William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,464
-Katika hili tafsiri ya nani kalala na nani kaamka ni subjective inawezekana wewe ukawa na usingizi mzito wakati ukihisi umeamka,hotuba yangu inawezekana usiipende sana lakini hayo ni mawazo yangu ambayo wewe pia unayako ,haki uliyonayo wewe kuyapinga yangu,ni haki hiyo hiyo niliyonayo mimi kukataa mawazo yako,si lazima tufikiri sawa,tuamue sawa,ikitokea hivo wote tutakuwa na matatizo,na si lazima hapa katika forum tukawa wote na mtazamo unaofanana,na si lazima ukalazimisha nione unachoona na mm silazima nikakulazimisha ukaona ninachoona.
Nilisema tuufunge mjadala huu hapa kwani muda wa mjadala juu ya swala hili si sasa na tusipoteze nguvu nyingi sasa kujadili haya mambo,2014 tutakutana jamvini kujadili nani anafaa kuwa Rais wa Nchi yetu regadless anatoka wapi,sasa tutumie muda kujadili BEI MCHELE,BEI SEMBE,AJIRA,STABILITY YA UCHUMI WETU,UMOJA WA KITAIFA,KUPANDA KWA GHARAMA ZA MAISHA,NAULI ZA DALA DALA ZINONGEZEKA WAKATI VIPATO VYETU BADO DUNI,BEI ZA MAFUTA,TATIZO LA UMEME(Wewe hili hulifahamu bcs utotoni ulikaa upanga,unatumia jenereta,na sasa ukirudi likizo unatumia jenereta nyumbani na huko ulipo hamna mgao wa 16hrs) na kwa sisi wana CCM namna gani tunakisaidia chama kutekeleza majukumu yake kupitia serekali ili kuleta TIJA katika maisha ya watanzania ,haya ya lowasa na wengine si ya tija kwa sasa.Matatizo yetu hapa nyumbani ni ya msingi sana kuliko kujadili hayo unayotaka sasa tuyajidili.
Mwisho inawezekana ulitarajia nifikiri kama wewe ambae umekulia ndani ya mfumo huu,ume enjoy matunda na sasa upo nje ya nchi ukiwa hujui bughudha za daladala,hujui tatizo la mgao ulitaka niimbe ngonjera zako, nimalize kwa kusema tena Turudi katika msingi wa mjadala wangu,nilichosema ninakiamini,nitakisimamia sitabadili msimamoa katika hilo unless kuwe na Tangible Facts juu ya yale uliosema,Kuhusu kuandikiwa hotuba ni vizuri umesema hunifahamu kwahiyo kama walivosema wahenga USILOLIJUA NI USIKU WA GIZA,so nivizuri ukapata muda kidogo kunifahamu na hilo utaweza tu kama utajipa muda kunifahamu.
- Well, siwezi kuwa kwenye usingizi wa aina yoyote, I mean how can kiongozi wa taifa wa stature yako akaja hapa JF kumlilia mwananchi kama mimi aliyelala usingizi, huoni kwamba wananchi walio macho watashindwa kubaini kati yangu na wewe nani yuko usingizini? ha! ha! ha! ha!
- Ni kweli kabisa kama mwanachi nina haki ya kukuuliza wewe kiongozi uliyefukuzwa mara mbili, Moral Authority ya kutoa hotuba za kuelimisha wanachama wa chama kilichokufukuza uongozini mwake umeitoa wapi? Waannchi wengi wamekuuliza maswali humu mbona huwajibu, ila umenikomalia mimi mwananchi niliyelala usingizi? ha! ha! ha! ha! ha! ha! Unajua una hoja zinachekesha sana! ambazo ninaweza kuzijibu bila hata kufikiri sana!
- Tuufunge mjadala maana sasa unakugusa pabaya sana, hapana hapa tunaelimishana na kuelimisha taifa, waannchi wanajionea ni kwa nini hili taifa limedumaa ni kwa sababu ya kuwahi kuongozwa na watu kama wewe, unayeamini kwamba wananchi wana shida ya umeme, lakini wewe utampigia kura Lowassa aliyewaletea hilo hilo tatizo la umeme, Bashe watu kama nyinyi ondokeni huko kwenye siasa za taifa maana wewe na hao MAPACHA WATATU tayari Mmeshindwa, waachieni wengine sasa, I mean mimi hata nikiwa anything sio kiongozi na wala sikutoa hotuba anywhere na kuwadanganya wananchi kwa maneno ambayo mimi mwenyewe nikiwa kiongozi nimsehindwa kuyatimiza,
- Bashe mimi ni mwananchi ni haki yangu kukuuliza maswali ya msingi reardless of who is my father au mother, tizama kwenye hoja zangu ni wapi nimeuulizia kuhusu baba yako au mama yako, wewe hoja ya kwanza Mama Kilango, Malecela! badala ya kusimamia hoja zako mwenyewe ulizozitoa kwenye UV-CCM na kuwalipa media wa kupambe, sasa ukaona na huku JF nako unaweza kupambwa hapa hatupambi mtu, umetoa hotuba umeileta hapa sasa simama hapa ujibu maswali waliyoshindwa kukuuliza kule UV-CCM kwa sababu ya kuwaogopa wanaokutuma MAPACHA WATATU,
- Bashe siasa za kisasa ni hoja, sio manguvu na hasira, mimi sio kiongozi mwenzio wewe ndio mwenye burden of the proof ya kuonyesha kwamba una uwezo wa uongozi, nilitegemea utaonyesha uwezo wako wa kuongoza mpaka wananchi tuamini kwamba ulionewa kwenye kufukuzwa, lakini kwa haya yote uliyoyasema hapa kwenye hii thread, naomba nikwambie kwamba huna uwezo wa kuongoza wala kutafuta maoni ya aina yoyote kwa taifa, na ndio maana hili taifa tumekwama sana, I mean kiongozi wa stature yako anashindwa kujibu hoja za hotuba yake mwenyewe, badala yake unanijibu mwananchi kama mimi ninayekuuliza ishus za baba, mama na location yangu? Damn maan!
Ahsante Sana Mheshimiwa na Mungu Aibariki JF, maana huko kote umesfiwa sana sasa hapa tunakuomba ubebe msalaba wako unalilia baba na mama zetu wananchi na location zetu, kweli hili taifa sijui tulilogwa na nani, I mean can you imagine Trump anamuuliza Obama cheti cha kuzaliwa, halafu Obama anaaanza kumjibu kwamba wewe umezaliwa kwenye utajiri hujui lolote kuhusu umasikini? ha! ha! ha! ha! ha! ha!, Only in Tanzania!
William @ NYC, USA.