Utitiri wa Malori umekithiri barabara ya Morogoro, hatua za haraka zahitaji kuchukuliwa, tusisubiri hadi janga litokee

Mchanya

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
976
1,525
Ile wikiendi ya sikukuu ya Nane Nane niliendesha gari kutoka Dar hadi Morogoro na kugeuza baada ya siku kadhaa, na Jumamosi ya juzi pia niliendesha kutoka Dar hadi Chalinze, nilichokiona barabarani nyakati zote, wakati wa kwenda na hata wakati wa kurudi, kilinishtua na kunishangaza sana, idadi kubwa ya malori ambayo sijawahi kuiona kabla.

Ni utitiri wa malori usio wa kawaida, sikuweza kuamini macho yangu kwamba unaweza kupishana na malori hadi 100 yakiwa kwenye msafara.

Ikitokea tatizo dogo katikati ya barabara basi wenye magari mengine ya kawaida watataabika kwa kukaa kwenye foleni isiyo na maelezo. Sina hakika nini kimesababisha hali hii, mwenye kujua atujuze, lakini ni wazi kwamba:

a) Wingi wa malori hayo utaathiri ubora wa barabara
b) Kuna mazingira hatarishi ya ajali na uhalifu kujitokeza barabarani
c) Usafiri kwenye barabara hiyo utasababisha ucheleweshaji na kero kubwa kwa wananchi

Tusingoje hadi balaa litokee ndipo tuchukue hatua, ni muhimu hatua za tahadhari zinahitaji kuchukuliwa SASA.
 
Acha lawama,hujui hapo kwenye hizo lori 100 kuna familia zaidi ya 500 zinafaidika?
 
Ile wikiendi ya sikukuu ya Nane Nane niliendesha gari kutoka Dar hadi Morogoro na kugeuza baada ya siku kadhaa, na Jumamosi ya juzi pia niliendesha kutoka Dar hadi Chalinze, nilichokiona barabarani nyakati zote, wakati wa kwenda na hata wakati wa kurudi, kilinishtua na kunishangaza sana, idadi kubwa ya malori ambayo sijawahi kuiona kabla.

Ni utitiri wa malori usio wa kawaida, sikuweza kuamini macho yangu kwamba unaweza kupishana na malori hadi 100 yakiwa kwenye msafara.

Ikitokea tatizo dogo katikati ya barabara basi wenye magari mengine ya kawaida watataabika kwa kukaa kwenye foleni isiyo na maelezo. Sina hakika nini kimesababisha hali hii, mwenye kujua atujuze, lakini ni wazi kwamba:

a) Wingi wa malori hayo utaathiri ubora wa barabara
b) Kuna mazingira hatarishi ya ajali na uhalifu kujitokeza barabarani
c) Usafiri kwenye barabara hiyo utasababisha ucheleweshaji na kero kubwa kwa wananchi

Tusingoje hadi balaa litokee ndipo tuchukue hatua, ni muhimu hatua za tahadhari zinahitaji kuchukuliwa SASA.
Hio barabara likiharibikaga lori moja hapo kati jua kwamba dar to moro ni masaa kumi
 
Back
Top Bottom