- Mheshimiwa Bashe, suala la Malecela na Mangula na EPA kusemwa majuzi sana kule Tabora, tulisema wazi lina mkono wa mafisadi baada ya kutemwa NEC na CC, na hapa sasa wewe mwenyewe unathibitishia wazi kwamba ni kweli, Bashe hizi siasa mmejifunzia wapi where unaishia kusema usichotaka kusema? Ha! ha! ha! ha! ha!
- Ndg william sikutaka kukujibu ila nikusaidie kwakuwa umekuwa nje ya nchi inawezekana huna taarifa nyingi za hapa Nyumbani,sikumjadili mangula usitafute chaka la kuficha maovu ya Baba yako hili la malecela kuhusika na EPA limeongelewa kwa mud mrefu na Vyombo vya habari hapa Nyumbani,ukiongelea UFISADI malecela nae ni FISADI tena ni miongoni ambao mwalimu Nyerere aliwataja katika KITABU chake alichoandika kuhusu HATMA YA UONGOZI WA NCHI YETU,thats why nilisema tukiongelea swala la UADILIFU wewe BINAFSI NI ZAO LA VIONGOZI WASIO WAADILIFU dont take it personal ,kinachoumiza taifa leo kuna ambao wamekuwa sehemu ya mfumo mbovu ,sehemu ya matokea ya mfumo huo lakini mbele ya PUBLIC wanajionyesha ni watu wema sana kama ulivo wewe,hatuwezi kujadili UFISADI,ama UADILIFU tukakuacha wewe Nje thats why niliamua kufunga mjadala wa LOWASA na kuomba let us not agree on this.
- I mean unashindwa kuelewa a very simple idea ya hii mijadala JF kwamba sio kushinda ila ni kuelimishana kihoja na wakati ni huu wa sasa, umeenda huko kwenye UV-CCM umewakaripia wee masikini wa Mungu wasioelewa kitu, sasa unakuja hapa unatakiwa kusimamia hoja zako mwenyewe, unalilia Malecela! ha! ha! ha! Malecela ndiye aliyekuambia umtetee Lowassa? Now seriously what Malecela has to do na msimamo kwamba Lowassa ni matatizo ya mamalaka zetu kama ana makosa mbona hawajamshitaki kwenye sheria, kweli this is all you could do kutetea msimamo mzito kama huo?
-Niweke record sawa sawa katika hili sikusema niko hapa kushindana bali nilisema tufunge mjadala huu wa lowasa kwani huu si wakati sahihi wakujadili hoja ya lowasa na nimekuwa clear kwamba tusubiri muda ufike kama atagombea na kuteuliwa binafsi kama mpiga kura nitampa kura yangu unless nipate hoja,sababu za msingi sio hizi hoja zako eti nilienda texas kupiga picha,mara ooh tulipambana kubenea akadhurika tutajuaje kama wewe na wale walioaminisha umma kwamba ni wapambanaji walikuwa sehemu ya mkakati ili mfanikishe mnayotaka basi mumdhuru kubenea ili kujenga imani na kufanikisha mpango wenu.Swala la kubenea kuumizwa kinyama halikuwa jambo jema,lakini ni makosa vilevile kutumia maumivu ya kubenea kuhalalisha ile sinema ya kuigiza.
Usipotoshe watu kwamba nilikuwa nafoka ,usiaminishe watu kwamba wewe ndo unaweza kufikiri kuliko wote waliokuwa katika kikao hicho,usiaminishe umma kwamba waliohudhuria hawana taarifa za kutosha juu ya Taifa lao,kilichokuleta speed hapa si msingi wa mjadala uliokuwepo bali ni swala la kusadikika lililojengwa na LAMPARD na hoja ya Makundi,mimi kundi langu mmelitaja na kulitamka sasa WEWE na LAMPARD kundi lenu ni lipi?mmenihukumu mm nipo kwa maslahi ya kundi flani,je nyinyi mnasimamia maslahi ya kundi lipi?na kundi hilo lipo kwa maslahi ya mtu yupi?
- Ninakushuru sana kwamba umetutaja sana JF kwenye media kwamba utatutumia na tume yako, that is all I see to be good kwenye hotuba zako, otherwise please Brother unahitaji ukarabati hali ya juu sana kuhusu kusimamia hoja zako hapa, sio wote hapa tumelala usingizi kama huko UV-CCM, nimeisoma sana hotuba yako sikutegemea kwamba watu wazima wenye akili timamu walikuwa wamekaa wanakusikiliza mwanzo mpaka mwisho bila hata kukuuuliza maswali!
-Katika hili tafsiri ya nani kalala na nani kaamka ni subjective inawezekana wewe ukawa na usingizi mzito wakati ukihisi umeamka,hotuba yangu inawezekana usiipende sana lakini hayo ni mawazo yangu ambayo wewe pia unayako ,haki uliyonayo wewe kuyapinga yangu,ni haki hiyo hiyo niliyonayo mimi kukataa mawazo yako,si lazima tufikiri sawa,tuamue sawa,ikitokea hivo wote tutakuwa na matatizo,na si lazima hapa katika forum tukawa wote na mtazamo unaofanana,na si lazima ukalazimisha nione unachoona na mm silazima nikakulazimisha ukaona ninachoona.
Nilisema tuufunge mjadala huu hapa kwani muda wa mjadala juu ya swala hili si sasa na tusipoteze nguvu nyingi sasa kujadili haya mambo,2014 tutakutana jamvini kujadili nani anafaa kuwa Rais wa Nchi yetu regadless anatoka wapi,sasa tutumie muda kujadili BEI MCHELE,BEI SEMBE,AJIRA,STABILITY YA UCHUMI WETU,UMOJA WA KITAIFA,KUPANDA KWA GHARAMA ZA MAISHA,NAULI ZA DALA DALA ZINONGEZEKA WAKATI VIPATO VYETU BADO DUNI,BEI ZA MAFUTA,TATIZO LA UMEME(Wewe hili hulifahamu bcs utotoni ulikaa upanga,unatumia jenereta,na sasa ukirudi likizo unatumia jenereta nyumbani na huko ulipo hamna mgao wa 16hrs) na kwa sisi wana CCM namna gani tunakisaidia chama kutekeleza majukumu yake kupitia serekali ili kuleta TIJA katika maisha ya watanzania ,haya ya lowasa na wengine si ya tija kwa sasa.Matatizo yetu hapa nyumbani ni ya msingi sana kuliko kujadili hayo unayotaka sasa tuyajidili.
- Well, karibu sana mkuu ukweli ni kwamba hapa hatushindani ila tunaweka hoja na wananchi wanaamua mchele na pumba zilipo, ila seriously sikufashamu sana ila sikutegemea this coming from you, wewe mwenyewe kaa chini uangalie hotuba yako na haya majibu yako hapa JF utajionea mwenyewe tofauti ilivyo kubwa sana na ndio inayotupelekea wengine wetu hapa kuamini kwamba ile hotuba hukuandika wewe, anyways karibu sana mkuu tulemishane kuhusu taifa letu, hopefully na wengine kama wewe huko CCM watakuja hapa kusimamia hoja zao, kama ulivyofanya, inatupa nafasi wananchi kuwaelewa vizuri, maana baada ya kukusoma hapa sasa sina wasi wasi kabisa kwamba ukipewa uongozi wa juu nitegemee nini toka kwako!
Mwisho inawezekana ulitarajia nifikiri kama wewe ambae umekulia ndani ya mfumo huu,ume enjoy matunda na sasa upo nje ya nchi ukiwa hujui bughudha za daladala,hujui tatizo la mgao ulitaka niimbe ngonjera zako, nimalize kwa kusema tena Turudi katika msingi wa mjadala wangu,nilichosema ninakiamini,nitakisimamia sitabadili msimamoa katika hilo unless kuwe na Tangible Facts juu ya yale uliosema,Kuhusu kuandikiwa hotuba ni vizuri umesema hunifahamu kwahiyo kama walivosema wahenga USILOLIJUA NI USIKU WA GIZA,so nivizuri ukapata muda kidogo kunifahamu na hilo utaweza tu kama utajipa muda kunifahamu.
MUNGU AIBARIKI JF!
MUNFU IBARIKI TANZANIA MUNGU IBARIKI AFRIKA
William @ NYC, USA.