Uturuki: Wanawake wapigwa marufuku kucheka hadharani

Uturuki: Wanawake wapigwa marufuku kucheka hadharani

Dj mat

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
747
Reaction score
476
Inaweza kuwa kali ya mwaka, lkn ni kweli imetokea nchini Uturuki ambapo wanawake wamezuiwa kucheka hadharani kwa madai kuwa hali hiyo inachangia kuporomoka kwa maadaili.

Agizo hilo limetolewa na Naibu waziri mkuu wa nchi hiyo Bulent Arinic ktk salam zake za sikukuu ya Eid El Fitri.

Aliongeza kuwa wanawake pia wamekuwa na tabia ya kutumia simu kwa muda mrefu kujadili mambo yasiyo na msingi.


Source: Gazeti la Mwananchi 03/08/2014

Kauli kama hiyo ikitolewa hapa bongo itatekelezwa?
 
Filomena imagine if u were there

Unajua nimekuwa speechless baada ya kufikiri ningekuwa ni mim ndo napewa hayo masharti.....
Tuache utani usilolipenda usimfanyie mwenzio period! Mwanaume utabaki kuwa mwanaume tu hata iwaje msitake kuonekana kwa nguvu wakati tayari mnaonekana.
 
Unajua nimekuwa speechless baada ya kufikiri ningekuwa ni mim ndo napewa hayo masharti.....
Tuache utani usilolipenda usimfanyie mwenzio period! Mwanaume utabaki kuwa mwanaume tu hata iwaje msitake kuonekana kwa nguvu wakati tayari mnaonekana.

Waislamu waangalie sana baadhi ya sheria zao, nyingine ni kandamizi kupindukia...
 
Nnavyopenda kucheka ningepigwa risasi hadharani,
 
Huo uonevu uliopitiliza kucheka si maamuzi binafsi mwanaume akicheka havunji maadili ila mwanamke anavunja

Pia amesema hv "siku hizi maadili yameporomoka ,wanawake wanachekacheka hovyo hadharani jambo ambalo linanikera sana.Lazima tubadilike,turudi ktk misingi yetu".
 
mtu akicheka tu hadharani amevunja maadali;hatari sna

Mkuu ndo Uislam huo! Shangaa pole pole wasijekutusikia! Kwenye nyuzi kama hizi huwezi kumwona FaizaFuska, Kahtaan and the like!! Wanaishia kuchungulia kwa mbali tu!! Ingekuwa habari kutoka kijiblogu cha Le Mutiz na habari za kugeuzwa kanisa ungewaona wanavyopiga kelele na kuachia mapaja wazi!
 
Mkuu ndo Uislam huo! Shangaa pole pole wasijekutusikia! Kwenye nyuzi kama hizi huwezi kumwona FaizaFuska, Kahtaan and the like!! Wanaishia kuchungulia kwa mbali tu!! Ingekuwa habari kutoka kijiblogu cha Le Mutiz na habari za kugeuzwa kanisa ungewaona wanavyopiga kelele na kuachia mapaja wazi!

Mkuu hapa Uislam unahusika vipi?

Aliyetoa amri ni Sheikh?

Ni wapi ametamka kwa niaba ya Uislam?

Kama ni Eid hata wasiyo Waislam kama Mizengo pinda wametoa speech ..
 
Hahahaha hahah nicheke mimi kabla na huku hatujakatazwa
 
Naam, mwanamke kujichekesha-chekesha hovyo hadharani inahusu nini?

Huyo waziri barabara kabisa. Na hilo la simu wala si uongo, wengi utawakuta wanaongea mambo ya kijinga-jinga tu.
 
Naam, mwanamke kujichekesha-chekesha hovyo hadharani inahusu nini?

Huyo waziri barabara kabisa. Na hilo la simu wala si uongo, wengi utawakuta wanaongea mambo ya kijinga-jinga tu.

prs ulikuwa unabisha nini!? huyu hapa ni muislamu hasa na ni mwanamke.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom