UVCCM: Hussein Bashe amjibu Nape kiaina

UVCCM: Hussein Bashe amjibu Nape kiaina

Alisema wasitumie muda Mwingi kujadili chadema tutumie muda mwingi kujenga chama chetu na kutimiza wajibu wetu, alimaliza kuwaasa vijana wasiwaze kuwa CCM ni watawala alisema dhana hiyo ni mbovu,bali alisema dhana sahihi ni kujenga Fikra kuwa CCM ni chama kinachoongoza ni si Tawala. Alisema leo CCM inaimba Nyimbo za Chadema na akasema Tumeingia katika POLITICAL TRAP ya chadema tunafanyia kazi ya kwao na kuacha ya kwetu 2015 tutaulizwa yakwetu tutakua hatuna majibu, alisema CCM tumekua REACTIVE badala ya PROACTIVE,badala ya kuwa Viongozi sasa Tunaongozwa,Tumebaki kuwaza Madaraka Badala ya kuwaza Namna Gani tutamiza wajibu wetu.

Aliwataka UVCCM kubadilika na kusema Maslahi ya Nchi na Chama yatalindwa kwa sisi kutekeleza wajibu wetu na kuacha UROHO wa Madaraka bila ya hivo tutaivuruga Nchi na Chama chetu alishangaa Tabia sikuhizi ccm kila mtu anasharubu na Kutoa Matamko.
Bashe kwanini unatumia jina la kificho? Unayoyasema yana mantiki na ingekuwa credit kwako zaidi kama ungekuja na jina lako hasa!
 
Ndugu Hussein Mohammed Bashe bado ananipa wasiwasi kuwa hali za mivutano kule Nzega hajazimaliza............naendelea kuamini hivyo? i know politics na nimesomea and i know what i mean by saying that, kwanza naomba ukane hadharani huna jeraha,vita, kisasi kwenye nafsi yako juu ya uchaguzi wa jimbo la Nzega na mtu yeyote. na hili linalozunguka sasa kwamba ukishindwa wewe kurudi jimboni nzega mnamuanda kijana mwenzio SALIM ALLY wa UDSM kuja kuchukua jimbo 2015 je hili ni kweli?.

-umezungumza kuhusu uchaguzi na wanaccm 2015, mbona wewe tayari unakundi lako kwa ajili ya LOWASA AMA NCHIMBI kuwa rais baada ya Jakaya? mbona unaongoza zengwe la kumuingiza JAMAL KASSIM kuwa mwenyekiti wa Taifa UV-CCM na katika hilo wewe ukiwa kama mhasibu wa kutunza pesa za kampeni na kuwagawiya wapiga kura? sijui unapozungumza hayo unadhani unayofanya wewe wananchi hawaoni ama hawaelewi? na hili mnalopanga la mdogo wako IBRAHIM MOHAMED BASHE kuwa Rais wa UDOM mmefikia wapi? maana naona maandalizi ni makali sana, JUA TU KWAMBA KILA MNALOFANYA NA KUNDI LAKO LINAFAHAMIKA ila natakakusema tu huo ndio mwisho wenu wa kufanya haya madudu yoooooooooooye...yoooote so kila mnaloona mnaweza kufanya fanyeni after muda fulani ndio mwisho wa kundi lenu wote kuwalaghai WATANZANIA.

-UVCCM ambayo wewe ni mjumbe mnakazi kubwa sana kuibadilisha, ila nadhani ndio mnakamilisha muda wenu wa umri kikanuni sitegemei mnaweza CHAKACHUA TENA UMRI MRUDI HAPO, malizeni muda wenu waingine VIJANA WANAOWEZA FANYA KAZI SAWA SAWA KWA MASLAHI YA VIJANA WA TANZANIA, naamini nusu yenu mnaondoka 2012, japo mnapiga debe suala la umri liongezeke ili muendelee kukaa hapo UVCCM kwa maslahi ya kundi lenu, enough is enough.

Mwengine huyu ndani ya Gamba, Kigwangwalla!
 
[/I][/B]
Mr. Bashe,
1) Achana na visasi jifunze -forgive & forget
2) Jijenge kisiasa wewe mwenyewe - yuko sahihi mno jamaa kukwambia hivyo, huenda we hujijui waweza simama na miguu yako mwenyewe, na kwa hayo uliyosema unakubalika na mtu mwenye busara yeyote hasa unapokemea udini, ukabila na mashambulizi ya binafsi (personal attacks) badala ya kuleta maendeleo kwa wananchi
3) Karibu CDM ukishasimama mwenyewe!

Just curious! Hivi Bashe kama anaona Lowassa ni kiongozi mzuri, na zaidi ya hapo anafanya kazi na Rostam kweli CDM wanaweza kufanya kazi na mtu wa hivi? Kuna usemi unasema " kama unataka kujua mimi ni mtu wa aina gani try to study those I hang out with." I am not a politician but; hizi siasa za kuhama hama ndio zinazovuruga vyama. Hivi Tanzania mwananchi hawezi ku-support kiongozi/viongozi wa chama kingine mpaka ujiunge na hicho chama? Kama kweli tunatanguliza nchi kwanza why are we supporting someone kutokana na itikadi/chama chake na sio uwezo wake?
 
Bashe unapiga porojo tu za siasa tu na nakuhakikishia ubunge wa Nzega utausikia tu kama ukiendelea kujaza orodha ya miaka 20 ya hujuma. We kiongozi gani unasema oooh nimesamehe lakini siwezi kusahau mwaka XYZ mara sina kinyongo lakini sitasahau mwaka XXX mara ooh sina tatizo na mtu lakini sijasahau mwaka XY! Hayo ya kuto kusahau unayaweka ya nini? Kama huwezi kusahau bwana mdogo siasa haikufai nenda kawe mvuvi tu.
 
Bashe unapiga porojo tu za siasa tu na nakuhakikishia ubunge wa Nzega utausikia tu kama ukiendelea kujaza orodha ya miaka 20 ya hujuma. We kiongozi gani unasema oooh nimesamehe lakini siwezi kusahau mwaka XYZ mara sina kinyongo lakini sitasahau mwaka XXX mara ooh sina tatizo na mtu lakini sijasahau mwaka XY! Hayo ya kuto kusahau unayaweka ya nini? Kama huwezi kusahau bwana mdogo siasa haikufai nenda kawe mvuvi tu.

Kabwela Mzito

Huwezi kupanga Mkakati wako wa kesho kwa kusahau Matukio ya Jana,Huyu dogo ameonyesha ukomavu wa Kisiasa na Uongozi,Kiongozi Makini ni Yule ambae anatumia Historia kama Sehemu ya Kumbukumbu zake Muhimu.Matukio yaliyomkuta Bwana Bashe hawezi kuyasahau kwani hayo ni sehemu ya Historia yake ya Maisha yake ya Kisiasa.

Angesema Sijasamehe,Angesema Atalipiza Kisasi hata Mimi Ningelimshangaa,Angesema Amesamehe na Amesahau Ningelimshangaa kwani Watanzania Wengi Tunalikumbuka Tukio la Mwaka Jana ambalo lilinifanya hata Mimi kutaka Kumfahau Bashe.

Umesema Ubunge Asahau kwakuwa anakumbuka Matukio yaliyomkuta katika siasa Nakushangaa ni namna gani unataka kiongozi ambae hana kumbukumbu ya Matukio yaliyomkuta yeye Binafsi,je atakumbuka matukio yaliyowakuta anaowaongoza?Leo hii sisi watu wa Kagera Tumesamehe Uzembe wa Serekali yetu iliyopelekea ndg zetu kufariki ktk tukio la MV BUKOBA lakini hatuwezi kusahau kwani ni sehemu ya Historia yetu.

Bashe samehe lakini Usisahau wana Nzega wanakumbuka Iweje wewe Usahau utakua kiongozi Dhaifu asiekuwa na Kumbukumbu ya Historia yake Binafsi.

Ila dogo CCM ndo mwisho wake ondokaaaaaaaaa
 
Hotuba imetulia kisawasawa... hatutaki majungu ila maisha ya Mtanzania yaboreshwe iwe CCM. CDM, CUF sawa ila maisha ya mtanzania yakae sawa
 
.....Akili za mwenzio changanya na za kwako.....hata malaika wa shetani ana mabawa...
 
Bashe unapiga porojo tu za siasa tu na nakuhakikishia ubunge wa Nzega utausikia tu kama ukiendelea kujaza orodha ya miaka 20 ya hujuma. We kiongozi gani unasema oooh nimesamehe lakini siwezi kusahau mwaka XYZ mara sina kinyongo lakini sitasahau mwaka XXX mara ooh sina tatizo na mtu lakini sijasahau mwaka XY! Hayo ya kuto kusahau unayaweka ya nini? Kama huwezi kusahau bwana mdogo siasa haikufai nenda kawe mvuvi tu.

Mzito kabwela, kuna tofauti kubwa kati ya Kusamehe (Forgive) , na kusahau (Forget) .Bashe mimi ni mpiga kura wako wa Nzenga na ni mmoja wa wanachama wa CCM waliokupigia kura kilichofanywa na JK a.k.a Mbayuwayu si tu kilikuhumiza wewe hata sisi wananzega kilituhuzinisha sana ,na Ninakuhunga mkono statement yako ''umesamehee lakini hautasahau'' Waziri mkuu wa Uingereza miaka ya 1930, s Benjanim Israel aliwahi kusema ili ufanikiwe katika siasa za ni vizuri umsamehee adui yako lakini usisahau jina lake ''Forgive your are Enemy but never forget is name".Na Tunapenda kukuhakikishia kwamba hatujamsamehee Mbayuwayu na mwanae shorti(mfupi kama mbilikimo) the way walivyo treat suala la jimbo la Nzega
Mzito Kabwela Please ya Nzega tuachie wana-Nzega
 
Kwa kweli katika hili Bashe ameongea vema . Nadhani Hata kikwete amesikia huko Mwanza ingawa yeye ndiye mdini wa kwanza. Watu hawataki hadithi wanataka kuona sukari ,unga mafuta vinapungua bei. Sasa haya magamba mengine hayaelewi yanakalia porojo kwenye majukwaa ambayo hata watu hawahudhulii kwa wingi. Dr Slaa endelea kuwaelimisha watu juu ya haki zao ili Mkwele achomoke kabla mambo hayajawa mabaya maana mi naona 2015 ni mbali sana na shida zitakuwa zimetumaliza.
 
Bashe hoja ulizotoa zinaua chama chetu nani kakuambia useme hayo yote? umekosa uzalendo katika chama
 
ni hotuba nzuri......lakini mapacha watatu lazima wahukumiwe kutokana na matendo yao ndipo wananchi tutakapo kuwa na imani na chama chenu.....
 
Huyu kijana ameongea pointi nzuri sana, sasa sijui kama wakubwa wake watakubali huo ushauri
 
Baada ya kusoma post ya kwanza ya thread hii nikajiambia " well saida Bashe" lakini majibu aliyotoa bashe kwa lampard (offcourse ana uhuru na haki ya kujibu kama alivyo jibu) ndipo nikaona kuna uwalakini ... kama kweli Bashe anamsapport Lowasa, basi ...
 
Ndg yangu Lampard acha Upotoshaji,

Nikujibu kwa Ufupi:

Sikweli kuwa nina mdogo wangu aneitwa IBRAHIM anaesoma UDOM, mdogo wangu Ibrahim amemaliza Mzumbe na sasa yupo Mtaani akitafuta ajira kama Vijana wengine wa Kitanzania.

Hoja ya kwamba nina jeraha, ama kinyongo, ama chuki nayo ni Upotoshaji. Sina kinyongo that's why nilirudi Jimboni kumsaidia aliyeteuliwa ili chama changu kishinde, this tells a lot. Nadhani waliokupa taarifa hizi wamekupotosha. Lakini haina maana nimesahau yaliyotokea na wala sipo hapa kujadili uhalali wa hoja iliyotumika kutoniteua, bali nikuthibitishie sina kinyongo lakini siwezi kusahau kama ambavyo sijasahau matukio. Ya 2007, Kizota pale jina na kura nilojipigia zilipopotea kimuujiza. Sitasahau ya 2005 Nzega ktk kura za maoni na mimi kuwa Mshindi wa Tatu, sitasahau ya 2008 Dodoma, yote haya yamekua sehemu ya Historia yangu hayatafutika lakini sina kinyongo.

2010 nilimsaidia mbunge wangu kwani niliamini si yeye wala Chama (taasisi) walionikosea that's why mimi na team yangu ilimsaidia Kigwangalla.

Hoja yako kuwa ninamuandaa SALUM ALLY ni hoja potofu, 2015 kama nilivowahi kusema nitarudi kugombea Jimbo la Nzega na hivi sasa naendelea kutekeleza ahadi nilizotoa 2010 kwani wana Nzega walinipa kura 14,420 kati ya kura 19,000 zilizopigwa.

Hoja yako ya kuwa mimi nina kundi: Hakuna mwanasiasa asiyekuwa na kundi lake, msingi wa hoja yangu ni kwamba siasa 2015 zinakiumiza chama kwani sasa kuanza mikakati hiyo ni kudhoofisha chama wajibu wangu na wewe na wana CCM wote ni kumsaidia Rais Kikwete kutekeleza Majukumu yake KUFIKIA MATARAJIO ya WATANZANIA; bila ya hivo 2015 CCM haitakuwa na uhalali wa kuchaguliwa, ni wendawazimu kuanza kampeni leo wakati hata nusu ya tearm ya Pili ya Kikwete haijafika. Nikushauri acha mawazo mgando hayo.

Hoja yako kuwa namuunga Mkono Lowassa na Nchimbi kwa URAIS nayo ni upotoshaji. Hawa watu hawajatangaza labda wamekuambia wewe mimi sina taarifa. Ila kama Lowassa atasema anagombea sitasita kumuunga mkono kwani ninaamini katika uwezo wake wa kusimamia na kufanya kazi hilo sina mashaka nalo (ni msimamo wangu binafsi ambao unaweza kuendelea kubaki hivi ama kubadilika kulingana na wakati husika), kama chama kitamteua nitamuunga mkono bila shaka. Lakini sasa sina taarifa hizo.

Hoja ya Jamal nayo ni upotoshaji. Si kweli unalosema, na usimzushie ili aonekane ameanza kampeni mumkate, na mtu anapokuwa na Uwezo ni vizuri mkakubali. Uwezo wa Jamal hauna mashaka, kama chama kitamteua atahukumiwa na wapiga Kura na mimi nitakayemuunga mkono muda ukifika utamjua kwani sina sifa ya Kujificha katika Msimamo wangu.

Ndg yangu,

Hoja yako juu ya umri nikutoe shaka; Mimi ninaheshimu kanuni na taratibu, sina uroho wa madaraka, Kamati yangu haijapewa ktk Hadidu rejea zake hatuna suala 'Umri' kwa hiyo usiwe unahukumu bila Facts.

Pia ninapoongelea hoja ya Urais 2015 ninamaanisha kwamba wana CCM tufanye siasa 'above Group Politics' kwa Maslahi ya Chama Chetu na taifa. Linapokuja suala la nchi ni muhimu kufanya kazi 'Above Party Politics', hii itaisaidia nchi yetu. Nikushauri usipende kuwa kasuku, ongea kitu ambacho unakijua na una Facts zake. Ni rahisi kujua UJINGA wa mtu kupitia maandishi, kwahiyo wanpokupa cha kuongea fanya uchunguzi.

Lampard, nimeona kauli yako unasema kundi letu mtalimaliza; maana yake wewe una kundi unalolinda. Usionyeshe 'ujinga' wako kirahisi hivi. Nchi hii imeumizwa na 'Cheap Politics' ni Vizuri ukaanza kufikiri above Group Politics na Party Politics. Fanya uchunguzi kuwa na Facts kabla hujaongea.

Ndg yangu Lampard,

Nikuombe usiwe miongoni mwa wanaoumiza nchi kwa kufanya siasa ambazo ni 'Based On Speculations'.

Leo nchi yetu imeumia sana kwa aina hii ya siasa, CCM kimekuwa chama ambacho kinaumizwa sana na siasa hizi za Uzushi na Uongo.

Nilivyokusoma unaonyesha wewe ni Mwana CCM mwenye kundi ndani ya CCM. Nikushauri usikubali kila unachoaminishwa. Jifunze kuwa tabia ya kuhoji, why, how, when, which, what... Hii itakusaidia kusimamia unachoamini kwa Hoja.

Nimeona ukijisifia usomi wako wa Siasa; Nikiri inawezekana ni msomi wa siasa, basi anza kuwa 'Mwana Tafakuri' ili usomi wako uwe na Tija. Usikubali kuugua ugonjwa wa kugawanyika kwani ukianza kauli hizi KUNDI LENU na KUNDI LAO na KUNDI LETU, kesho utaingia katika kansa ya Kugawanyika ambayo hutumiwa na wana siasa MUFLISI ambao hujadili na kutazama mambo kwa Msingi wa Ukabila, Dini, Ukanda n.k. Tutaua nchi na chama chetu, waambie walokupa taarifa Next time wakupe Taarifa za kweli.

Mwisho nikuhakikishie: Sina Kinyongo, Sina Hasira bali sijasahau, Nzega 2015 sina ninayemuandaa Nzega bali nitarudi kugombea mwenyewe.

Kila la kheri Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika.

Heshima kwako Hussein Bashe.

Kwanza naomba kukupongeza kwa kuja jamvini na kujibu baadhi ya hoja na kutoa ufafanuzi katika masuala mbali mbali.Nikiri umejitahidi kujenga hoja lakini pia nikiri lugha unayotumia haifai kabisa ndani ya jamii iliyostaharabika,imejaa dharau,kiburi na zaidi ya yote inakatisha tamaa.

Umekiri mwenyewe umechezewa rafu kibao ndani ya chama chako baya zaidi umeonyesha dhahiri wewe ni mtu wa visasi na vinyongo.Vipi mambo uliyotendewa miaka mingi nyuma hutaki kusahau ? Labda imani na asili yako imekufunza hivyo,ukitendewa jambo baya siku zote ni lazima ujifunze kusamehee na kusahau.Ni uzushi na ubazazi kusema umesamee jambo fulani lakini huwezi kusahau.

Unakiri Lowassa akigombea urais utamuunga mkono hakika kati ya mambo ya kipumbavu uliyowahi kukiri hadharani hakuna kama hili na ikiwa msimamo wako ni huu hakika waliokunyima nafasi ya kugombea ubunge hawakufanya kosa kabisa walikuwa sahihi na ikiwa watakufanyia tena mwaka 2015 watakuwa wamelitendea taifa letu changa jambo jema.

Nikiri mwamzoni nilidhani Bashe ni miongoni mwa vijana wanaoweza kulisaidia taifa lakini baada ya kupitia andiko lako nimegundua hufai hata kurejeshewa uraia wa Tanzania.Vijana wa aina yako ndio wameifikisha Somalia hapo ilipo sasa [kukumbatia magaidi na wezi wa mali za umma]

Mwisho Mungu hawezi kuibarikia Tanzania wala Afrika kama tutawatukuza wezi na mafisadi.

Naomba kuwasilisha.
 
Jamani pamoja na yote inabidi jamaa asifiwe kwa kusema ukweli,hivi mtu hawezi kuwa na mawazo huru mpaka atumwe na watu wengine?jaribuni kusoma maudhui ya ujumbe acheni kumjaji mtu binafsi,ameongea ukweli kabisa kuhusu mstakabali wa maisha yetu amekikosoa chama cha magamba,amemkosoa Nape,nampa big up maana tunakokwenda kuna giza na mkulu mwenyewe chenga tupu.nawasilisha
 
suala sijui bashe katumwa anamuongelea nani hili si la msingi, la muhimu ni ujumbe aliousema una mashiko si mchezo. Saa nyingine hata vichaa na wendawazimu huongea ukweli judge the message not the messenger

jamali kassim naye anajua siasa??? Ccm mmekwisha
 
Back
Top Bottom