Kuna jamaa yangu figo zake ziliacha kufanya kazi mtoto wake wa kipekee alijitolea kumpa moja lakini bibi mzaa baba akakataa mjukuu wake atoe kwa kudai mwanae ameshaishi vya kutosha afe tu sio kumuumizia mjukuu wake wa pekee,na kweli baada ya muda akafariki dunia.Sasa huzuni ilikuja baada ya mjukuu nae kuuawa na majambazi baada ya miaka 2 kwa hiyo bibi akakosa wote.Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!
Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?