafu wa Lowassa na kulinganisha na wa Malecela kila mmoja tutamsema kwa wakati wake ila hilo ulisemalo la wewe kumsupport Lowassa wala halina tatizo katiba inakuruhusu lakini sisi wananchi tunaamini ampendae na kumsupport jambazi ni JAMBAZI.