Utu na utoaji!

sidhani dearest....manake vitu vidogo tu tabu ije kuwa figo...maybe mama yangu mzazi
Kuna kitu nimefikiria kufanya...sio ethical ila ntapata kujua wangapi watoaji wangapi sio!Ntaleta feedback!
 
sjui kwanini hii comment yako ndio nimeiamini zaidi halaf ile ya BJ kisha ndio zinafatia nyengine. Nadhani hapa tunajiburudisha tu lakini likija suala la utoaji kweli usishangae hao wanaosema watatoa wakazima simu zao, mimi bana only God knows, sio mchoyo lakini na laifu nalipenda ajabu.

Acha uchoyo!Tukifa wote utakula life na nani?
 
Kuna kitu nimefikiria kufanya...sio ethical ila ntapata kujua wangapi watoaji wangapi sio!Ntaleta feedback!

usipoleta mi na wewe....lile suala lingine hadi leo hujaleta feedback,nakuangalia tu...9t 9t dearest!
 
Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!

Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?

Lizzy kisa chako kimenigusa sana.

Achilia kutoa figo, kutoa damu tu ya kumwongezea ndugu huwa inakuwa mgogoro. Wengine hata wakiambiwa watest damu hawarudi tena hospitali.

Ndo maana wenye pesa zao wanaenda apolo India. Nasikia huko kuna wahindi wengi tu wanauza figo zao kujikwamua kimaisha.

Binafsi, napima kama ikitokea naweza? I guess kwa mtu ambaye nina mapenzi makubwa sana kwake nitaweza kwa neema ya Mungu.
 
Sijakuelewa wewe na mtoaji damu wako!Ilikuwaje mpaka imzidie mgonjwa?
ok umekula leo lakini? kama haujakula ni tabu sana kunielewa ujue!

ni hivi, BJ ameongelea kwamba check up ya haja inahitajika na afya kuthibitishwa kabla kugaiana mafigo kwa vile uhai sio kitu cha kuchezewa, namimi nikasisitiza hilo kwa kutoa mfano hai kabisa, lakini mfano wangu haukuegemea kwenye kugaiana mafigo, umeegemea kwenye kuchangiana damu ambapo check up ya kizembe ilifanyika. Aliechangia damu hakuwa na damu ya kutosha kuchangia damu.
 
SuperMan yani mpaka damt watu wanabania??Hiyo ni hatari sasa!Mbona mtu hata hapungukiwi chochote??Binafsi napenda sana kua blood donor sema kwa sasa siwezi...
 
majini mahaba si yapo bana! dah! yaani naomba kesho akuje mshefa alembee sredi anaomba mchango wa figo halaf tuone kama mtaonekana online.

Nimekusoma pale juu..nlikua sijaelewa kwamba aliyotoa nae alipungukiwa!!Hehehe nna uhakika yangu haitaendana na yake!
 
SuperMan yani mpaka damt watu wanabania??Hiyo ni hatari sasa!Mbona mtu hata hapungukiwi chochote??Binafsi napenda sana kua blood donor sema kwa sasa siwezi...

Lizzy mimi nimeshuhudia mara nyingi tu. Wakati sisi wengine kutoa Damu ni hobby, kuna watu ni kama kiama hivi. wengine wanadai itagundulika ina "Mchanga" LOL.

Kwa nini kwa sasa huwezi kutoa?
 
Lizzy mimi nimeshuhudia mara nyingi tu. Wakati sisi wengine kutoa Damu ni hobby, kuna watu ni kama kiama hivi. wengine wanadai itagundulika ina "Mchanga" LOL.

Kwa nini kwa sasa huwezi kutoa?

Hahahaha eti ina mchanga!!Mmh low iron...inabidi nijiweke sawa kwanza!
 
Watu wanaogopa hata kutoa damu nini figo. Hasa mtu akijua hajatulia anaogopa asijeambiwa afya haijatulia.
 
Ukweli ukibidi kusemwa, usemwe tu. Mi kwa sasa naona napata tabu hata kufikiria. Na siwezi kujikosha kwa kujipa ujasiri hata niliokuwa sina. Nahofia kuja kunifika then nikaenda kinyume na kauli zangu za majigambo. Mungu atunusuru na haya ila jibu nitakuwa nalo endapo kama yatatokea kwa watu wa karibu nami.
 
Back
Top Bottom