Utu na utoaji!

Ukweli ukibidi kusemwa, usemwe tu. Mi kwa sasa naona napata tabu hata kufikiria. Na siwezi kujikosha kwa kujipa ujasiri hata niliokuwa sina. Nahofia kuja kunifika then nikaenda kinyume na kauli zangu za majigambo. Mungu atunusuru na haya ila jibu nitakuwa nalo endapo kama yatatokea kwa watu wa karibu nami.


Nakubaliana na wewe.
 
Watu wanaogopa hata kutoa damu nini figo. Hasa mtu akijua hajatulia anaogopa asijeambiwa afya haijatulia.
Kutoa figo sawa ila damu kwani mtu atapungukiwa nini??Labda hao unaosema wanaogopa wasijekutwa/julika wana ngoma ndo naweza kuelewa wanachokwepa ni nini!
 
Kwaroho zetu binadamu najua jambo lakujitolea ni gumu sana kuingia akilini linashindikana la vitu kama pesa na chakula. Hadi mtu aone atanufaikaje kwa msaada anaoutoa.
Lizz, michelle mnadhani la viungo vya mwili litakuwa rahisi? Hiyo haipo unless further notes.
 
Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!
Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?

Lizzy! swalilako gumu sana, kirahisi naweza sema nitajitolea, lakini kiukweli itategemea litapotokea.. Watu tunakimbia hata kujitolea damu! kwa figo mmh, tuombe Mungu yasitukute kwani hapo tutatofautisha rangi saba bila mikwaruzo! Mungu epushia mbali.
 
Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!
Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?

nini figo lizzy, watu kujitolea damu tu huwa ni mtihani mkubwa.
 
Kwaroho zetu binadamu najua jambo lakujitolea ni gumu sana kuingia akilini linashindikana la vitu kama pesa na chakula. Hadi mtu aone atanufaikaje kwa msaada anaoutoa.
Lizz, michelle mnadhani la viungo vya mwili litakuwa rahisi? Hiyo haipo unless further notes.

Hivi utajisikiaje kusimama kaburini ukilia huku ukijua fika ungeweza kuisogeza siku hiyo mbele ila hukufanya hivyo??
 
Lizzy! swalilako gumu sana, kirahisi naweza sema nitajitolea, lakini kiukweli itategemea litapotokea.. Watu tunakimbia hata kujitolea damu! kwa figo mmh, tuombe Mungu yasitukute kwani hapo tutatofautisha rangi saba bila mikwaruzo! Mungu epushia mbali.

Hao wanaokimbia hata kutoa damu wananichekesha kweli.Hua wanadhani itaishaa ama?
 
Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!
Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?

...huenda tukawalaumu ndugu wa huyo mheshimiwa, lakini hatujui kimewasibu nini mpaka wamesitisha kutoa huo ushirikiano. Huenda hawajapewa ushauri nasaha unaohitajika kwenye case kama hii. Tunadanganyana na kutishana as if ukijitolea figo yako, siku ukipata mushkeli basi ndio RIP hiyo...

Vile vile, lifestyle zinaweza kuwa zinachangia maamuzi ya hawa wanandugu. Who am I to judge them? ni wao na mwenyezi Mungu wao. Kuna msemo, what goes around comes around. Wenzetu kule India, biashara ya kuuza kidneys imeshamiri sana kiasi cha kupelekea black market ya viungo vya binadamu.

Binafsi na bad experience kipindi mzee wangu anaumwa (Cancer,) alikuwa anahitajika kuongezewa damu mara kwa mara. Kilikuwa ni kipimo tosha kwa wanandugu, jamaa na marafiki tutasaidianaje. Wengi walikuwa wanakimbia hata kutest kama Blood Groups zina match. Wengine siku ya kutoa damu waliingia mitini, na wengine kushawishiwa kwa 'mshiko!' ...Ilibidi baadhi warudie kuchangia damu kukidhi mahitaji ya mgonjwa.

Siku nikikumbwa na mtihani kama huu, Mw'Mungu ataniwezesha nguvu na imani nijitolee figo kuliko kumuona ndugu yangu akiteseka.
 
Juzi kuna kapindi kilinisikitisha kweli!Kuna baba ambae ana tatizo la figo..zimefail kabisa kwahiyo anategemea mashine kuishi!Huyo mzee ana dada na kaka zaidi ya watatu na hamna hata mmoja aliyetaka hata kupima kuona kama wanamatch na ndugu yao achilia mbali kujitolea figo imsaidie!
Ikabidi nijiulize wangapi kati ya ndugu na rafiki zangu wakikutwa na tatizo kama hilo ntakua tayari kujitolea figo yangu moja kusaidia.Wachache ningewapa kwa moyo mkunjufu na wengine ningewapa tu ilimradi!Wewe je?
lIZZY, KUTOA FIGO NI RAHISI KAMA UKO NCHI ILIYOENDELEA, LAKINI KUTOA FIGO TANZANIA YAWEZA IKAWA NDIO MWISHO WA MAISHA YAKO
 
Back
Top Bottom