Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Fidel80

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2008
Posts
21,945
Reaction score
4,506
Ndugu zanguni ni kweli pesa ina mvuto wa Mapenzi mpaka ikafikia kipindi mtu ukavutiwa kimapenzi na mtu flani kwa sababu ana pesa? Ni kweli pesa ni moja ya chambo katika mapenzi?

Pesa unaweza ukaitumia kuvuta wapenzi wengi na wakakubali kutokana na pesa yako?
Ni kweli pesa ina mvuto katika penzi kuliko upendo wa moyoni?

Angalia pedeshee huyu hapa chini anavyotumia pesa yake katika mapenzi, huyu jamaa tunaweza kusema aliwadhalilisha hawa mabinti kwa kuwachezea ndimi na kila aina ya uchafu kutokana na njaa zao ya pesa walikubali huku wakikata kilaji.

Wanawake kweli mnakubali kufanyiwa hivi? Angalia warembo walivyo wazuri hao.


Pedeshee Pius Rutta 'Mzee wa Pamba' akibonyeza totoz Msasani Beach club.



Hapo Pedeshee akionekana katika malavidavi.

 
Wanasema hapendwi mtu mkwanja tu ndo unaopendwa duh kwa hali hii basi ndoa nyingi ni za kisanii mtu akifilisika au kufukuzwa kazi hana pesa basi wajanja wataanza kukubebea wife wako....
 
Wanasema hapendwi mtu mkwanja tu ndo unaopendwa duh kwa hali hii basi ndoa nyingi ni za kisanii mtu akifilisika au kufukuzwa kazi hana pesa basi wajanja wataanza kukubebea wife wako....

Kwa kweli Fidel kwa ndoa ambazo hazina mapenzi ya kweli ni utata tu. Huyu alogundua pesa na alaaniwe.
 
Kwa kweli Fidel kwa ndoa ambazo hazina mapenzi ya kweli ni utata tu. Huyu alogundua pesa na alaaniwe.

Bila pesa Mwana huwezi ng'aa lazima mtoto upigwe soap soap ung'ae upelekwe pale Game uchague viwalo shopping ya kufa mtu utamtosa kweli Masanilo hapo bado hajakupeleka show room uchague Vogue mmeo haki ya nani unamsahau...teh teh teh
 
Tamaa ooh nimekupenda ooh nini kumbe umependa kabaloon kake wanawake bana mi nachoka sana nasisitiza hit and run ndo njia pekee angalia hao wasichana wote wanampenda jamaa


hujafikishwa kigoma mwisho wa reli Fidel, mwenyewe utabembeleza ndoa!
 
Fide acha kitu pesa mwana! Ni balaa. Asilimia kubwa ya ndoa zetu za sasa zinaendeshwa na fweza. Mtu anayedai feza sio kila kitu ni mwongo. Muulizeni hata Mwanajamiione atakwambia jinsi jamaa anavyoipenda salary slip yake!
 
Ni ukweli usiopingika kwamba mapenzi ya kweli yapo,lakini pia pesa ina nafasi yake katika mapenzi.Pesa ina nafasi gani katika mapenzi,differs from person to person,na hapa wapo watakao sema kwamba pesa haina nafasi kabisa kwao katika suala la mapenzi,who knows they might be telling the truth.
 
Tamaa ooh nimekupenda ooh nini kumbe umependa kabaloon kake wanawake bana mi nachoka sana nasisitiza hit and run ndo njia pekee angalia hao wasichana wote wanampenda jamaa

Yaani nakwambia ndio maana nikawa nasema itabidi tufanye tafiti juu ya nafasi ya pesa katika mapenzi (kiumweliukweli) kwa sababu hali inatisha kana inafikia hatua wanawake tunakubali kuchanganywa mpaka watatu wanne kisa bwana ana pesa basi ukimwi hautakaa uishe.
 
hujafikishwa kigoma mwisho wa reli Fidel, mwenyewe utabembeleza ndoa!

Kule vipo vitu navyo taka mimi umbo namba 8 weweeee balaa mi kama kawaida yangu siwezi nikafia kwenye kidonda kama Movin pick toto lalipeleka lakini na hit na kurun siwezi nikatangaza ndoa najua ananichuna tu tupo wengi.
 
Fide acha kitu pesa mwana! Ni balaa. Asilimia kubwa ya ndoa zetu za sasa zinaendeshwa na fweza. Mtu anayedai feza sio kila kitu ni mwongo. Muulizeni hata Mwanajamiione atakwambia jinsi jamaa anavyoipenda salary slip yake!

Na nadhani dhana ya wanawake wanapenda wenye pesa imebadilika sasa kwani hata wanaume nao wanapenda ila tu wao wana stara huweziwapanga kama wanataka kulipia Luku.
 
Na nadhani dhana ya wanawake wanapenda wenye pesa imebadilika sasa kwani hata wanaume nao wanapenda ila tu wao wana stara huweziwapanga kama wanataka kulipia Luku.

Mi naona ni umaskini unachangia kama yule dada wa Denish ambaye kuna mwarabu ana mtaka anaomba ushauri...watu tunapenda maisha mazuri kuliko kipato chetu ndo tatizo hapo lilipo ndo maana wengi wanadondokea kupangwa kama wananunua umeme wa luku au wanachukua pesa kwenye ATM.
 
tatizo kwa kiasi kikubwa linachangiwa na hao wanaotanguliza pesa ili kukonga mioyo ya wanawake.Utashangaa mtu anajua kabisa kwamba mwanamke huyo hana hata shida ya hela lakini atajifaragua kujionyesha anazo kwa kutoa ofa za hapa na pale.Kuna thread moja hapa inayozungumzia " unatongozaje" kuna wachangiaji wameshauri kuwa mwaga pesa tu utampata mwanamke!
Ila tukirudi kwenye mada, asikudanganye mtu, pesa inasaidia kurutubisha penzi.Ukiwa huna pesa penzi hilo litafifia upesi sana maana mtafurahia nini bila pesa? unahitaji kutoka kwenda matembezi ( outing), mpeane zawadi, na mambo mengine mengi tu.Ila sishauri mwanaume kumpa mwanamke pesa kwa mtindo wa "kuhonga" au kila mara kutaka yeye tu ndiyo alipie gharama za mapenzi.
 
Ah wapi,,, nao wanapangwa tu,,, ukijipendekeza kabla ya muda ulioambiwa uje unatimuliwa tu. Money talks kila mahali. Na ukizingatia hawa vijana wetu hawana kazi, akibahatika kupewa hako katenda ka kumfurahisha jimama basi hata wawe kumi wao hawajali.
 


Naona WOS tunaweza tukaunganisha na ile ya mzizi kwa asiye na pesa yeye atatumia kimzizi kumpata mwanamke lakini mwenye pesa yeye atamwaga pesa papu jamaa siku ya kwanza hakuna hata mazungumzo anampiga mwanamke na Laki tano weweeeeeeee utazima fegi hata swala la sijui atakuwa na UKIMWI hilo halipo kabisa.
 

Miye nnaogopa penzi la mkopo. Tukimalizana tu nakupa chako,,, tusijuane. Unikopeshe penzi ili uje uchukue nyingi zaidi. No nooooooooooo, hapana!
 

Mimi huwa nahisi kuwa wale wanaoishi maisha ya chmi vijijini huwa wana maisha mazuri ya kindoa than walioko mjini au huwa nakosea? Kuna wakati huwa natamani kama ningekuwa huko katika hali hiyo yaani nisiwe na ufahamu wa mambo ya pesa kwa kiasi hiki cha kimjini ningekuwa na raha sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…