Most of ur posts defines a whine that u r!! When u start a thread also show subjectively why he is doubtful, we don't give a toss wether Bashe, Rostam,kikwete, Slaa paid for his education..its his ability as a leader that will get him the coveted post, now get tht in u and work on it
Most of ur posts defines a whine that u r!! When u start a thread also show subjectively why he is doubtful, we don't give a toss wether Bashe, Rostam,kikwete, Slaa paid for his education..its his ability as a leader that will get him the coveted post, now get tht in u and work on it
Yaani post zake hazieleweki kabisa!!! Sijui ana haraka au ndio wale wale???
nashukuru kumkubali kwenu bashe bt mjue anauwezo wakuwashinda wabunge 6 wa cdm kwa hoja kwenye mjadala,kubalin na hilo.
Suala sijui bashe katumwa anamuongelea nani hili si la msingi, la muhimu ni Ujumbe aliousema una mashiko si mchezo. Saa nyingine hata vichaa na wendawazimu huongea ukweli judge the message not the messenger
Ndg yangu Lampard acha Upotoshaji,
Nikujibu kwa Ufupi:
Sikweli kuwa nina mdogo wangu aneitwa IBRAHIM anaesoma UDOM, mdogo wangu Ibrahim amemaliza Mzumbe na sasa yupo Mtaani akitafuta ajira kama Vijana wengine wa Kitanzania.
Hoja ya kwamba nina jeraha, ama kinyongo, ama chuki nayo ni Upotoshaji. Sina kinyongo that's why nilirudi Jimboni kumsaidia aliyeteuliwa ili chama changu kishinde, this tells a lot. Nadhani waliokupa taarifa hizi wamekupotosha. Lakini haina maana nimesahau yaliyotokea na wala sipo hapa kujadili uhalali wa hoja iliyotumika kutoniteua, bali nikuthibitishie sina kinyongo lakini siwezi kusahau kama ambavyo sijasahau matukio. Ya 2007, Kizota pale jina na kura nilojipigia zilipopotea kimuujiza. Sitasahau ya 2005 Nzega ktk kura za maoni na mimi kuwa Mshindi wa Tatu, sitasahau ya 2008 Dodoma, yote haya yamekua sehemu ya Historia yangu hayatafutika lakini sina kinyongo.
2010 nilimsaidia mbunge wangu kwani niliamini si yeye wala Chama (taasisi) walionikosea that's why mimi na team yangu ilimsaidia Kigwangalla.
Hoja yako kuwa ninamuandaa SALUM ALLY ni hoja potofu, 2015 kama nilivowahi kusema nitarudi kugombea Jimbo la Nzega na hivi sasa naendelea kutekeleza ahadi nilizotoa 2010 kwani wana Nzega walinipa kura 14,420 kati ya kura 19,000 zilizopigwa.
Hoja yako ya kuwa mimi nina kundi: Hakuna mwanasiasa asiyekuwa na kundi lake, msingi wa hoja yangu ni kwamba siasa 2015 zinakiumiza chama kwani sasa kuanza mikakati hiyo ni kudhoofisha chama wajibu wangu na wewe na wana CCM wote ni kumsaidia Rais Kikwete kutekeleza Majukumu yake KUFIKIA MATARAJIO ya WATANZANIA; bila ya hivo 2015 CCM haitakuwa na uhalali wa kuchaguliwa, ni wendawazimu kuanza kampeni leo wakati hata nusu ya tearm ya Pili ya Kikwete haijafika. Nikushauri acha mawazo mgando hayo.
Hoja yako kuwa namuunga Mkono Lowassa na Nchimbi kwa URAIS nayo ni upotoshaji. Hawa watu hawajatangaza labda wamekuambia wewe mimi sina taarifa. Ila kama Lowassa atasema anagombea sitasita kumuunga mkono kwani ninaamini katika uwezo wake wa kusimamia na kufanya kazi hilo sina mashaka nalo (ni msimamo wangu binafsi ambao unaweza kuendelea kubaki hivi ama kubadilika kulingana na wakati husika), kama chama kitamteua nitamuunga mkono bila shaka. Lakini sasa sina taarifa hizo.
Hoja ya Jamal nayo ni upotoshaji. Si kweli unalosema, na usimzushie ili aonekane ameanza kampeni mumkate, na mtu anapokuwa na Uwezo ni vizuri mkakubali. Uwezo wa Jamal hauna mashaka, kama chama kitamteua atahukumiwa na wapiga Kura na mimi nitakayemuunga mkono muda ukifika utamjua kwani sina sifa ya Kujificha katika Msimamo wangu.
Ndg yangu,
Hoja yako juu ya umri nikutoe shaka; Mimi ninaheshimu kanuni na taratibu, sina uroho wa madaraka, Kamati yangu haijapewa ktk Hadidu rejea zake hatuna suala 'Umri' kwa hiyo usiwe unahukumu bila Facts.
Pia ninapoongelea hoja ya Urais 2015 ninamaanisha kwamba wana CCM tufanye siasa 'above Group Politics' kwa Maslahi ya Chama Chetu na taifa. Linapokuja suala la nchi ni muhimu kufanya kazi 'Above Party Politics', hii itaisaidia nchi yetu. Nikushauri usipende kuwa kasuku, ongea kitu ambacho unakijua na una Facts zake. Ni rahisi kujua UJINGA wa mtu kupitia maandishi, kwahiyo wanpokupa cha kuongea fanya uchunguzi.
Lampard, nimeona kauli yako unasema kundi letu mtalimaliza; maana yake wewe una kundi unalolinda. Usionyeshe 'ujinga' wako kirahisi hivi. Nchi hii imeumizwa na 'Cheap Politics' ni Vizuri ukaanza kufikiri above Group Politics na Party Politics. Fanya uchunguzi kuwa na Facts kabla hujaongea.
Ndg yangu Lampard,
Nikuombe usiwe miongoni mwa wanaoumiza nchi kwa kufanya siasa ambazo ni 'Based On Speculations'.
Leo nchi yetu imeumia sana kwa aina hii ya siasa, CCM kimekuwa chama ambacho kinaumizwa sana na siasa hizi za Uzushi na Uongo.
Nilivyokusoma unaonyesha wewe ni Mwana CCM mwenye kundi ndani ya CCM. Nikushauri usikubali kila unachoaminishwa. Jifunze kuwa tabia ya kuhoji, why, how, when, which, what... Hii itakusaidia kusimamia unachoamini kwa Hoja.
Nimeona ukijisifia usomi wako wa Siasa; Nikiri inawezekana ni msomi wa siasa, basi anza kuwa 'Mwana Tafakuri' ili usomi wako uwe na Tija. Usikubali kuugua ugonjwa wa kugawanyika kwani ukianza kauli hizi KUNDI LENU na KUNDI LAO na KUNDI LETU, kesho utaingia katika kansa ya Kugawanyika ambayo hutumiwa na wana siasa MUFLISI ambao hujadili na kutazama mambo kwa Msingi wa Ukabila, Dini, Ukanda n.k. Tutaua nchi na chama chetu, waambie walokupa taarifa Next time wakupe Taarifa za kweli.
Mwisho nikuhakikishie: Sina Kinyongo, Sina Hasira bali sijasahau, Nzega 2015 sina ninayemuandaa Nzega bali nitarudi kugombea mwenyewe.
Kila la kheri Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika.
Duuu mkuu wewe unatisha! yaani nimekukubari,kwanza unajua kujenga hoja kwa kuipangilia,pili yaonyesha mkichwa wako umejaa busara na hekima.....Jamani makachero wa CDM mko wapi? huyu Bashe hastahili kuwa ccm hata kidogo!. Hebu mtafuteni huyu kijana na kisha mkaenae kwa marefu na mapana. Lakini huu ni mtizamo wangu tuNdg yangu Lampard acha Upotoshaji,
Nikujibu kwa Ufupi:
Sikweli kuwa nina mdogo wangu aneitwa IBRAHIM anaesoma UDOM, mdogo wangu Ibrahim amemaliza Mzumbe na sasa yupo Mtaani akitafuta ajira kama Vijana wengine wa Kitanzania.
Hoja ya kwamba nina jeraha, ama kinyongo, ama chuki nayo ni Upotoshaji. Sina kinyongo that's why nilirudi Jimboni kumsaidia aliyeteuliwa ili chama changu kishinde, this tells a lot. Nadhani waliokupa taarifa hizi wamekupotosha. Lakini haina maana nimesahau yaliyotokea na wala sipo hapa kujadili uhalali wa hoja iliyotumika kutoniteua, bali nikuthibitishie sina kinyongo lakini siwezi kusahau kama ambavyo sijasahau matukio. Ya 2007, Kizota pale jina na kura nilojipigia zilipopotea kimuujiza. Sitasahau ya 2005 Nzega ktk kura za maoni na mimi kuwa Mshindi wa Tatu, sitasahau ya 2008 Dodoma, yote haya yamekua sehemu ya Historia yangu hayatafutika lakini sina kinyongo.
2010 nilimsaidia mbunge wangu kwani niliamini si yeye wala Chama (taasisi) walionikosea that's why mimi na team yangu ilimsaidia Kigwangalla.
Hoja yako kuwa ninamuandaa SALUM ALLY ni hoja potofu, 2015 kama nilivowahi kusema nitarudi kugombea Jimbo la Nzega na hivi sasa naendelea kutekeleza ahadi nilizotoa 2010 kwani wana Nzega walinipa kura 14,420 kati ya kura 19,000 zilizopigwa.
Hoja yako ya kuwa mimi nina kundi: Hakuna mwanasiasa asiyekuwa na kundi lake, msingi wa hoja yangu ni kwamba siasa 2015 zinakiumiza chama kwani sasa kuanza mikakati hiyo ni kudhoofisha chama wajibu wangu na wewe na wana CCM wote ni kumsaidia Rais Kikwete kutekeleza Majukumu yake KUFIKIA MATARAJIO ya WATANZANIA; bila ya hivo 2015 CCM haitakuwa na uhalali wa kuchaguliwa, ni wendawazimu kuanza kampeni leo wakati hata nusu ya tearm ya Pili ya Kikwete haijafika. Nikushauri acha mawazo mgando hayo.
Hoja yako kuwa namuunga Mkono Lowassa na Nchimbi kwa URAIS nayo ni upotoshaji. Hawa watu hawajatangaza labda wamekuambia wewe mimi sina taarifa. Ila kama Lowassa atasema anagombea sitasita kumuunga mkono kwani ninaamini katika uwezo wake wa kusimamia na kufanya kazi hilo sina mashaka nalo (ni msimamo wangu binafsi ambao unaweza kuendelea kubaki hivi ama kubadilika kulingana na wakati husika), kama chama kitamteua nitamuunga mkono bila shaka. Lakini sasa sina taarifa hizo.
Hoja ya Jamal nayo ni upotoshaji. Si kweli unalosema, na usimzushie ili aonekane ameanza kampeni mumkate, na mtu anapokuwa na Uwezo ni vizuri mkakubali. Uwezo wa Jamal hauna mashaka, kama chama kitamteua atahukumiwa na wapiga Kura na mimi nitakayemuunga mkono muda ukifika utamjua kwani sina sifa ya Kujificha katika Msimamo wangu.
Ndg yangu,
Hoja yako juu ya umri nikutoe shaka; Mimi ninaheshimu kanuni na taratibu, sina uroho wa madaraka, Kamati yangu haijapewa ktk Hadidu rejea zake hatuna suala 'Umri' kwa hiyo usiwe unahukumu bila Facts.
Pia ninapoongelea hoja ya Urais 2015 ninamaanisha kwamba wana CCM tufanye siasa 'above Group Politics' kwa Maslahi ya Chama Chetu na taifa. Linapokuja suala la nchi ni muhimu kufanya kazi 'Above Party Politics', hii itaisaidia nchi yetu. Nikushauri usipende kuwa kasuku, ongea kitu ambacho unakijua na una Facts zake. Ni rahisi kujua UJINGA wa mtu kupitia maandishi, kwahiyo wanpokupa cha kuongea fanya uchunguzi.
Lampard, nimeona kauli yako unasema kundi letu mtalimaliza; maana yake wewe una kundi unalolinda. Usionyeshe 'ujinga' wako kirahisi hivi. Nchi hii imeumizwa na 'Cheap Politics' ni Vizuri ukaanza kufikiri above Group Politics na Party Politics. Fanya uchunguzi kuwa na Facts kabla hujaongea.
Ndg yangu Lampard,
Nikuombe usiwe miongoni mwa wanaoumiza nchi kwa kufanya siasa ambazo ni 'Based On Speculations'.
Leo nchi yetu imeumia sana kwa aina hii ya siasa, CCM kimekuwa chama ambacho kinaumizwa sana na siasa hizi za Uzushi na Uongo.
Nilivyokusoma unaonyesha wewe ni Mwana CCM mwenye kundi ndani ya CCM. Nikushauri usikubali kila unachoaminishwa. Jifunze kuwa tabia ya kuhoji, why, how, when, which, what... Hii itakusaidia kusimamia unachoamini kwa Hoja.
Nimeona ukijisifia usomi wako wa Siasa; Nikiri inawezekana ni msomi wa siasa, basi anza kuwa 'Mwana Tafakuri' ili usomi wako uwe na Tija. Usikubali kuugua ugonjwa wa kugawanyika kwani ukianza kauli hizi KUNDI LENU na KUNDI LAO na KUNDI LETU, kesho utaingia katika kansa ya Kugawanyika ambayo hutumiwa na wana siasa MUFLISI ambao hujadili na kutazama mambo kwa Msingi wa Ukabila, Dini, Ukanda n.k. Tutaua nchi na chama chetu, waambie walokupa taarifa Next time wakupe Taarifa za kweli.
Mwisho nikuhakikishie: Sina Kinyongo, Sina Hasira bali sijasahau, Nzega 2015 sina ninayemuandaa Nzega bali nitarudi kugombea mwenyewe.
Kila la kheri Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika.
Mr. Bashe, hotuba yako inaonesha kuwa unaweza kuwa mwandishi au mzungumzaji mzuri sana, na labda ndio maana umeweza kupata nafasi ulizopata ndani ya umoja wa vijana, na labda hata kupata ajira uliyonayo kwa ndugu Rostam. Wasi wasi wangu kwako ni kama una credibility ya kusema uliyosema. Mtu yoyote akiisoma habari hii bila kuangalia background ya mtoa hotuba ataona kuwa hii ni habari nzuri sana yenye mvuto mkubwa sana. Ila tu ukiangalia background ya ndugu Bashe unaona hotuba hii ina walakini:
Kwanza je ndugu Bashe ambaye ni mwajiriwa wa Rostam, anaweza kwa vyovyote vile kusema ukweli kuhusu ubaya wa bosi wake? Jibu utalipata kwenye hotuba hii kwamba ndugu Bashe hayuko tayari kwa hili. Ameongoea kuhusu watu wanaotuhumiwa, sidhani kwamba suala la Rostam na Dowans bado ni tuhuma. Ushahidi unaonyesha Rostam ndiye haswa muhusika mkuu wa Dowans, na hata mwakilishi mliyemleta alitamuka hilo. Hizi sio tuhuma huu ni ukweli kwamba Rostam, mwajiri wako, mwana CCM yuko ndani ya ufisadi wa Dowans, na kama kiongozi anatakiwa awajibike kwa hili kwa kurudisha nyuma heshima ya CCM na serikali ya CCM.
Pili, ukiisoma kwa undani hotuba hii imelenga kumushambulia ndugu Nape, ambaye ni kiongozi wa chama chako wewe. Umefanya ushambulizi huo kiujanja ujanja ili ionekane tuhuma za watu waliotuhumiwa kwa ufisadi ni sawa kabisa na tuhuma za wale wanaotuhumiwa kwa kuanzisha CCJ?, Ndugu Bashe, kumbuka kosa la ufisadi ni uhujumu wa uchumi na la uanzishaji wa CCJ ni upanuzi wa demokrasia nchini. Ushauri wangu ni kwamba mwacheni Nape afanye kazi yake ya kurudisha mvuto wa wananchi, ili waje wapimwe na kulaumiwa kwa hilo na usitumie kamati yako kuendeleza siasa za makundi ambazo zimeifikisha CCM hapa ilipo sasa hivi
Inafurahisha sana unavyotafasiri sababu zilizo potezea umaarufu CCM, wakati huo huo unaendeleza sababu hizo katika hotuba hii. Na kama hili ndilo utalifanya mikoa yote utakayo zunguka then tutastaajabu kama utakuja na kitu kipya cha kusaidia umoja wa vijana uliokuchagua.
Hussein Bashe, sina tatizo na asili yako kwakuwa nchi hii imekuwa ya hovyo chini ya CCM, imekuwa ya hovyo zaidi tangu aingie madarakani Kikwete ambapo wagiriki, wachina, wabelgini, wakomoro na wangazija wanachuma raslimali za walipakodi kama hawana akili nzuri, usomali wako haunipi shida kabisa we ukipata fursa ya kukamua chini ya CCM kamua mwanawane.
Pili sina tatizo na mbinu unazotumia kupata madaraka makubwa. Kama una wadogo zako vyuoni, misikitini na penginepo wewe endelea tu mradi azma yako iimie maana tangu mlipolivunja azimio la Arusha kila mtu anatumia mbinu anazozijua yeye kupata ulaji.
Lipo jambo moja ambalo unalazimika kulitazama. Majibu yako yamekaa kihuni. Wenzako HUSAMEHE NA KUSAHAU. Haina maana kusamehe halafu unakumbukumbu ya hujuma za miaka sita iliyopita. Unaonekana ni mtu wa visasi, hutufai watanzania na huwafai wana Nzega.
Baya zaidi ni kuwa achana na LOWASSA. Heshima yako itashuka ukiendelea kumtukuza huyu jambazi. Achana nae jijenge kisiasa wewe mwenyewe.
Ni hayo tu