Ndoa ilikua changa kipindi hicho! Waambie wenye ndoa inayoanzia miaka 8 na kuendelea watatoa majibu mazuri!....
suluhu wanayo wenyewe kwa kukiri mapungufu yao na kusameheana, lakini kumbuka kuna kesi ya ubakaji ambayo mlalamikaji hata akimsamehe mtuhumiwa bado sheria/jamhuri yaweza kuendelea na kesi hapo ndio kwenye changamoto
Mmh mbona kwenye sporah show walsema wako kwenye ndoa 10 yearz sasa tena wakasema wakasema wanatumia simu moja... Da kwel pale maneno tu ya moyon wanayajua wenyewe
Mleta mada ni dada yetu Flora mbasha.. mpeni ushauri wenu..ametingwa
Thanks, kwa mawazo yako...Waza maisha pambana na umasikini, ndoa ikija shukuru! Mabinti tunakosea sana kuweka too much expectation kwenye ndoa! Kwamba itakupa raha ya ajabu, kwamba dhiki zimepata mtatuzi, kwamba utapendwa na kujaliwa kuliko wanawake wote duniani, kwamba maisha yatakuwa fairy tale.
Ukiingia kwenye ndoa ukikuta sivyo lol taharuki na kuchanganyikiwa na kupoteza mwelekeo mzima wa destiny yako! Be Care!
Wachukue kalikizo waende ughaibuni wakazungumze kiutu uzima hope Watapata ufumbuzi
Assume wameindoa kwa hiari yao kwenye macho ya kisheria
Hii kesi ukiipeleka mahakamani ni yule aliyefanyiwa hicho kitendo ndo anastahili kuitoa lakini kwa vile ni kesi ya jinai jamhuri ndo inasimamia kesi hii. Sio rahisi kama unavyosema
Kama mahakama ikijiridhisha alibaka kweli,sheria ifate mkondo wake tu! Nakerwa wanaopenda kumaliza masuala ya ubakaji kifamilia!!!
Kuhusu hiyo ndoa yao,watajua wenyewe,wakiamua kusameheana au kila mmoja ashike njia. Kila mmoja asikilize moyo wake!!!!
Ndoa si lelemama!
Mmh mbona kwenye sporah show walsema wako kwenye ndoa 10 yearz sasa tena wakasema wakasema wanatumia simu moja... Da kwel pale maneno tu ya moyon wanayajua wenyewe
Yaani mambo ya kifamilia yangebidi yamalizike kifamilia. Lakini kwa hili wamechelewa lishafika kwenye mkono wa sheria ashaenda mpakq polisi amefanyiwa uchunguz vipimo vya daktari vimeonyesha hivo. Hapo mahakaman kazi inakuwa ndogo sana labda watoe rushwa kubwa sana. Jamaa ataenda ndani atafungwa miezi michache huku mtaani kutulie then watamtoa kwa faini kama watamalizana kifamilia.