Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Pasco tungemuelewa Mh Mwigulu Nchemba kama angefupisha maelezo kwa kusema "..waungwana, vyeti ni vyangu na nimesoma kama vinavyoonyesha, ila nilirudia shule kwa majina ya mtu mwingine ili kuweza kupata nafasi ya kuendelea na masomo shule ya msingi" ingefaa zaidi
Sasa si alishasema kuwa alikaa nyumbani miaka miwili kuchunga ngombe?
Ina maana aliporudi aliendelea na jina la mtu mwingine
 
Mkuu Mahanju, Mhe. Mwingulu Nchemba ni verified member humu na trusted source hivyo alichosema humu ndio ukweli wenyewe halisi. Wewe ndio unadanganya.
Pasco
Ni ukweli wake na sii lazima uwe ukweli halisi.

Pasco lihurumie taifa acha kumshabikia mwongo.
 
mmh,kasema jina alipewa akiwa na siku saba.

kwa maana hiyo aliitwa tangu akiwa mtoto.

tena anasema baada ya kuambiwa arudi shule baada ya kuacha aliamua kuchukua jina la daktari.

iweje achukue jina ambalo alikuwa nalo tangu akiwa na siku saba?.
tena majina mawili yote,mmh.

anatakiwa aseme kuwa alitumia jina lake lingine ambalo hata akiwa anasoma na alipoacha alikuwa nalo na kuna watu waliomuita hilo jina.

anaposema alichukua la daktari alipoacha,je lile ambalo alipewa akiwa na siku saba ni lingine?.

pia hajasema akiwa darasa la kwanza hadi alipoacha alikuwa anatumia njina gani!!!
 
Nafikiria tu saahizi Paskalii angekuwa NDO msemaji wa pale jumba jeupe kupitia kambi ile ya KUZUNGURUSHA
Mkuu Yohana Mbatizaji utakuwa hujui. Mimi namfahamu Paskali vizuri sana kwa sababu mimi na yeye ni mapacha wa tumbo moja. Msemaji wa pale alikuwa awe ni yule jamaa wa Mtanzania, msaidizi wake ni huyu jamaa wa DW aliyepo, Paskali yeye angekula tuu tenda za production ya vipindi vya TV kupitia kampuni yake ya PPR.
Pasco
 
pasco kama kuna jina bandia basi kuna vyeti feki.,, yeye anatoa historia ya kuzaliwa utadhani alikuepo wakati hsyo matukio ya kuzaliwa na majina aliyopewa kama umesoma Topic moja inaitwa Logic kwenye hesabu sentensi zako nikiunganisha majibu yaleta uwongo na majibu ya mwigulu pia ni uwongo..
 
Mkuu Iparamasa, ni kweli kutumia jina la mtu mwingine ni kufoji ila hayo majina ya Mwigulu Nchemba sio majina ya mtu yoyote ni just given names, kama alivyoeleza mwenyewe, siku mtoto anapoandikishwa shule huwa kuna fomu ya majina ya wazazi, kwenye fomu zile za kumuandikisha shule huyu kijana wa Kinyiramba Lameck Madelu Mkumbo, wazazi wake walimuandikisha kwa majina yao kabisa ya Kinyiramba ila wakaomba utawala wa shule kumuandikisha mtoto wao kwa given names za Nesi wa Kisukuma Mwigulu Nchemba na hapo hakuna jinai yoyote kwa sababu ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mtu unaruhusiwa kutumia jina lolote mfano Pasco wa JF ni Mashokolokubangashe as long as sio impersonation ya Mashokolokubangashe original.
Pasco
Yaani hivyo tu. Na wewe umeridhika.
 
Huja address swali langu kwa nn MTU ana opt Ku acha kutumia majina yake sahihi anatumia bandia? Anaficha nn? Na hayo majina bandia na kiuhalisia ni ya nani au yamepatikanaje?? Mimi ni Osokoni naona umeshanipa jina bandia Mkuu Pasco
Mkuu Osoko, as long as hakuna kosa lolote la jinai kutumia jina lolote, then mtu yoyote yuko huru kutumia jina lolote kujiandikisha popote, ila cheti cha kuzaliwa, kuandikishwa shule, passport na Nida lazima utumie majina halisi ya wazazi, hivyo tusimsakame Mhe. Mwigulu Nchemba , nendeni immigration mkaone DN data zake au Nida.
Pasco
 
Mkuu Jogi, Mhe. Mwingulu Nchemba ni verified member humu hivyo alichosema yeye ndicho ukweli, wewe ni just a pen name kama mimi na unachosema wewe ni uongo wa mchana kweupe! .

NB. Hii mada ni kama ya utani utani lakini tungekuwa nchi za wenzetu hapa kuna mtu akaondoka but not Tanzania. Kwa sababu kutaleta a very bad Precedence na watu kama kina Katto sijui itakuwaje.
Pasco
Mkuu nazidi kuwa na mashaka, haiyumkini account yako imedukuliwa.

Maelezo ya mtuhumiwa unaya classify kuwa ya kweli kwa sababu amesema hivyo!!!!?

Hawa watu "hata kama wanaongelea gizani" (anonymity) wanapaaza sauti kusema "MNADANGANYWAAAA" unapendekeza tukubali tu maelezo rahisi ya "verified user"????

MUNGU ALIMTIMUA SHETANI MBINGUNI, MAANA HAKUNA NAMNA UTAFANYA USHETANI KISA UKO MBINGUNI.

Verification of username haitakuwa na maana kama muhusika anashindwa ku clear tuhuma inayomkabili ya kutudanganya kama taifa.

Amefanya mtihani wa darasa la saba mara mbili kwa manufaa yake!!?
 
Wanabodi,
Katika zoezi la kusaka vyeti bandia, kuna watu wanashindwa kutofautisha kati ya vyeti bandia na majina bandia.

Cheti bandia ni cheti ambacho ama hakipo kabisa hivyo kimetengezwa cheti fake kwa forgery ama ni cheti cha kweli lakini anayekitumia sii mwenyewe mwenye cheti halisi, hivyo kufoji cheti cha mtu mwingine, hili ni kosa kubwa la jinai na huu ni wizi!.

Jina bandia ni kutumia majina ya kuunga unga ambayo sio majina yako halisi, lakini aliyeingia darasani kusoma ni wewe, aliyehitimu ni wewe, hivyo hicho cheti ulichokipata ni cheti halali na sio cheti bandia ila jina ndilo jina bandia.

Nimesoma utetezi wa Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kuhusu tuhuma za kuwa na cheti bandia, nimejiridhisha kabisa tena pasi shaka kuwa vyeti vya Mhe. Mwingulu Nchemba sio vyeti fake ila majina ya Mwigulu Nchemba ndilo jina bandia.

Sio kila jina bandia ni forgery, kuna majina bandia yanayoitwa Nick Names sio forgery bali ni just given names. Given names hizo zinapokuwa registered kwenye vyeti, vyeti hivyo ni halali ila jina la mwenye cheti ndilo jina bandia ambalo halina kosa lolote kisheria.

Uthibitisho huu ni kufuatia utetezi huu wa Mhe. Mwingulu Nchemba umethibitisha jina la Mwigulu Nchemba ni jina bandia la mtu halisi aitwae mwenye given name ya Lameck Madelu Mkumbo ambaye hata majina hayo,hakuna jina lolote la wazazi wake wala jina la ukoo wake, kama anavyojieleza yeye mwenyewe.


Mkuu Mhe. Mwigulu, kwa vile hili bandiko nimelikutia page 33, na sijaweza kusoma mabandiko yate ya nyuma, hivyo siwezi kujua kama ulijibu haya, ila kwanza kwa heshma na taadhima, nakupongeza sana kujitokeza kujibu tuhuma, ila very unfortunately, majibu yako, hayajitoshelezi kabisa!, hakuna kitu chochote ulichojibu hapa, you leave more questions than answers and there is something fishy!.

Majina yana formula ya majina, na hayawezi kuijiibukia tuu hivi hivi, na formula hiyo ni universal, dunia nzima.

Jina lina given name, yaani jina ulilopewa wewe, hili given name linaweza kuwa moja au hata kumi, haijalishi, kwenye given name, ni lile jina unaloitwa, liwe la utoto, ubatizo, etc, Kiingeza linaitwa fast name!.

Jina la pili, ni lazima liwe ni jina la kwanza la mzazi wako, na hapa hakuna excuse, kama mwanzo kwenye given name, umetumia jina la nyumbani, la kilugha, then jina la pili lazima liwe jina la ubatizo, ukitangulia na jina la ubatizo, then jina la pili au liwe ni jina la kwanza, la mzazi wako, au ukitumia fast name ya majina mawili yote ya kwako, then jina la tatu ni lazima liwe ni jina la kwanza la mzazi wako!, na jina la nne ni lazima liwe ni jina la ukoo wenu yaani sir name.

Kwenye majina yako, sijaweza kuona jina la mzazi na jina la ukoo, huwezi kutumia majina yote ya given name bila jina la mzazi na jina la ukoo!.

Naomba wenye acess na immigration, fatulieni DN ya Mhe. Mwigulu Mchemba muone imeandikwaje, kwa sababu bila jina la mzazi na jina la ukoo mtu huwezi kupata passport kwa majina ya kuokotezwa!.

This is the begining of opening a pandora box, we have to reach to the bottom of this, ila asante sana kujitokeza na kujibu, kwa sababu uwongo, ukisemwa sana na kuachwa kurudiwa rudiwa bila kukanushwa hugeuka kuwa ni ukweli.

Kwa kuwasaidia wengine wasio jua, hakuna kosa lolote la jinai kujiita jina lolote la bandia na kuitumia popote.

Japo jina la Mwigulu Nchemba ni jina bandia ila vyeti vyake vyote ni vyeti halali.

Kutumia jina bandia, given name sio kosa kisheria na hakuna jinai yoyote! .

Hata mimi Pasco wa JF naweza kuisajili kama Mashokolokubangashe na nikatambulika kama Mashokolokubangashe na vyeti vyangu vyote vikasomeka Mashokolokubangashe na nikawa sijafanya kosa lolote la jinai, ila ikitokea kwenye ujazaji wa fomu zozote za kisheria kama hati ya kusafiria au cheti cha kuzaliwa lazima nitaonyesha majina halisi ya wazazi wangu, na ikitokea kule nako nimejiorodhesha jina la Mashokolokubangashe kuwa ni moja ya majina ya wazazi wangu, then hivyo inageuka forgery, cheating na ni kosa la jinai.

Hivyo natoa wito kwako wanaomtuhumu Mwigulu kudanga wapate uthibitisho toka NIDA na Uhamiaji, watayaona majina halisi wazazi wa Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba.

Finally, wewe mwana Ilboru mwenzangu, ujege mara moja moja humu jf sio mpaka tuu kuja kujibu tuhuma, na ile shule iliokufikisha hapo uikumbukege!.
NB. Tukilimaliza vizuri hili zoezi la vyeti bandia, tunaweza kuamua kuanzisha msako wa wenye majina bandia, na kisha hata kwenye asili za watumishi wa umma, maana kuna a very interesting story ya kijana mmoja wa kabila la Kihaya, mwenye jina la Katto.
Asante.
Pasco
Rejea, kati ya wagombea wote wa urais wa CCM, Mhe. Mwingulu, ndie aliye ni impress sana kuliko wote kwa kuwa the most genuine kumbe...
Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President ...
Kwanini MTU atumie jina bandia wakati cheti ni sahii acha wehu wako toa mantik hapo ili uajiliwe serikalini nilazima elimu yako ijulikane sasa hapo alitumia jina bandia kwa sababu gani
 
Hilo ndio swali ninalotaka Pasco alijibu.
Mkuu Kisu cha Ngari, nimelijibu hili mara kibao kuwa kuna majina ya aina tatu
1.given names
2. Middle names could be la ubatizo la la mzazi
3. Surname or family name, jina la ukoo.
Bandiko la Mwigulu ameonyesha majina ya Mwigulu Nchemba ni just given, hakuna kosa lolote kutumia given names popote hadi kwenye vyeti, bungeni hadi kwenye passport ila kwenye fomu za kuandikishwa shule majina ya wazazi yapo. Kule Immigration kuna DN file yake yenye majina halisi ya wazazi wake na Nida pia.

Kwa vile hakuna mwenye majina yake ya kuandikishwa, mwenye DN yake au kule Nida kuonyesha wazazi wake ni nani, akikutwa kule amedanganya hapa ndio tutasema mengine ila hata ilitokea akawa amedanganya bado kuna bonge la caveat ya kijana fulani Banyamulenge wa Kihaya kwa jina la Katto.
Pasco
 
Pasco umechanganya mambo kuhusu mfumo au utaratibu wa majina. Kwa sehemu kubwa duniani kuna mifumo miwili ya majina, kuna huu wa nchi za magharibi ambao kutokana na ukoloni ndiyo na sisi tumeurithi na upo wa nchi za mashariki. Huu wa magharibi huwa unaanza na "first name" au kama ukipenda "forename" halafu ukimalizia na "surname" yaani jina la ukoo. Unaweza pia kuwa na jina au majina ya kati "middle name/s". Mfano ni Juma Maharage au Juma Pasco Maharage.
Ule wa mashariki huanza na jina la ukoo halafu likaja la kwako au pengine ukawa na jina la kati. Mfano Wachina; ukisikia anaitwa Xi Jinping basi ujue "Xi" siyo first name bali ndiyo jina la ukoo halafu "Jinping" ndiyo la kwake. Kwa maana nyingine kama Juma Maharage angekuwa Mchina basi angeitwa "Maharage Juma".
Sasa basi utaratibu sahihi hata kwa hapa kwetu kwa mfano ni mtu kuitwa jina lolote la kwanza (first name) au hata la kati (middle name) kama wazazi wake watakavyopenda ila jina la ukoo (surname) linabaki lile lile ambalo linatumika kifamilia. Hili linatakiwa liwe la "kilugha" sababu hakuna ukoo wa Kitanzania au Kiafrika wenye jina la kizungu, yote yanapaswa kuwa ya kikwetu.
Kuna utaratibu mbovu hapa kwetu ambapo mtu anayeitwa kwa mfano "Steven Paul Mkama" anazaa mtoto halafu badala ya kumuita mfano "Judith Mkama" au "Judith Roselyn Mkama" utasikia anamuita "Judith Steven" au "Judith Steven Mkama".
Haya ni makosa maarufu sana. Kwa mfano huu, huyu mtoto ni Judith Roselyn, hayo ndiyo majina yake sahihi. Jina pekee analoazima ni "Mkama" ambalo ni la ukoo. "Steven" na "Paul" hapaswi kabisa kuyatumia kwa sababu haya ni "personal names" za baba yake kama vile yeye alivyo na personal names zake mbili yaani Judith Roselyn. Atakapokuwa anatumia personal name yoyote ya baba yake tayari anapoteza huo ukoo. Hili tatizo linajitokeza mara nyingi mno hapa Tanzania.
Kuhusu "nicknames", haya ni majina ya utani ambayo hayachukuliwi kuwa rasmi, mfano yule beki wa Yanga anayeitwa "Canavarro", hakuna mtu yeyote anayeamini kwamba hilo ndiyo jina lake na wala hawezi kulitumia "officially" popote. Yapo pia majina yanayoitwa "stage names" ambayo hutumiwa sana na wanamuziki au wacheza sinema na wengine huamua kuyatumia rasmi kisheria kama majina yao. Mfano mwanamuziki maarufu wa Uingereza anayefahamika kama "Elton John" jina hili ni stage name ambayo amelirasimisha. Majina yake ya kuzaliwa ni Reginald Kenneth Dwight.
Kwa leo niishie hapa.

Umelonga mkuu!
 
Pasco umetumia criteria gani kusema majina ni universal? Embu Fanya utafiti kuhusu wanaume Wa Java (Indonesia), mbona hawana jina la baba wala ukoo only one given name eg
Suharto
Sukarno
 
pasco eti tena veryfied user humu hawezi kudanganya kama amedanganya kwenye vyeti atashindwa kudanganya Jamii Forum hili nalo linahitaji Elimu kujua kwa mtu aliesoma shule na akafauru vizuri hawezi kutetea majina feki na vyeti bandia kwamba kimoja kipo sahihi kimoja hakipo sahihi..
 
Back
Top Bottom