Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Ebo!
Penzi la mkopo ndo lipi hilo?
Mi naogopa sana demu kila ukimpa kazawadi,,, eti ah acha tu mpenzi, ukimpa hela akajinunu chochote hataki eti hakuna shida. Ngoja siku anataka kuchukua,,, Oh honey unajau yule shangazi wa mama mkubwa kule Kigoma anaumwa sana anatakiwa kupelekwa mhimbili kwa matibabu na ma mkubwa hayuko mi ndo niko na wananitegema mimi tu. Hata hivyo nilienda benki nikakuta kuna foleni sana na nataka niondoke sasa hivi nimeuliza precission wamenambia tiketi zipo na ntachukulia pale pale airport.
Mwanaume umeunganishiwa hata majibu hujatoa,,,,
Anaendelea,,,, nimewaambia kuwa wamtayarishe mi nikifika tu nageuza na ndege ya jioni hivyo nitamleta kwa ndege! Du
Ukifikiria mkopo ulopewa wa MAPENZI unajikuta unauliza kinyonge kwani shs ngapi dear?
Kwa haraka haraka tu kama m1unusu itatosha,,,,, We hapo ndo utajua ka ulikuwa DECI ama Upatu,,,, Kaazi kwelikweli