Utunzaji wa vyakula kwenye friji

Utunzaji wa vyakula kwenye friji

Habari!!!! Naomba kujua mnatunza vipi vyakula kwenye friji ili visiharibike? Mfano; samaki,nyama,nyanya,karoti,matunda,na mboga mboga? Je? Mnawasha friji kila siku bila kulipumzisha,au mnawasha kwa mda tu na kuzima?
Friji huwa haizimwi, na binafsi yangu toka nilipoliwasha mara ya kwanza sijawahi kulizima

Huwa linazimika lenyewe pale umeme ukikatika na umeme ukirudi ngoma isambe na nimeweka fridge guard kwa hiyo hofu ya kuungua sina

Kuhusu vyakula, nyama naweka kwenye mifuko ya nylon kisha nagandisha pia sausages n.k

Vingine kama maziwa fresh na mtindi naweka kwenye friji hivi kwa ubaridi tu zinadumu

Kuna baadhi ya misosi au matunda hayapaswi kuwekwa kwenye friji hivyo siyanunui kwa wingi kama tikiti, mkate n.k
 
KUHIIFADHI KAROTI
Osha vizuri
Zimenye maganda yote ziwe safi
Weka kwenye bakuli safi
Tia maji kwenye bakuli karot ziwe chini maji yawe yamezid
Funga mfuniko wa bakuli lako hifadhi kwenye jokofu
1. Zitaweza kukaa muda gani bila kuharibika?
2. Zikiwekwa kwenye maji bila kuondoa maganda zitaharibika?
 
Pia kuna zile zip bags maalumu kwa ajili ya kuhifadhia vyakula aidha kwenye freezer au fridge.
 
Mnawasha Jokofu Ila umeme hamtaki kulipia -hii ndo akili ya MTU mweusi.

Nyumba za kupanga MTU hana vyakula hana vinywaji Ila anawasha jokofu anaweka maji ya chumvi

Akili za black people.
 
Nyanya blend, uichemsheeee hadi iive ikauke kabisa maji.....ikipoa weka kwa kontena freez, utamaliza mwaka mzima haununui nyanya.
Wakati wa ku-blend nyanya unachanganya na maji kidogo au nyanya zenyewe tu bila kuongezea maji?
 
Unawasha masaa 24 wakati kuna maziwa lita 1, angalia gharama ya umeme na hayo maziwa. Kiuchumi imekaaje?
 
Hauweki maji, nyanya yenyewe ina maji ya kutosha
Na kama umei-blend na kuihifadhi kwenye freezer ambapo itaganda unapohitaji kuitumia si utalazimika kuweka maji kidogo kwenye chombo ili yasaidie kuibandua/kuiyeyusha kukuwezesha kuchota kidogo ya kutumia siku hiyo? Na ukifanya hivyo si maji yatapunguza ladha yake? Au utafanyaje ili kwenye kuchota kidogo kidogo kusisababishe inayobaki ikapoteza ladha yake ndugu?
 
Na kama umei-blend na kuihifadhi kwenye freezer ambapo itaganda unapohitaji kuitumia si utalazimika kuweka maji kidogo kwenye chombo ili yasaidie kuibandua/kuiyeyusha kukuwezesha kuchota kidogo ya kutumia siku hiyo? Na ukifanya hivyo si maji yatapunguza ladha yake? Au utafanyaje ili kwenye kuchota kidogo kidogo kusisababishe inayobaki ikapoteza ladha yake ndugu?
Hapa sidhani kama itakauka maji,hiyo process hapo ni kama vile unakuwa umetengeneza nyanya za kwenye makopo hazikauki maji bali zinakuwa rojo rojo...
 
Hapa sidhani kama itakauka maji,hiyo process hapo ni kama vile unakuwa umetengeneza nyanya za kwenye makopo hazikauki maji bali zinakuwa rojo rojo...
Na kama kwa process hiyo utapata kitu rojo rojo pale utakapoweka kwenye FREEZER si baridi yake itagandisha kabisa hiyo rojo rojo?
 
Na kama umei-blend na kuihifadhi kwenye freezer ambapo itaganda unapohitaji kuitumia si utalazimika kuweka maji kidogo kwenye chombo ili yasaidie kuibandua/kuiyeyusha kukuwezesha kuchota kidogo ya kutumia siku hiyo? Na ukifanya hivyo si maji yatapunguza ladha yake? Au utafanyaje ili kwenye kuchota kidogo kidogo kusisababishe inayobaki ikapoteza ladha yake ndugu?
Ikiganda muda unataka kuipikia unatoa kontena inakaa inayeyuka kidogo unatoa, au unatoa na kisu....

Nb: tumia kidogo sana inakolea kama nyanya ya kopo
 
Back
Top Bottom