Utu na utoaji!

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,799
59,264
Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!
Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?
 
KUna watu naweza wapa figo yangu kama tuna match.....ni ngumu dearest kusema ukweli,kuwa naweza mpa kila ndugu yangu au kila rafiki yangu
 
Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!
Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?
dah! napita transit tu wakuu.
 
Bila shaka yoyote, ningekuwa na kaka au dada na wanahitaji organ donor bila hata kuombwa ningependekeza nipimwe nione kama kama niko match na kujitolea. Vivyo hivyo ningefanya kwa baba, mama, au mwana.
 
sasa kwanini usiende kupima nakumsaidia huyo mzee? kama utamechi nae kwakuwa umeonyesha moyo bora ufanye hivyo silazima awe rafiki au ndugu kuta ni moyo
 
sasa kwanini usiende kupima nakumsaidia huyo mzee? kama utamechi nae kwakuwa umeonyesha moyo bora ufanye hivyo silazima awe rafiki au ndugu kuta ni moyo

Angekua huku UngaLTD labda ningefikiria kumsaidia!
 
Bila shaka yoyote, ningekuwa na kaka au dada na wanahitaji organ donor bila hata kuombwa ningependekeza nipimwe nione kama kama niko match na kujitolea. Vivyo hivyo ningefanya kwa baba, mama, au mwana.

Afadhali bado wapo wenye mioyo ya kujitolea...
 
Linapokuja suala hili, watu wengi tunakuwa wabinafsi na kuhofia kupatwa matatizo au kufa tukisaidia..Nadhani ushauri mzuri wa kiafya juu ya hili unahitajika katika jamii mana wengine unawaza kutoa figo basi maisha yanakuwa na hitilafu.
Inapokuja kwa wazazi & watoto nitaobarikiwa, nitasaidia kadiri ya uwezo wangu la afya ikiruhusu!!..sina siblings!!
 
Linapokuja suala hili, watu wengi tunakuwa wabinafsi na kuhofia kupatwa matatizo au kufa tukisaidia..Nadhani ushauri mzuri wa kiafya juu ya hili unahitajika katika jamii mana wengine unawaza kutoa figo basi maisha yanakuwa na hitilafu.
Inapokuja kwa wazazi & watoto nitaobarikiwa, nitasaidia kadiri ya uwezo wangu la afya ikiruhusu!!..sina siblings!!
good point BJ, nimewahi kushuhudia kesi moja jamaa kaenda kumsaidia jamaa damu halaf msaidiaji damu akapaparika paparika kama kapigwa shoti ya umeme halaf akapoteza faham, baada ya kuchunguzwa kumbe yule msaidiwaji ana damu nyingi kuliko msaidiaji, ikabidi jamaa alejeshewe damu yake haraka iwezekanavyo.
 
BJ kweli elimu inahitajika ili watu wajue kujitolea figo moja sio kutaka kifo!

We Kloro mbona sijakusoma!?Kwani wanamwekea mtu damu tu bila mpangilio?
 
BJ kweli elimu inahitajika ili watu wajue kujitolea figo moja sio kutaka kifo!

We Kloro mbona sijakusoma!?Kwani wanamwekea mtu damu tu bila mpangilio?
haujanielewa mimi au BJ? huo wangu mimi ni mfano tu wa kusisitiza point ya BJ, rejea post ya BJ.
 
good point BJ, nimewahi kushuhudia kesi moja jamaa kaenda kumsaidia jamaa damu halaf msaidiaji damu akapaparika paparika kama kapigwa shoti ya umeme halaf akapoteza faham, baada ya kuchunguzwa kumbe yule msaidiwaji ana damu nyingi kuliko msaidiaji, ikabidi jamaa alejeshewe damu yake haraka iwezekanavyo.
confirmed.....Kloro is crazy...can anyone help with a new brain for him??? pls call 811
 
sidhani dearest....manake vitu vidogo tu tabu ije kuwa figo...maybe mama yangu mzazi
sjui kwanini hii comment yako ndio nimeiamini zaidi halaf ile ya BJ kisha ndio zinafatia nyengine. Nadhani hapa tunajiburudisha tu lakini likija suala la utoaji kweli usishangae hao wanaosema watatoa wakazima simu zao, mimi bana only God knows, sio mchoyo lakini na laifu nalipenda ajabu.
 
confirmed.....Kloro is crazy...can anyone help with a new brain for him??? pls call 811
hehehe halaf hii mikwala yako ndio unataka tuamini kwamba huishi uswahilini sio?, hii kesi si ilitokea kwenye klinik ya mitaa yenu!
 
Back
Top Bottom